Saturday, October 31, 2015

FULL-TIME: #LFC defeat Chelsea Football Club 3-1 at Stamford Bridge thanks to a Philippe Coutinho brace and a goal from substitute Christian Benteke.




Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wabunge ambao wataingia Bungeni baada ya uchaguzi Mkuu uliofanyika nchini kote Oktoba 25, 2015 ni kama ifuatavyo. 
Idadi kubwa ya wabunge hao ni kutoka chama tawala cha CCM, ikifuatiwa na Chadema na CUF na vyama vingine kama NCCR-Mageuzi na ACT-Wazalendo.
WABUNGE WALIOSHINDA KUPITIA CCM
Jimbo la Busega (Raphael Chegeni), Nyamagana (Stanslaus Mabula), Msalala (Ezekiel Maige), Ngara (Alex Gashaza), Kigamboni (Faustine Ndugulile), Kishapu (Suleiman Nchambi) na Kisarawe (Suleiman Jaffo).
Majimbo mengine ni Bagamoyo (Dk Shukuru Kawamba), Ilemela (Angelina Mabula), Ilala (Mussa Azzan ‘Zungu’), Singida Mjini (Mussa Sima), Same Magharibi (Dk Mathayo David Mathayo), Rungwe (Saul Amon), Mbogwe (Augustino Masele), Chalinze (Ridhiwani Kikwete), Iramba Magharibi (Mwigulu Nchemba) na Hanang (Dk Mary Nagu).
Aidha, majimbo mengine ni Njombe Kaskazini (Joram Hongoli), Dodoma Mjini (Antony Mavunde), Mtama (Nape Nnauye), Babati Vijijini (Jitu Soni), Kahama Mjini (Jumanne Kishimba), Sikonge (George Kakunda), Nzega Mjini (Hussein Bashe), Urambo (Margaret Sitta), Mpanda Vijijini (Moshi Kakoso) na Geita Mjini (Constantine Kanyasu).
Chama hicho pia kilijipatia ushindi katika majimbo ya Mbeya Vijijini (Oran Njeza), Mafinga Mjini (Cosato Chumi), Kalenga (Godfrey Mgimwa), Isimani (William Lukuvi), Songea Mjini (Leonidas Gama), Mkalama (Allan Kiula), Newala (George Mkuchika), Kavuu (Dk Prudenciana Kikwembe) na Kwimba (Mansoor Shanif).
Mengine ni Bukoba Vijijini (Jason Rweikiza), Nyasa (Stella Manyanya), Kondoa Mjini (Edwin Sanda), Kondoa Vijijini (Dk Kashatu Kijaji), Chemba (Juma Nkamia), Chamwino (Joel Mwaka), Mtera (Livingstone Lusinde), Bahi (Omar Baduel), Mpwapwa (George Lubeleje), Kibakwe (George Simbachawene) na Kongwa (Job Ndugai).
CCM pia imepata Sengerema (William Ngeleja), Maswa Mashariki (Stanslaus Nyongo), Maswa Magharibi (Mshimba Ndaki), Itilima (Njalu Silanga), Bariadi (Andrew Chenge), Meatu (Salum Hamis), Muheza (Balozi Adadi Rajabu), Kasulu Mjini (Daniel Nsanzugwanko), Buhigwe (Albert Ntabaliba), Handeni Vijijini (Mboni Mhita) na Morogoro Mjini (Abdulaziz Abood).
Gairo (Ahmed Shabiby), Rorya (Lameck Airo), Ngorongoro (William Ole Nasha), Mvomero (Suleiman Murad), Morogoro Kusini Mashariki (Mgumba Omary), Morogoro Kusini (Prosper Mbena), Nkasi Kusini (Deuderius Mipata), Nkasi Kaskazini (Ally Keissy), Singida Kaskazini (Lazaro Nyalandu), Singida Magharibi (Elibariki Kingu) na Igunga (Dk Dalaly Kafumu).
Mengine yaliyoenda CCM ni Solwa (Ahmed Salum), Katavi (Issac Kamwele), Mpanda Mjini (Sebastian Kapufi), Mpanda Vijijini (Moshi Kakoso), Nsimbo (Richard Mbogo), Ruangwa (Kassim Majaliwa), Sumbawanga Mjini (Aeshi Hilaly), Kyela (Dk Harrison Mwakyembe), Ileje (Janeth Mbene) na Mbarali (Pirmohamed Mulla).
Majimbo mengine yaliyochukuliwa na chama hicho ni Busokelo (Atupele Mwakibete), Vwawa (Japhet Hasunga), Lupa (Victor Mwambalaswa), Songwe (Philipo Mulugo), Madaba (Joseph Mhagama), Peramiho (Jenista Mhagama), Kilosa Kati (Mohamed Bawazir), Kiteto (Emanuel Papian), Mbulu (Paul Isaay) na Karagwe (Innocent Bashungwa).
Kyerwa (Innocent Bilakwate), Nkenge (Dk Diodorus Kamala), Muleba Kusini (Profesa Anna Tibaijuka), Muleba Kaskazini (Charles Mwijage), Biharamulo Magharibi (Mukasa Oscar), Mwibara (Kangi Lugola), Bunda Vijijini (Boniphace Getere), Makete (Dk Norman Sigala), Kibaha Vijijini (Hamoud Jumaa) na Sumve (Richard Ndassa).
Magu (Kiswaga Destery), Chato (Dk Merdad Kalemani), Nzega Vijijini (Dk Khamis Kigwangallah), Njombe Mjini (Edward Mwalongo), Mwanga (Profesa Jumanne Maghembe), Nyangh’wale (Hussein Kassu), Newala Vijijini (Rashid Akbal), Butiama (Nimrod Mkono), Korogwe Vijijini (Stephen Ngonyani) na Korogwe Mjini (Mary Chatanda).
Misungwi (Charles Kitwanga), Busanda (Lolensia Bukwimba), Manonga (Seif Gulamali), Tabora Mjini (Emmanuel Mwakasaka), Mlalo (Rashid Shangazi), Kisesa (Luhaga Mpina), Lindi Mjini (Selemani Kaunje), Mkinga (Dustan Kitandula), Mbinga Mjini (Sixtus Mapunda), Mbinga Vijijini (Martin Msuha) na Musoma Mjini (Vedastus Mathayo).
Mengine ni Geita Vijijini (Joseph Kasheku), Kibaha Mjini (Silvestry Koka), Bukombe (Dotto Biteko), Shinyanga Mjini (Steven Masele), Msalala (Ezekiel Maige), Pangani (Jumaa Aweso), Mufindi Kaskazini (Mahamoud Mgimwa), Mufindi Kusini (Mendrad Kigola), Kilolo (Venance Mwamoto) na Maswa Mashariki (Stanslaus Nyongo).
Maswa Magharibi (Mashimba Ndaki), Chilonwa (Joel Mwaka), Mtwara Vijijini (Hawa Ghasia), Nanyamba (Abdallah Chikota), Tunduru Kusini (Daimu Mpakate), Tunduru Kaskazini (Ramo Makani), Bunda Vijijini (Boniface Mgetere), Mkuranga (Abdallah Ulega) na Mbulu Vijijini (Gregory Massay) nayo yameenda CCM.
Mengine ni Mbulu Mjini (Zacharia Paul), Kilindi (Kigua Mohamed), Namtumbo (Edwin Ngonyani), Ushetu (Elias Kuandikwa), Bumbuli (January Makamba), Segerea (Bonnah Kaluwa), Kalambo (Josephat Kandege), Wanging’ombe (Gerson Lwenge), Kigoma Kaskazini (Peter Serukamba), Muhambwe (Justus Nditiye), Kasulu Vijijini (Agustie Vuma) na Kilolo (Venance Mwamoto).
WABUNGE WA CHADEMA
Kwa upande wa CHADEMA, hadi sasa kimejinyakulia majimbo 35 ambayo ni Kibamba (John Mnyika), Mikumi (Joseph Haule), Bukoba Mjini (Wilfred Lwakatare), Same Mashariki (Nagenjwa Kayoboka), Rombo (Joseph Selasini), Bunda Mjini (Ester Bulaya), Hai (Freeman Mbowe) na Mbeya Mjini (Joseph Mbilinyi).
Majimbo mengine ni Kawe (Halima James Mdee), Longido (Onesmo Nangole), Ukonga (Waitara Mwita), Mlimba (Suzan Kiwanga), Singida Mashariki (Tundu Lissu), Ubungo (Said Kubenea), Mbozi (Paschal Haonga), Tunduma (Frank Mwakajoka), Momba (David Silinde), Kilombero (Peter Lijualikali) na Karatu (Willy Qambalo).
Aidha, chama hicho kilishinda katika majimbo ya Simanjiro (James ole Millya), Arumeru Magharibi (Gipson ole Meseyeki), Tarime Mjini (Ester Matiko), Siha (Godwin Mollel), Buyungu (Kasuku Bilago), Monduli (Julius Kalanga), Arumeru Mashariki (Joshua Nassari), Serengeti (Marwa Ryoba) na Babati Mjini (Pauline Gekul).
Mengine ni Moshi Mjini (Jaffar Michael), Tarime Vijijini (John Heche), Iringa Mjini (Peter Msigwa), Ndanda (Cecil Mwambe) na Moshi Vijijini (Anthony Komu). CUF yenyewe hadi sasa kina majimbo 17 ambayo ni Temeke (Abdallah Mtolea), Mchinga (Hamidu Bobali), Kilwa Kusini (Said Bungala), Kaliua (Magdalena Sakaya), Tandahimba (Ahmad Katani), Mtwara Mjini (Maftaha Nachuma), Kinondoni (Maulid Mtulia), Kilwa Kaskazini (Vedasto Ngombale) na Tanga Mjini (Musa Mbaruk). Majimbo mengine ni Wawi, Chakechake, Ole, Ziwani, Kojani, Gando, Wete na Mgogono.
WABUNGE WENGINE KUPTIA CHADEMA, CUF, ACT WAZALENDO na NCCR MAGEUZI
Hai(Freeman Mbowe), Vunjo (James Mbatia) Kigoma Mjini (Zitto Kabwe), Arumeru Mashariki (Joshua Nassari), Kawe (Halima Mdee), Ukonga (Waitara Mwita), Kibamba (John Mnyika), Ubungo (Said Kubenea), Bunda Mjini (Ester Bulaya), Tunduma (Frank Mwakanjoka), Siha (Dk Godwin Mollel), Tarime Vijijini (Esther Matiko), Same Mashariki (Nagenjwa Kayoboka), Kaliua (Magdalena Sakaya), Mlimba (Suzan Kiwanga), Iringa Mjini (Peter Msigwa).
Chanzo: Habari Leo Online

Friday, October 30, 2015


 Msafara wa Bw Magufuli umelindwa vikali na maafisa wa usalama
11:30am: Msafara wa Rais mteule John Magufuli pamoja na ule wa Rais Jakaya Kikwete waelekea ikulu chini ya ulinzi mkali. 

Friday, October 23, 2015

 Albino
Visa vya albino kushambuliwa na kukatwa viungo huongezeka sana wakati wa uchaguzi
Mwanamume mwenye ulemavu wa ngozi anauguza majeraha baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana eneo la Mkuranga, Tanzania.
Shambulio hilo dhidi ya albino huyo limetokea siku chache tu kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika.
Kumekuwepo na wasiwasi kwamba huenda watu wenye ulemavu wakashambuliwa zaidi kwani baadhi ya watu wanaoamini katika ushirikina hudai viungo vyao vinaweza kumpa mtu bahati.
Wanaume watatu wanadaiwa kuingia kwa nguvu nyumbani kwa Mohammed Said, 35, katika mji huo ulio katika mwambao wa Pwani kilomita 42 kutoka mji mkuu wa kibiashara wa Dar es Salaam.
Walimkata kichwani kwa upanga wakati wa shambulio hilo Jumatano usiku.
Polisi wamesema wanawasaka watu hao.

Saturday, October 17, 2015

 Aliyekuwa Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe enzi za Uhai wake.
 Msaidizi wa Mbunge huyo, Casablanga Haule enzi za Uhai wake.
 Padri Plasdus Ngabuma enzi za Uhai wake.
 Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Ludewa, Deogratias Filikunjombe wakati wa ibada ya kuuaga iliyofanyika nyumbani kwake Kijichi Dar es Salaam leo mchana.



Mke wa marehemu Deogratias Filikunjombe, Sarah Filikunjombe (kushoto) akilia kwa uchungu baada ya kupata tarifa za kifo cha mumewe.filikunjombeNdugu, jamaa na marafiki wakionekana wenye huzuni nyumbani kwa Deogratias Filikunjombe.filikunjombe (3)Nyumbani kwa Deogratias Filikunjombe Mbagala Kijichi, Dar es Salaam.silaaCapt. William Silaa enzi za uhai wake.chopaFilikunjombe akiwaaga wananchi wake.
Mbunge wa Ludewa Mhe. Deogratias Haule Filikunjombe amefariki dunia katia ajali ya Chopa katika hifadhi ya wanyama ya Selous, pamoja na rubani Kepteni William Silaa mfanyakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa.
Wengine waliofariki kwenye ajali hiyo ni Vitalis Blanka haule na Ofisa Tawala wa Wilaya ya Tarime, Bw. Egdi Mkwera ambaye alikuwa mtaalam wa mifugo.
Picha hapo chini ni Chopa iliyosababsha kifo cha Filikunjombe, Capt. William Silaa na watu wengine wawili.  chopa 2

Thursday, October 8, 2015

http://ichef.bbci.co.uk/news/ws/660/amz/worldservice/live/assets/images/2015/10/08/151008115839_bard_prison_initiative_512x288_bardprisoninitiative.jpg

Kundi la wafungwa kutoka New York limeshinda mdahalo dhidi ya kundi kutoka Chuo Kikuu cha Harvard, chuo kilichoorodheshwa bora zaidi duniani.
Wafungwa hao kutoka Eastern New York Correctional Facility walikuwa wamewaalika wanafunzi hao kutoka Harvard kwa shindano la mjadala gerezani.
Kwenye mdahalo huo, wafungwa walitetea msimamo kwamba watoto wa wazazi walioingia Marekani kinyume cha sheria wanafaa kukataliwa shuleni.
Mdahalo huo uliamuliwa na jopo lisiloegemea upande wowote.
Muda mfupi baada ya kushindwa, wanafunzi hao wa Harvard walijitetea kwenye ukurasa wa timu yao kwenye Facebook.


Mchoraji wa miundo ya magari nchini India Sudhakr Yadav amejaribu kuweka rekodi ya pili ya Guiness kwa kutengeneza gari analotumai litakuwa ndilo kubwa zaidi duniani.
Gari hilo, ambalo limeundwa likifanana na gari aina ya Ford Toure lililoundwa mwaka 1922, lina urefu wa futi 26 (mita 8) kwenda juu na ukubwa wa futi 50 lina ukubwa maradufu wa basi lililo na ghorofa mbili mjini London.

Sunday, October 4, 2015


Mwanasiasa mkongwe na Mwenyekiti wa chama cha kisiasa cha  DP Christopher Mtikilaamefariki dunia alfajiri ya leo wakati akitokea Morogoro kuelekea Dar es salaam.