Friday, May 15, 2015


Nawaleta hawa kwenu

Thursday, May 14, 2015

Watch this my fans if you like you can comment on this


KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, wanafunzi wa shule za msingi za Mwangaza na Ngarenaro, juzi walidaiwa kupata kipigo kutoka kwa vijana waliojiita ‘Makamanda’ wa umoja wa vyama vya siasa vya upinzani ujulikanao kama Ukawa, baada ya baadhi yao kufika katika mkutano huo uliofanyika viwanja vya karibu na shule yao.
 
Baadhi ya viongozi wakuu wa umoja huo, akiwemo mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu, Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi) na Mbunge wa Arusha Mjini kwa tiketi ya Chadema, Godbless Lema, walishuhudia kitendo hicho, lakini cha kushangaza hawakuchukua hatua yoyote ya kuwazuia vijana hao kuwachapa watoto mijeledi kwa kisingizio kuwa hawakustahili kuwepo uwanjani hapo.
 
Hatua hiyo imekuja licha ya kuwa umoja huo ulikuwa unafanya mkutano wake katika eneo la shule ya Msingi Ngarenaro, uwanja ambao hutumika na shule za msingi za Ngarenaro na Mwangaza pamoja na shule ya Sekondari ya Ngarenaro.

Tuesday, May 12, 2015

 BEN POL KUJA NA REMIX YA SOPHIA KUTOKA CONGA MUSIC...
 
 Waweza pia kucheki na kudownload video kutoka kitaa kwetu blog

Wednesday, May 6, 2015


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki moon amelaani vikali shambulizi la waasi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambalo limeuwa wanajeshi wawili wa umoja huo ambao wanatoka Tanzania.
Wanajeshi wa Umoja wa Mataifa wakifanya doria Mashariki mwa Kongo
Shambulizi hilo lilifanywa Jumanne jioni katika kijiji cha Kisiki, umbali wa km 38 Kaskazini mwa mji wa Beni. Mbali na wanajeshi wawili waliouawa na 13 ambao walijeruhiwa, wengine wapatao 4 hawajulikani walipo.
Wanajeshi wa Tanzania ambao ni sehemu ya kikosi maalumu cha kuingilia kati walikuwa wakifanya doria walipofanyiwa shambulizi hilo na watu wanaoaminika kuwa waasi wa Allied Democratic Forces (ADF) kutoka Uganda.

Sunday, May 3, 2015

Tarehe May 3, 2015
Bomu lajeruhi watu watano mkoani Morogoro.
Bomu lajeruhi watu watano mkoani Morogoro.
Vijana wawili wanatafutwa na jeshi la Polisi mkoani Morogoro kwa kumrushia bomu dereva wa gari la mwenyekiti  wa Halmashauri ya wilaya ya Kilombero, David Ligazio ,Novatus Ngope (47), pamoja na kujeruhi watu wengine wanne walipokuwa kwenye sherehe za Siku ya Wafanyakazi Duniani juzi.
Bomu hilo liliwajeruhi watu hao walipokuwa kwenye maadhimisho hayo yaliyofanyika katika kijiji cha Msolwa Ujamaa, Kata ya Sanje ,wilayani Kilombero, mkoani Morogoro
Kwa mujibu wa Mkuu wa wilaya ya Kilombero, Lephy Gembe alithibitisha kutokea tukio hilo  na kusema tukio hilo lilitokea majira ya saa 2:00 usiku wa Mei Mosi mwaka huu eneo la Kijiji cha Sanje.
Alisema vijana wawili wanaotuhumiwa kurusha mlipuko huo baada ya kuwajeruhi watu hao watano, walifanikiwa kukimbia kutoka eneo la tukio na jeshi la  Polisi inaendelea kuwasaka ili sheria ichukue  mkondo wake.

Tarehe May 2, 2015
44
Mwanamuziki Naseeb Abdul, na mrembo Zari wakiingia ukumbini
22
Wanamuziki Nay wa Mitego na Shetta wakiwa katika pozi
11
Mwanamuziki Diamond akifanya majonjo kwa mama kijacho wake Zari
1111
Baadhi ya warembo waliotoa huduma katika hafla hiyo
5545
Baadhi ya warembo waliotoa huduma katika hafla hiyo

Tarehe May 2, 2015
Mwanamuziki Peter Okoye katika pozi
Mwanamuziki Peter Okoye katika pozi
Wanamuziki nchini Nigeria, Peter na Paul Okoye, wamekuwa wakikwaruzana mara kwa mara kiasi cha kuwashangaza watu kuwa iwaje ndugu wa damu wanakosana wakati wanafanya kazi kama timu.
Hatua hiyo imepelekea Peter, kuweka wazi kuwa, kugombana kwao kusichukuliwe kama kitu cha ajabu kwani nao ni binadamu hivyo kukosana kupo na hakupingiki.
Amesema kuwa kutofautiana kwao ni jambo la kawaida na imekuwa ikitokea hivyo mara nyingi lakini baadaye maisha yanaendelea.
Ameongeza kuwa huwa inatokea kutofautiana kwa hapa na pale kama walivyo binadamu wengine na baadaye kumaliza tofauti zao na kufanya kazi.
Amesema kuwa wao ni kama wanandoa walioishi kwa zaidi ya miaka 20 hivyo kukosana kupo na kama binadamu hupatana na kupanda jukwaani kufanya makamuzi kama kawaida bila watu kujua kama wamegombana.

Tarehe May 3, 2015
Msanii wa filamu nchini Tanzania, Weru Sengo katika pozi
Msanii wa filamu nchini Tanzania, Weru Sengo katika pozi
Wasanii Steve Nyerere na Weru Sengo, katika pozi
Wasanii Steve Nyerere na Weru Sengo, katika pozi
Msanii wa filamu nchini Tanzania, Weru Sengo anadaiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na msanii mwenzake Steve Nyerere, ambapo wamekuwa wakionekana sehemu mbalimbali wakila bata.
Inadaiwa kuwa badala ya kutoka katika matembezi au kula bata na mke wake, Steve, amekuwa akitoka na Weru, jambo ambalo watu wameona sio la kulifumbia macho na inadaiwa kuwa hata katika shoo ya Zari, walikuwa wote na kumuacha mke wake.
Vyanzo hivyo vimedai kuwa Steve, aweke bayana kama ameamua kuoa mke wa pili bila kumshirikisha mke wake kabla hawajamfanyia maandamano kama wanawake kutokana na mke wake kuwa mvumilivu na mtu anayejiheshimu.
Chanzo hicho kimetoa wito kwa mke wa Steve kumpenda mume wake zaidi ya mwanzo, kama amesikia au kuona kitu ni kawaida kwenye ndoa kupata majaribu, hivyo asimame kama mama na kudai kuwa lazima kama mke anajua udhaifu wa mume wake na kumtaka amkamatie hapo kwenye udhaifu bila kusahau kumuomba Mungu.
Kwa mujibu wa mke wa Steve, Suzy Cleo, amesema kuwa anashukuru kwa ushauri alioupata kutoka cha chanzo makini na kudai kuwa atahakikisha kuwa hatatikisika kama mwamba wa mlima Sayun

Rio Ferdinand akiwa na mkwewake Rebecca Ellison enzi za uhai wake
Rio Ferdinand akiwa na mkwewake Rebecca Ellison enzi za uhai wake
Rebecca Ellison ambaye alikuwa ni mke wa mlinzi wa zamani wa klabu ya Manchester United na timu ya taifa ya Uingereza Rio Ferdinand amefariki dunia baada ya kusumbuliwa na maradhi ya kansa kwa muda mfupi.
Rebecca alizaa watoto watatu na Ferdinand, watoto wao wanafahamika kwa majina ya Lorenz, Tate na Tia.
Habari hizi zimemdhoofisha Ferdinand wakati huu mgumu wa ligi kuu ya soka Uingereza, Ferdinand kwa sasa anapambana kwenye kikosi chake cha Queens Park Rangers kuhakikisha kinasalia kwenye likgi kuu kwa msimu ujao.

Tarehe May 1, 2015
Pacquiao (kushoto) akiwa na Mayweather na rekodi zaokwa pamoja
Pacquiao (kushoto) akiwa na Mayweather na rekodi zaokwa pamoja
Kuelekea pambano la ndondi la kukata na shoka kati ya Floyd Mayweather Jr dhidi ya Manny Pacquiao ‘Pac Man’ kuna orodha ya mabondia watano ambao kwa nyakati tofauti wamewahi kupambana na Mayweather na Pacquiao.
Na hivi ndivyo namna ambavyo kila mmoja aliwashinda wapinzani hao.
OSCAR DE LA HOYA
Mayweather alishinda, ilikuwa ni mwaka 2007
Pacquiao alishinda, ilikuwa ni mwaka 2008
Kwa mujibu wa wachambuzi wa mchezo huo wanasema kuwa, Pacquiao alishinda kwa mbinu bora zaidi.
Floyd Mayweather akimchapa konde la maana usoni mpinzani wake Oscar de la Hoya
Floyd Mayweather akimchapa konde la maana usoni mpinzani wake Oscar de la Hoya
Manny Pacquiao akimchakaza pia De La Hoya na kumsababishia kustaafu masumbwi rasmi
Manny Pacquiao akimchakaza pia De La Hoya na kumsababishia kustaafu masumbwi rasmi
RICKY HATTON
Mayweather alishinda kwa Techinical Knock Out mwaka 2007, tarehe 10
Pacquiao alishinda kwa Knock Out tarehe , 2009
Katika hili pambano Pacquiao anapewa faida kwa kushinda kwa ubora zaidi ya Mayweather
Hapa anasema; “Bado narudia kwa kusema kuwa Floyd anatakiwa kujifunza zaidi namna ya kumpiga huyu”, De La Hoya.
Mayweather akipambana na Ricky Hatton
Mayweather akipambana na Ricky Hatton
Pacquiao akionekana kumchakaza Ricky Hatton kiasi cha kupoteza fahamu kabisa katika mzunguko wa pili tu
Pacquiao akionekana kumchakaza Ricky Hatton kiasi cha kupoteza fahamu kabisa katika mzunguko wa pili tu
JUAN MANUEL MARQUEZ
Mayweather alishinda mwaka 2009
Pacquiao alidroo mwaka 2004
Pacquiao alishinda mwaka 2008
Pacquiao alishinda kwa pointi za majaji 2011
Pacquiao alipoteza kwa Knock Out katika raundi ya 6 mwka 2012
Hapa karata imemuangukia Mayweather.
Mayweather akipambana na Manuel Marquez
Mayweather akipambana na Manuel Marquez
Marquez alimpa Pacquiao wakati mgumu sana, lakini alisubiri mpaka pambano la mwisho kati ya mapambano 4 kumshinda Pacquiao
Marquez alimpa Pacquiao wakati mgumu sana, lakini alisubiri mpaka pambano la mwisho kati ya mapambano 4 kumshinda Pacquiao
SHANE MOSLEY
Mayweather alishinda mwaka 2010
Pacquiao alishinda mwaka 2011
Mayweather akimuadhibu Mosley
Mayweather akimuadhibu Mosley
Mosley akipokea kichapo toka kwa Pacquiao
Mosley akipokea kichapo toka kwa Pacquiao
MIGUEL COTTO
Mayweather alishinda mwaka 2012
Pacquiao alishinda mwaka 2009
Mayweather vs Pacquiao: kwenye pambano hili Pacquiao alionekana kushinda kwa mbinu bora zaidi ya Mayweather.
Miguel anasema: “Manny ana kasi na nguvu. Manny yuko bora zaidi ya Mayweather”
Miguel Cotto akimtundika konde Mayweather kabla ya kushindwa katika raundi ya mwisho kabisa ya mchezo
Miguel Cotto akimtundika konde Mayweather kabla ya kushindwa katika raundi ya mwisho kabisa ya mchezo
Pacquiao akizichapa dhidi ya Cotto
Pacquiao akizichapa dhidi ya Cotto

Saturday, May 2, 2015


iunasikitishasana
KWANZA KABISA WANAANZA TOA JENEZA LA ALIEKUFA KWA UGONJWA NA KUZANIWA AMEROGWA NA ALIYEZIKWA AKIWA HAI MAANA KATIKA KABURI HILO WALIZIWA WATU WAWILI KATIKA KABURI MOJA  ALIE HAI NA MFU
JENEZA LA ALIEKUFA KWA UGONJWA TAYARI LIMETOLEWA HILO PEMBENI SASA ANAFUKULIWAALIEZIKWA HAI
MWILI WA ALIEZIKWA AKIWA HAI SASA UNATOLEWA KABURINI

  1. Ujerumani imetuma meli mbili za jeshi lake la wanamaji katika juhudi za kuokowa wakimbizi wasipoteze maisha yao katika bahari ya Mediterenia wakati wakikimbilia barani Ulaya kutafuta maisha bora.
  2. Meli ya kivita ya usaidizi Berlin na manowari Hessen za Ujerumani.
  3. Meli ya kivita ya usaidizi "Berlin" na manowari "Hessen" za Ujerumani.
  4. Meli hizo mbili meli ya kivita ya usaidizi yenye jina la Berlin na manowari inayoitwa Hessen zimeondoka hapo Ijumaa (1.05.2015) katika eneo la Pembe ya Afrika kwa kupitia Mfereji wa Suez nchini Misri kabla ya kuingia bahari ya Mediterenia.
  5. Msemaji wa jeshi la wanamaji la Ujerumani mjini Rostock ameliambia shirika la habari la Ujerumani dpa kwamba meli hizo mbili ilikuwa zinatarajiwa kutia nanga huko Souda katika kisiwa cha Ugiriki cha Crete hapo Jumamosi(02.05.2015).
  6. Amesema meli hizo zitatumika kusafrisha chakula na mablanketi kwa ajili ya wakimbizi wanaohatarisha maisha kukimbilia Ulaya kwa kupitia bahari ya Mediterenia ambapo wiki chache zilizopita mashua moja iliokuwa imebeba wahamiaji kutoka Libya ilizama na kuuwa takriban watu 800.

Friday, May 1, 2015

Saudi Arabia imesema majeshi yake yamewauwa na waasi wa Yemen waliofanya shambulizi lao la kwanza kubwa dhidi ya nchi hiyo tangu kuanza mwezi uliopita mashambulizi ya angani yanayoongozwa na Saudia
Wizara ya ulinzi ya Saudi Arabia imesema wanajeshi wake watatu pia waliuawa katika mapambano hayo baada ya waasi wa Houthi kuvilenga vituo vyao vya uangalizi, wakati jeshi lake likijaribu kuzuia shambulizi hilo.
Kumekuwa na makabiliano hapo kabla lakini hii ni mara ya kwanza ambapo jeshi la Saudi Arabia limeripoti kuhusu shambulizi kamili la waasi wa Houthi katika mipaka yake. Katika mji mkuu Sanaa, mashambulizi mapya ya kutokea angani yanayoongozwa na Saudia yamefanywa katika uwanja wa ndege ikiwa ni siku chache tu baada ya ndege za kivita kuilipua njia ya ndege katika uwanja huo ili kuzuia ndege moja ya Iran kutua.
Wakati huo huo, mawaziri wa mataifa ya Ghuba hapo jana walipinga pendekezo la kuandaa mazungumzo katika nchi isiyounga mkono upande wowote katika mzozo wa kisiasa nchini Yemen, wakati ripoti ya watalaamu ikisema kuwa Iran imekuwa ikiwapa silaha waasi wa Houthi tangu mwaka wa 2009.

Wednesday, April 29, 2015




Indonesia imewauwa wasafirishaji nane wa madawa ya kulevya siku ya Jumatano, wakiwemo raia saba wa kigeni, hatua iliyolaaniwa vika nya Australia na Brazil, zilizojaribu kuwaokoa raia wake bila mafanikio.
Indonesia imetete hatua yake hiyo ikiitaja kuwa ni muhimu katika mapambano dhidi ya madawa ya kulevya, na kusema haina wasiwasi kuhusiana na hatua zilizochukuliwa na Australia kufuatia mauaji hayo, ilizozitaja kuwa ni hisia za muda ambazo hazitadumu zaidi ya miezi mitatu.
Australia ilimuondoa balozi wake kutoka Indonesia kupinga mauaji hayo yaliyofanyika saa sita za usiku, lakini rais wa Indonesia Joko Widodo amesema alikuwa akitekeleza tu sheria dhidi ya wasafirishaji wa madawa ya kulevya.
Watuhumiwa hao -- wawili kutoka Australia, moja kutoka Brazil na wanne kutoka Nigeria -- waliuawa kwa kupigwa risasi pamoja na Muindonesia moja, licha ya kelele za mataifa ya kigeni na maombi ya huruma kutoka kwa wanafamilia wao.


Maelfu ya maafisa wa polisi nchini Marekani wameamriwa kuwasaidia maafisa waliozingirwa mjini Baltimore, baada ya ghasia zilizosababishwa na waandamanaji waliojawa na hasira, kufuatia kifo cha Mmarekani mweusi.
Muandamanaji akiwafokea polisi waliokuwa wanajaribu kudhibiti hali mjini Baltimore
Watu 27 wametiwa nguvuni huku polisi 15 wakijeruhiwa wakati waandamanaji hao wengi wao wanafunzi waliokuwa wanarusha mawe na kupora biashara za watu, walipopambana na maafisa wa polisi.
Ghasia mjini Baltimore zilianza baada ya mazishi ya kijana Mmarekani mweusi kwa jina Freddie Gray, aliyekuwa na miaka 25 na aliyefariki tarehe 19 mwezi wa Aprili kufuatia majeraha mabaya ya uti wa mgongo aliyoyapata wakati alipokuwa anatiwa nguvuni na maafisa wa polisi.


Chama tawala nchini Afrika Kusini African National Congress ANC kimelaani wimbi la mashambulizi dhidi ya raia wa kigeni ambayo yamesababisha vifo vya watu sita na kusababisha hali ya wasiwasi nchini humo
Taarifa kutoka kwa chama cha ANC imesema katika kipindi cha majuma kadhaa sasa, taifa la Afrika Kusini limeghubikwa na wimbi la mashambulizi ya kufedhehesha yanayowalenga raia wa kigeni kutoka nchi nyingine za Afrika.
ANC imeyataja mashambulizi hayo vitendo vya kihalifu dhidi ya watu wanyonge ambao wanatafuta hifadhi, faraja na kujiendeleza kiuchumi na kuongeza raia wa kigeni hapaswi kulaumiwa kwa changamoto zinazowakumba raia wa Afrika Kusini.
Katika mji wa kusini mwa nchi hiyo wa Durban mashambulizi yaliyochochewa na chuki dhidi ya wageni yamezilenga biashara na makaazi ya raia wa kigeni wakiwemo kutoka Somalia, Ethiopia na Malawi licha ya polisi kuimarisha doria katika mji huo kuzuia mashambulizi hayo.
Rais yuko kimya
Taarifa hiyo kutoka kwa ANC inakuja baada ya shutuma kuwa Rais Jacob Zuma ameshindwa kutoa tamko hadharani kuyalaani mashambulizi hayo. Mapema mwaka huu, raia wa kigeni pia walishambuliwa na maduka yao kuporwa katika kitongoji cha Soweto kilichoko karibu na mji wa Johannesburg.
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma
Mashirika ya kutoa misaada yamesema zaidi ya raia 2,000 wa kigeni wameutoroka mji wa Durban wakihofia maisha yao na sasa wanaishi katika kambi za muda chini ya ulinzi wa polisi na iwapo mashambulizi hayo hayatasitishwa,idadi ya waathiriwa inatarajiwa kuongezeka.
Mhamiaji mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Johnny ambaye ni raia wa Zimbabwe anasema anatafakari kurejea nyumbani
Jana maduka mengi yalifungwa katikati mwa mji wa Johannesburg baada ya wafanyaibishara kuhofia ghasia zitazuka baada ya vitisho kusambazwa katika mitandao ya kijamii.
Msumbiji imetangaza inapanga kuwasaidia raia wake walioko Afrika Kusini kurejea nyumbani baada ya waziri wa habari wa Malawi Kondwani Nankhumwa kusema wanawarejsha nyumbani raia wao 400 waliochomewa nyumba na mali zao. Malawi ndiyo nchi ya kwanza ya Afrika kuwaondoa raia wake kutoka Afrika Kusini.
Mfalme anashutumiwa kuchochea chuki
Mfalme Goodwill Zwelithini kiongozi wa kabila kubwa zaidi nchini Afrika Kusini la kwa Zulu Natal anashutumiwa kwa kuchochea mashambulizi hayo baada ya kutoa hotuba wiki mbili zilizopita akiwataka raia wa kigeni kufunga virago na kurejea makwao.
Baadhi ya waafrika Kusini wakikabiliana na raia wa kigeni mjini Durban
Mwakilishi wa mfalme huyo Thulani Zulu amekanusha kuwa mfalme huyo ndiye aliyechochea mashambulizi hayo na kuongeza kuwa amesikitishwa na yanayojiri na anayalaani .
Wanaharakati wanaopinga chuki dhidi ya raia wa kigeni wanapanga maandamano makubwa mjini Durban hii leo kuishinikiza serikali kuchukua hatua zaidi kuwalinda wahamiaji. Polisi Afrika Kusini imesema imewakamata watu74 kuhusiana na mashambulizi hayo.
Raia wa Afrika Kusini ambao hawana ajira wanawashutumu wageni kuwa wanachukua nafasi zao za kazi. Mwaka 2008, watu 62 waliuawa katika mitaa ya Johannesburg kutokana na chuki hizo dhidi ya wageni.

Juhudi za kukabiliana na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi nchini Tanzania zinapata nguvu mpya kupitia kampeni mbalimbali zinazolenga kuhamasisha jamii kupinga vitendo hivyo vya kinyama.
Watoto wenye ulemavu wa ngozi katika shule ya msingi ya Mitindo.
Pamoja na kampeni kadhaa zilizoanzishwa, siku ya Jumapili (tarehe 15 Machi) kulitarajiwa kuzinduliwa kampeni nyingine inayotumia kombe maalumu litakalozungushwa nchini kote kutuma ujumbe wa amani na kupinga mauaji ya albino.
Kampeni hii inazinduliwa katika wakati ambapo jeshi la polisi likitangaza kuwatia mbaroni zaidi wa waganga wa kienyeji 55 wanaotuhumiwa kupiga ramli zinazochonganisha watu ikiwamo zile zinazochochea mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi.

Tuesday, April 21, 2015






Serikali imerejesha mafunzo ya madereva kila baada ya miaka mitatu wakati wa kumalizika kwa muda wa leseni zao, huku ikifafanua kuwa elimu watakayoipata ina umuhimu katika kazi zao, kutokana na mabadiliko mbalimbali yanayotokea katika sekta hiyo.

 

Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Makongoro Mahanga, alitangaza uamuzi huo wa Serikali jana katika mkutano kati yake na viongozi wa madereva wa mabasi nchini.

 

Mkutano huo umefanyika kama ilivyoahidiwa na Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka, wakati alipokuwa akijitahidi kumaliza mgomo wa madereva uliofanyika Aprili 10 mwaka huu, wakati walipokuwa wakipinga pamoja na mambo mengine, sharti la kwenda shule ili kupata leseni mpya.

 

Madereva hao walitaka Serikali ifanyie marekebisho Sheria ya Usalama Barabarani, kwa kuondoa kipengele kinachowataka madereva kwenda Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kwa mafunzo ya muda mfupi kila wakati leseni zao zinapoisha, ili kupata sifa ya kupata leseni nyingine.

 

Sababu ya kupinga kupata mafunzo, ilidaiwa kuwa utaratibu huo uliotangazwa Machi 30, mwaka huu, ulianzishwa bila kushirikisha madereva katika kuuandaa.

 

Pia walipinga kutakiwa kujilipia gharama za shule hiyo ambazo walidai ni Sh 560,000 kwa magari ya kawaida na Sh 200,000 kwa magari ya abiria.

 

Sababu nyingine iliyochangia wapinge shule hiyo, walidai ni kukosekana kwa mikataba ya ajira, inayoweza kuwahakikishia kulindwa kwa kazi zao hadi wanapomaliza mafunzo.

 

Madai mengine yaliyokuwa nje ya shule hiyo, madereva hao walitaka kuondolewa kwa faini ya Sh 300,000 kwa kila kosa la barabarani na kuitaka Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchikavu (Sumatra), kuhakiki uhalisia wa dereva anayeandikishwa na mmiliki wa chombo husika.

 

Majibu ya Serikali Mahanga aliyekuwa Mwenyekiti wa kikao hicho, alisoma tamko la Serikali lililoeleza kuwa pamoja na kurejesha mafunzo hayo, utekelezaji wake hautafanyika mara moja kwa kuwa Kanuni zake hazijakamilika.

 

“Tangazo hili (la kwenda shule) limetolewa kwa kuzingatia umuhimu wa mafunzo kazini kwa wafanyakazi na madereva kama ilivyo kwa wafanyakazi wengine,” alisema Mahanga.

 

Alisisitiza kuwa baada ya miaka mitatu ya leseni, dereva atatakiwa kupata mafunzo mafupi, ambayo ni kati ya siku tatu hadi saba na atakayegharimia mafunzo hayo ni mwajiri, si mfanyakazi na ni katika chuo chochote kinachotambulika.

 

Akifafanua, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani, Mwamini Malemi aliyekuwepo katika mkutano huo, alisema mitaala ya mafunzo hayo bado inaandaliwa, hivyo si rahisi Kanuni hiyo kuanza kutekelezwa mwaka huu hata kama zitakamilika.

 

Kuhusu mikataba ya ajira ambayo ililalamikiwa mno na madereva wakati wa mgomo, Mahanga alisema Serikali itapitia upya mikataba hiyo ili kuhakikisha mambo yote muhimu yanazingatiwa.

 

Akiongezea hoja katika suala la mikataba, Malemi alisema ni lazima mikataba iwe imekamilika kabla ya kuanza kutumika kwa kanuni ya kwenda shule, ili ioneshe wajibu wa mwajiri katika kumsomesha mfanyakazi.

 

Kuhusu kauli iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova ya kuondoa tochi za kupima mwendo kasi barabarani, Mahanga alisema matumizi ya tochi zinazotumika kupima mwendo kasi na ratiba ni sehemu ya utekelezaji wa Sheria za Usalama Barabarani.

 

Hoja nyingine Katika kikao hicho mbali na hoja zilizosababisha mgomo, kulikuwa na hoja nyingine zilizowasilishwa, ikiwemo changamoto ya madereva kupata maelekezo yanayokinzana kutoka Jeshi la Polisi na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchikavu na Majini (Sumatra), kuhusu ratiba ya kuondoka wanakotoka na kuwasili wanakokwenda.

 

Akitoa majibu ya Serikali, Mahanga alisema amepokea hoja hiyo na ataifanya utafiti wa kina. Katika hoja ya kuwataka waajiri kuongeza posho za kazi, Mahanga alisema Serikali haiwezi kupanga posho za madereva katika kikao hicho, kwasababu kila mwajiri ana uwezo wake kulingana na safari za gari yake.

 

Hata hivyo, aliahidi kufanyika utafiti suala hilo katika nchi nyingine, ili aone namna ambavyo madereva wengine wamekuwa wakilipwa posho.

 

Serikali pia imeahidi kuimarisha ukaguzi sehemu za kazi kwa kushirikiana na Sumatra, utakaohusu wamiliki wa magari na kuhuisha mfumo wa kumbukumbu, utakaoonesha kila gari na dereva wake halisi na kuweka vitambulisho vya dereva katika kila gari analoendesha.

 

Mahanga alisema Serikali pia itaweka utaratibu mpya ambapo dereva mwenyewe atajiwekea bima ya ajali itakayoanzishwa na kujiunga na vyama vya wafanyakazi, ili watetee mikataba yao ili iweke pia maswala ya bima hizo.

 

Alisema pia Serikali imeanzisha Mfuko wa Fidia ya Wafanyakazi, ambao utaanza hivi karibuni, ambao mwajiri atawajibika kuchangia.

 

Chama cha Wafanyakazi  Kuhusu chama cha wafanyakazi, Mahanga alisema Serikali imepokea pendekezo la kusaidia madereva kuunda chama cha wafanyakazi chenye nguvu, ambapo alisema kumbukumbu zinaonesha madereva wana vyama vilivyosajiliwa kwa Msajili wa Vyama vya Wafanyakazi na Waajiri.

 

Alitaja vyama hivyo kuwa ni Umoja wa Wafanyakazi wa Mawasiliano na Usafiri Tanzania (COTWU), kilichosajiliwa mwaka 2000 na Chama cha Wafanyakazi cha Usafiri wa Barabara (TARWORTU) kilichosajiliwa mwaka 2013.

 

“Katika kushughulikia changamoto za wafanyakazi na mwajiri wote mnategemeana, jambo mtakalofanya ni kuanzisha majadiliano kupitia vyama vya wafanyakazi lakini kwanza muwe ndani ya vyama,” alisema Mahanga.

 

Wanung’unika  Baada ya kusomwa kwa tamko hilo la Serikali, Katibu Mkuu wa Vyama vya Madereva Tanzania, Mwanarashidi Salehe, alisema mafunzo wanayotakiwa kuchukua hayana tija yoyote, kwa kuwa wakufunzi ni wa kizamani na pia magari yanayotumika ni ya kizamani, ambayo hayaongezi chochote katika kazi yao.

 

“Kwanza hakuna kipya katika mafunzo hayo, mimi nimehudhuria mara mbili....pili katika kikao hiki tulitarajia tutakutana na wamiliki wa magari ambao ndio waajiri wetu ili waseme waliyonayo juu yetu na sisi tuseme yetu tujadiliane na kupata majibu,” alisema Salehe.

 

Mwenyekiti wa chama hicho, Clement Masanja alisema mikataba waliyonayo madereva ni dhaifu mno, haioneshi mambo ambayo dereva atanufaika nayo.

 

“Tulitarajia katika kikao hiki tutatoka na majibu ya posho za madereva, ili dereva ajue atalipwa kiasi gani kwa safari za ndani na nje ya nchi kwa sababu anavyolipwa ni manyanyaso matupu,” alisema Masanja.

Sunday, April 19, 2015


 wewe  ni  dereva  wa basi la abiria ama  gari  binafsi ?hebu  chukua  hatua ya  kupunguza ajali  leo kwa kujihadhari na  kona  hizi na Iyovi na Kitonga na  kona  nyingine kali kama  hizi nchini kwani maisha  yako ni  dhamani  kubwa na uhai  wake bado tunautamani
 Vema  kuheshimu alama  za barabarani na  kuacha mbwembwe  uwapo  barabarani katika kona kali kama hizi
 Katika kona  kama  hizi  zingatia  alama  za usalama  barabarani  usiwe na haraka  ya  kulipita gari la mbele