Wednesday, April 29, 2015




Indonesia imewauwa wasafirishaji nane wa madawa ya kulevya siku ya Jumatano, wakiwemo raia saba wa kigeni, hatua iliyolaaniwa vika nya Australia na Brazil, zilizojaribu kuwaokoa raia wake bila mafanikio.
Indonesia imetete hatua yake hiyo ikiitaja kuwa ni muhimu katika mapambano dhidi ya madawa ya kulevya, na kusema haina wasiwasi kuhusiana na hatua zilizochukuliwa na Australia kufuatia mauaji hayo, ilizozitaja kuwa ni hisia za muda ambazo hazitadumu zaidi ya miezi mitatu.
Australia ilimuondoa balozi wake kutoka Indonesia kupinga mauaji hayo yaliyofanyika saa sita za usiku, lakini rais wa Indonesia Joko Widodo amesema alikuwa akitekeleza tu sheria dhidi ya wasafirishaji wa madawa ya kulevya.
Watuhumiwa hao -- wawili kutoka Australia, moja kutoka Brazil na wanne kutoka Nigeria -- waliuawa kwa kupigwa risasi pamoja na Muindonesia moja, licha ya kelele za mataifa ya kigeni na maombi ya huruma kutoka kwa wanafamilia wao.


Maelfu ya maafisa wa polisi nchini Marekani wameamriwa kuwasaidia maafisa waliozingirwa mjini Baltimore, baada ya ghasia zilizosababishwa na waandamanaji waliojawa na hasira, kufuatia kifo cha Mmarekani mweusi.
Muandamanaji akiwafokea polisi waliokuwa wanajaribu kudhibiti hali mjini Baltimore
Watu 27 wametiwa nguvuni huku polisi 15 wakijeruhiwa wakati waandamanaji hao wengi wao wanafunzi waliokuwa wanarusha mawe na kupora biashara za watu, walipopambana na maafisa wa polisi.
Ghasia mjini Baltimore zilianza baada ya mazishi ya kijana Mmarekani mweusi kwa jina Freddie Gray, aliyekuwa na miaka 25 na aliyefariki tarehe 19 mwezi wa Aprili kufuatia majeraha mabaya ya uti wa mgongo aliyoyapata wakati alipokuwa anatiwa nguvuni na maafisa wa polisi.


Chama tawala nchini Afrika Kusini African National Congress ANC kimelaani wimbi la mashambulizi dhidi ya raia wa kigeni ambayo yamesababisha vifo vya watu sita na kusababisha hali ya wasiwasi nchini humo
Taarifa kutoka kwa chama cha ANC imesema katika kipindi cha majuma kadhaa sasa, taifa la Afrika Kusini limeghubikwa na wimbi la mashambulizi ya kufedhehesha yanayowalenga raia wa kigeni kutoka nchi nyingine za Afrika.
ANC imeyataja mashambulizi hayo vitendo vya kihalifu dhidi ya watu wanyonge ambao wanatafuta hifadhi, faraja na kujiendeleza kiuchumi na kuongeza raia wa kigeni hapaswi kulaumiwa kwa changamoto zinazowakumba raia wa Afrika Kusini.
Katika mji wa kusini mwa nchi hiyo wa Durban mashambulizi yaliyochochewa na chuki dhidi ya wageni yamezilenga biashara na makaazi ya raia wa kigeni wakiwemo kutoka Somalia, Ethiopia na Malawi licha ya polisi kuimarisha doria katika mji huo kuzuia mashambulizi hayo.
Rais yuko kimya
Taarifa hiyo kutoka kwa ANC inakuja baada ya shutuma kuwa Rais Jacob Zuma ameshindwa kutoa tamko hadharani kuyalaani mashambulizi hayo. Mapema mwaka huu, raia wa kigeni pia walishambuliwa na maduka yao kuporwa katika kitongoji cha Soweto kilichoko karibu na mji wa Johannesburg.
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma
Mashirika ya kutoa misaada yamesema zaidi ya raia 2,000 wa kigeni wameutoroka mji wa Durban wakihofia maisha yao na sasa wanaishi katika kambi za muda chini ya ulinzi wa polisi na iwapo mashambulizi hayo hayatasitishwa,idadi ya waathiriwa inatarajiwa kuongezeka.
Mhamiaji mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Johnny ambaye ni raia wa Zimbabwe anasema anatafakari kurejea nyumbani
Jana maduka mengi yalifungwa katikati mwa mji wa Johannesburg baada ya wafanyaibishara kuhofia ghasia zitazuka baada ya vitisho kusambazwa katika mitandao ya kijamii.
Msumbiji imetangaza inapanga kuwasaidia raia wake walioko Afrika Kusini kurejea nyumbani baada ya waziri wa habari wa Malawi Kondwani Nankhumwa kusema wanawarejsha nyumbani raia wao 400 waliochomewa nyumba na mali zao. Malawi ndiyo nchi ya kwanza ya Afrika kuwaondoa raia wake kutoka Afrika Kusini.
Mfalme anashutumiwa kuchochea chuki
Mfalme Goodwill Zwelithini kiongozi wa kabila kubwa zaidi nchini Afrika Kusini la kwa Zulu Natal anashutumiwa kwa kuchochea mashambulizi hayo baada ya kutoa hotuba wiki mbili zilizopita akiwataka raia wa kigeni kufunga virago na kurejea makwao.
Baadhi ya waafrika Kusini wakikabiliana na raia wa kigeni mjini Durban
Mwakilishi wa mfalme huyo Thulani Zulu amekanusha kuwa mfalme huyo ndiye aliyechochea mashambulizi hayo na kuongeza kuwa amesikitishwa na yanayojiri na anayalaani .
Wanaharakati wanaopinga chuki dhidi ya raia wa kigeni wanapanga maandamano makubwa mjini Durban hii leo kuishinikiza serikali kuchukua hatua zaidi kuwalinda wahamiaji. Polisi Afrika Kusini imesema imewakamata watu74 kuhusiana na mashambulizi hayo.
Raia wa Afrika Kusini ambao hawana ajira wanawashutumu wageni kuwa wanachukua nafasi zao za kazi. Mwaka 2008, watu 62 waliuawa katika mitaa ya Johannesburg kutokana na chuki hizo dhidi ya wageni.

Juhudi za kukabiliana na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi nchini Tanzania zinapata nguvu mpya kupitia kampeni mbalimbali zinazolenga kuhamasisha jamii kupinga vitendo hivyo vya kinyama.
Watoto wenye ulemavu wa ngozi katika shule ya msingi ya Mitindo.
Pamoja na kampeni kadhaa zilizoanzishwa, siku ya Jumapili (tarehe 15 Machi) kulitarajiwa kuzinduliwa kampeni nyingine inayotumia kombe maalumu litakalozungushwa nchini kote kutuma ujumbe wa amani na kupinga mauaji ya albino.
Kampeni hii inazinduliwa katika wakati ambapo jeshi la polisi likitangaza kuwatia mbaroni zaidi wa waganga wa kienyeji 55 wanaotuhumiwa kupiga ramli zinazochonganisha watu ikiwamo zile zinazochochea mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi.

Tuesday, April 21, 2015






Serikali imerejesha mafunzo ya madereva kila baada ya miaka mitatu wakati wa kumalizika kwa muda wa leseni zao, huku ikifafanua kuwa elimu watakayoipata ina umuhimu katika kazi zao, kutokana na mabadiliko mbalimbali yanayotokea katika sekta hiyo.

 

Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Makongoro Mahanga, alitangaza uamuzi huo wa Serikali jana katika mkutano kati yake na viongozi wa madereva wa mabasi nchini.

 

Mkutano huo umefanyika kama ilivyoahidiwa na Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka, wakati alipokuwa akijitahidi kumaliza mgomo wa madereva uliofanyika Aprili 10 mwaka huu, wakati walipokuwa wakipinga pamoja na mambo mengine, sharti la kwenda shule ili kupata leseni mpya.

 

Madereva hao walitaka Serikali ifanyie marekebisho Sheria ya Usalama Barabarani, kwa kuondoa kipengele kinachowataka madereva kwenda Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kwa mafunzo ya muda mfupi kila wakati leseni zao zinapoisha, ili kupata sifa ya kupata leseni nyingine.

 

Sababu ya kupinga kupata mafunzo, ilidaiwa kuwa utaratibu huo uliotangazwa Machi 30, mwaka huu, ulianzishwa bila kushirikisha madereva katika kuuandaa.

 

Pia walipinga kutakiwa kujilipia gharama za shule hiyo ambazo walidai ni Sh 560,000 kwa magari ya kawaida na Sh 200,000 kwa magari ya abiria.

 

Sababu nyingine iliyochangia wapinge shule hiyo, walidai ni kukosekana kwa mikataba ya ajira, inayoweza kuwahakikishia kulindwa kwa kazi zao hadi wanapomaliza mafunzo.

 

Madai mengine yaliyokuwa nje ya shule hiyo, madereva hao walitaka kuondolewa kwa faini ya Sh 300,000 kwa kila kosa la barabarani na kuitaka Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchikavu (Sumatra), kuhakiki uhalisia wa dereva anayeandikishwa na mmiliki wa chombo husika.

 

Majibu ya Serikali Mahanga aliyekuwa Mwenyekiti wa kikao hicho, alisoma tamko la Serikali lililoeleza kuwa pamoja na kurejesha mafunzo hayo, utekelezaji wake hautafanyika mara moja kwa kuwa Kanuni zake hazijakamilika.

 

“Tangazo hili (la kwenda shule) limetolewa kwa kuzingatia umuhimu wa mafunzo kazini kwa wafanyakazi na madereva kama ilivyo kwa wafanyakazi wengine,” alisema Mahanga.

 

Alisisitiza kuwa baada ya miaka mitatu ya leseni, dereva atatakiwa kupata mafunzo mafupi, ambayo ni kati ya siku tatu hadi saba na atakayegharimia mafunzo hayo ni mwajiri, si mfanyakazi na ni katika chuo chochote kinachotambulika.

 

Akifafanua, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani, Mwamini Malemi aliyekuwepo katika mkutano huo, alisema mitaala ya mafunzo hayo bado inaandaliwa, hivyo si rahisi Kanuni hiyo kuanza kutekelezwa mwaka huu hata kama zitakamilika.

 

Kuhusu mikataba ya ajira ambayo ililalamikiwa mno na madereva wakati wa mgomo, Mahanga alisema Serikali itapitia upya mikataba hiyo ili kuhakikisha mambo yote muhimu yanazingatiwa.

 

Akiongezea hoja katika suala la mikataba, Malemi alisema ni lazima mikataba iwe imekamilika kabla ya kuanza kutumika kwa kanuni ya kwenda shule, ili ioneshe wajibu wa mwajiri katika kumsomesha mfanyakazi.

 

Kuhusu kauli iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova ya kuondoa tochi za kupima mwendo kasi barabarani, Mahanga alisema matumizi ya tochi zinazotumika kupima mwendo kasi na ratiba ni sehemu ya utekelezaji wa Sheria za Usalama Barabarani.

 

Hoja nyingine Katika kikao hicho mbali na hoja zilizosababisha mgomo, kulikuwa na hoja nyingine zilizowasilishwa, ikiwemo changamoto ya madereva kupata maelekezo yanayokinzana kutoka Jeshi la Polisi na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchikavu na Majini (Sumatra), kuhusu ratiba ya kuondoka wanakotoka na kuwasili wanakokwenda.

 

Akitoa majibu ya Serikali, Mahanga alisema amepokea hoja hiyo na ataifanya utafiti wa kina. Katika hoja ya kuwataka waajiri kuongeza posho za kazi, Mahanga alisema Serikali haiwezi kupanga posho za madereva katika kikao hicho, kwasababu kila mwajiri ana uwezo wake kulingana na safari za gari yake.

 

Hata hivyo, aliahidi kufanyika utafiti suala hilo katika nchi nyingine, ili aone namna ambavyo madereva wengine wamekuwa wakilipwa posho.

 

Serikali pia imeahidi kuimarisha ukaguzi sehemu za kazi kwa kushirikiana na Sumatra, utakaohusu wamiliki wa magari na kuhuisha mfumo wa kumbukumbu, utakaoonesha kila gari na dereva wake halisi na kuweka vitambulisho vya dereva katika kila gari analoendesha.

 

Mahanga alisema Serikali pia itaweka utaratibu mpya ambapo dereva mwenyewe atajiwekea bima ya ajali itakayoanzishwa na kujiunga na vyama vya wafanyakazi, ili watetee mikataba yao ili iweke pia maswala ya bima hizo.

 

Alisema pia Serikali imeanzisha Mfuko wa Fidia ya Wafanyakazi, ambao utaanza hivi karibuni, ambao mwajiri atawajibika kuchangia.

 

Chama cha Wafanyakazi  Kuhusu chama cha wafanyakazi, Mahanga alisema Serikali imepokea pendekezo la kusaidia madereva kuunda chama cha wafanyakazi chenye nguvu, ambapo alisema kumbukumbu zinaonesha madereva wana vyama vilivyosajiliwa kwa Msajili wa Vyama vya Wafanyakazi na Waajiri.

 

Alitaja vyama hivyo kuwa ni Umoja wa Wafanyakazi wa Mawasiliano na Usafiri Tanzania (COTWU), kilichosajiliwa mwaka 2000 na Chama cha Wafanyakazi cha Usafiri wa Barabara (TARWORTU) kilichosajiliwa mwaka 2013.

 

“Katika kushughulikia changamoto za wafanyakazi na mwajiri wote mnategemeana, jambo mtakalofanya ni kuanzisha majadiliano kupitia vyama vya wafanyakazi lakini kwanza muwe ndani ya vyama,” alisema Mahanga.

 

Wanung’unika  Baada ya kusomwa kwa tamko hilo la Serikali, Katibu Mkuu wa Vyama vya Madereva Tanzania, Mwanarashidi Salehe, alisema mafunzo wanayotakiwa kuchukua hayana tija yoyote, kwa kuwa wakufunzi ni wa kizamani na pia magari yanayotumika ni ya kizamani, ambayo hayaongezi chochote katika kazi yao.

 

“Kwanza hakuna kipya katika mafunzo hayo, mimi nimehudhuria mara mbili....pili katika kikao hiki tulitarajia tutakutana na wamiliki wa magari ambao ndio waajiri wetu ili waseme waliyonayo juu yetu na sisi tuseme yetu tujadiliane na kupata majibu,” alisema Salehe.

 

Mwenyekiti wa chama hicho, Clement Masanja alisema mikataba waliyonayo madereva ni dhaifu mno, haioneshi mambo ambayo dereva atanufaika nayo.

 

“Tulitarajia katika kikao hiki tutatoka na majibu ya posho za madereva, ili dereva ajue atalipwa kiasi gani kwa safari za ndani na nje ya nchi kwa sababu anavyolipwa ni manyanyaso matupu,” alisema Masanja.

Sunday, April 19, 2015


 wewe  ni  dereva  wa basi la abiria ama  gari  binafsi ?hebu  chukua  hatua ya  kupunguza ajali  leo kwa kujihadhari na  kona  hizi na Iyovi na Kitonga na  kona  nyingine kali kama  hizi nchini kwani maisha  yako ni  dhamani  kubwa na uhai  wake bado tunautamani
 Vema  kuheshimu alama  za barabarani na  kuacha mbwembwe  uwapo  barabarani katika kona kali kama hizi
 Katika kona  kama  hizi  zingatia  alama  za usalama  barabarani  usiwe na haraka  ya  kulipita gari la mbele