Saturday, November 28, 2015

Rais wa Uturuki Rcep Tayyip Erdogan ameonyesha kujuta kwamba Uturuki iliidungua ndege ya kijeshi ya Urusi karibu na mpaka wa taifa hilo na Syria,lakini hakuomba msamaha kwa tukio hilo.
Aliuambia mkutano wa hadhara huko Balikesir kwamba alitamani kwamba tukio hilo halingetokea na kwamba halitarudiwa tena.
Rais wa Urusi Vladmir Putin amekataa kulijadili swala hilo na Erdogan hadi atakapoomba msamaha.
Moscow inapanga kuiwekea vikwazo vya kiuchumi Uturuki na tayari imeanza kupitia safari za watalii.
Uturuki imewaonya raia wake kutosafiri Urusi kwa dharura.