Tuesday, December 27, 2016


Kama tunavyofahamu, nchi yetu ina aina mbalimbali za nyoka ambao pindi wakimuuma mtu huleta madhara mbalimbali ya kiafya. Aidha tunafahamu kwamba tatizo hili lipo zaidi katika maeneo ya vijijini ambako uwezo wa wananchi kumudu gharama za matibabu ni mdogo.

Sunday, November 27, 2016

Maphorisa na Wizkid wametuletea hii ya pamoja inayoenda kwa jina la Good Love ikiwa imetayarishwa na Nana Rouges.
Wimbo mpya kutoka Niger unaoenda kwa jina la Life, Bisa Kdei  akimshirikisha Patroranking.

Do like that Kutoka kwa Korede Bello ikiwa imetayarishwa na Mavin Records chini ya Producer Altims.
Otile Brown Katuletea wimbi huu akimshirikisha Baraka The prince, Wimbo unaitwa Niseme Nawe.
Producer akiwa Teddy B. Na video Director akiwa Dr Eddie chini ya Dreamland Music Entertainment

Thursday, November 10, 2016

Msanii Yemi Alade kutoka Nigeria,ameamua kurudi bivi  baada ya MTV mama 2016 na hii ‘Tumbum’.
Kundi la Weusi wameachia wimbo mpya unaitwa “Nijue”, wamemshirikisha  Christian Bella, Producer ni Nahreel wa The Industry.

Sunday, October 30, 2016

https://encrypted-tbn0.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcSiTUqUeKicy0oJY8jyVoQJ_fIPUG_5l4K0N0I0sGwHdYIV5zmp
Mapema Jumamosi hii zilisambaa picha ‘fake’ inayomuonyesha msanii huyo mahiri duniani akiwa ameshasajiriwa kwa ajili ya tamasha hilo linalotarajiwa kufanyika Novemba 5 katika viwanja wa Leaders Club jijini Dar es salaam.
Kupitia ukurasa wa instagram wa Clouds FM umetoa taarifa hii:
Kumetokea uzushi kwamba tumemsajili msanii Jay Z kwa ajili ya kilele cha #Fiesta2016 hapo #November05. Tunapenda kukanusha habari hiyo; picha iliyotengenezwa kueneza habari hiyo ni batili
Wasanii wakimataifa ambao tayari uwepo wao umetangazwa ni pamoja na Yemi Alade wa Nigeria, Jose Chameleone wa Uganda pamoja na Tekno wa Nigeria.
Hii ni list ya wasanii wa Tanzania.
1. Ben Pol
2. Nandy
3. Christian Bella
4. Fid-Q
5. Weusi
6. Roma
7. Chegge
8. Dogo Janja
9. Billnass
10. Stamina
11. Jux
12. Barnaba
13. Maua Sama
14. Darassa
15. Vanessa Mdee
16. Sholo Mwamba
17. Jay Moe
18. Msami
19. Juma Nature
20. Snura
21. Baraka Da Prince
22. Shilole
23. Manfongo
24. Belle 9
25. Lord Eyes
26. Young Dee
27. Raymond
28. Mr. Blue
29. Alikiba




Source

Thursday, October 27, 2016

Image result for Abby Skillz Ft. Alikiba & Mr Blue – Averina
Kupakua wimbo huu bofya hapa chini
Bonyeza hapo chini ili kuona matokeo ya darasa la saba. (PALIPOANDIKWA MATOKEO HAYA HAPA)

Sunday, July 31, 2016


Msanii wa Nigeria "Tiwa Savage" aachiwa wimbo wake mpya "Bad" akimshirikisha "Wizkid". Video imefanywa na Director "Sesan"

Friday, July 22, 2016

Tume ya vyuo vikuu nchini TCU, imevizuia vyuo sita nchini kufanya udahili wa wanafunzi kwenye msimu wa masomo wa 2016/17.
WAZIRI-WA-ELIMU
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa. Joyce Ndalichako (Kulia)

Hatua hiyo imechukuliwa na tume hiyo kutokana na vyuo hivyo kutokidhi viwango vya elimu vilivyokuwa vikiitoa.
Vyuo hivyo ni pamoja na:
1. International Medical and Technological University (IMTU) – all programmes.
2. St. Francis University College of Health and Allied Sciences (SFUCHAS) – all programmes.
3. University of Bagamoyo (UoB) – all programmes.
4. St. Joseph University College of Engineering (SJUCET) – all programmes.
5. University of Dodoma (UDOM) – Doctor of Medicine Programme
6. State University of Zanzibar (SUZA). – Doctor of Medicine Programme.
Mchekeshaji Ismail Issa Makombe ‘Kundambanda’ amefariki dunia usiku wa kuamkia Ijumaa hii baada ya kusumbuliwa na matatizo ya tumbo kwa muda mrefu.
p.txt
Mwigizaji huyo ambaye pia aligombea ubunge katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, amekutwa na umauti akiwa nyumbani kwao Mtwara.
Akiongea na Bongo5 Ijumaa hii Mwenyekiti wa Chama cha wasanii wa Vichekesho Tanzania, Mkono Wa Mkonole amethitisha kutokea kwa msiba huo.
“Kweli ndugu yetu ametutoka na kwa taarifa zisizo rasmi kesho wanazika, lakini sisi kama wasanii wa vichekesho leo jioni tunakutana na kupanga jinsi ya kuweza kuhudhuria mazishi ya ndugu yetu,” alisema Mkonole.

Tuesday, July 12, 2016

Kama wewe ni mpenzi wa mziki mtamu kutoka Afrika basi huwezi kuchelewa kuiona video hii. Kwa hapa nadhani ni mwendo wa tuzo tu zinangojea kumiminika.
Basi ruka kidogoooooo.....

Saturday, July 2, 2016

 
Mkhitaryan
Mshambuliaji wa klabu ya Borussia Dortmund Henrikh Mkhitaryan amesajiliwa na klabu ya Manchester United ,kulingana na klabu hiyo ya Ujerumani.
Afisa mkuu wa Dortmund Hans-Joachim Watzke amesema kuwa wamekubali kumuuza mchezaji huyo kwa United ili kumzuia nahodha huyo wa Armenia kuwa ajenti huru mwishoni mwa msimu ujao.
''Iwapo tungekataa mchezaji huyo angekuwa huru mwaka 2017'' ,Watzke aliambia mtandao wa Dortmund.
United tayari imewasajili wachezaji wawili msimu huu akiwemo beki Eric Baily na mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic.
Mkhitayran alijiunga na Dortmund 2013 kutoka klabu ya Ukrain Shakhtar Donetsk kwa pauni milioni 23.

Sunday, June 26, 2016

 Sanamu (5)
Historia ya Mnara ule ilianza mwaka 1889, kisha, kabla na baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia (1914 - 1918) hadi Vita Kuu ya Pili ya Dunia (1939 - 1945).
Kwa ufupi Sanamu ya mwanzo kukaa pale ni sanamu ya Herman Von Wissman, Gavana wa Kijerumani ambaye anakumbukwa kwa kutekeleza utekaji na mauaji ya Abushir Ibn Salim Al Harthi, mtawala/sultani
wa Pangani Tanga.
June 24 2016 Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ‘TAMISEMI’ imetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ufundi kwa mwaka 2016. Wanafunzi waliochaguliwa ni kutoka shule za Serikali na zisizo za Serikali, Kwa urahisi zaidi unaweza kuyaona majina yote kwenye hii link hapa

Friday, June 17, 2016


Rapper Chidi Benz amefanikiwa kuirudisha afya yake baada ya kuachana na matumizi ya Madawa ya kulevya.

Mapema mwaka huu katika kituo kimoja cha runinga Chidi Benz alikiri kutumia Madawa ya kulevya na kuomba msaada ambapo meneja Diamond na Tip Top Connection, Babu Tale akishirikiana na Kalapina walimsaidia na kumpeleka katika kituo cha Bagamoyo Sober House ambacho kilimsaidia kuachana na Matumizi ya madawa ya kulevya.

Wednesday, June 8, 2016


Nchini kenya waziri wa fedha Henry Rotich leo amewasilisha bungeni bajeti ya makadirio ya matumizi ya pesa za serikali katika kipindi cha mwaka 2016-2017.
Bajeti hiyo ya jumla ya shilingi trilioni 2.26 inatarajiwa kufadhiliwa kupitia ukusanyaji wa ushuru na mikopo kutoka kwa washirika wa kimaendeleo. Serikali inalenga kukopa shilingi bilioni 778 hatua ambayo itaongeza deni la kenya ambalo kufikia sasa ni shilingi trilioni 3.32.
Matumizi zaidi itaelekezwa kwa ujenzi wa miundo mbinu ikiwa ni pamoja ujenzi wa reli ya kisasa, kuimarisha usalama, huduma za afya na pia kuziwezesha serikali za majimbo.
Kama ilivyo ada bajeti inaposomwa kuna wale wa wanaofaidi na wale wanaopoteza. Gesi ya kupikia na chakula cha mifugo umeondolewa ushuru, Huku ushuru wa petroli na mafuta taa ukiongezwa. Bidhaa za mafuta ya urembo zikiwekewa ushuru wa asilimia kumi kwa mara ya kwanza.
Waziri ametenga shilingi bilioni 4.3 kwa huduma za bure za wanawake wajawazito kujifungua,milioni 19.7 kwa maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2017 na shilingi milioni 7.9 kwa watoto mayatima.


Nchini Tanzania makadirio ya bajeti ya mwaka 2016 na 2017 ni trilioni 29,5 pesa za Tanzania ikiizidi bajeti ya mwaka wa 2015 na 2016 kwa trilioni 7.1.
Waziri wa Fedha nchini Tanzania Phillip Mpango alisema kuwa kati ya fedha hizo, Shilingi trilioni 18.46 zitatokana na jumla ya mapato ya ndani.
Kiwango hicho kimezidi shilingi trilioni 3.64 za bajeti iliyopita ambayo ililenga kukusanya shilingi trilioni 4.82.
Shilingi trilioni 17.72 zitakuwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida, huku trilioni 11.82 sawa na asilimia 40 ya bajeti nzima, zikitengwa kwa ajili ya shughuli za maendeleo.
Bwana Mpango alisema washirika wa maendeleo wanatarajiwa kuchangia shilingi trilioni 3.6, ikiwa ni ongezeko la shilingi trilioni 1.7 ikilinganishwa na shilingi trilioni 1.88 zilizokuwa zinategemewa kwenye bajeti iliyopita.
Makadirio ya bajeti nchini Uganda mwaka 2016 na 2017 iliyosomwa leo ni ya jumla ya dola bilion 7.5 ambayo ni sawa na trillioni 27. 3 pesa za Uganda, tofauti na bajeti ya mwaka uliopita ya mwaka 2015 na 2016 ambayo ilikuwa ni dola bilioni 6.9.
Bajei kubwa mwaka huu nchini Uganda imeelekezwa kwa wizara ya kazi na uchukuzi ambayo ilipewa dola blioni 1.1 huku wizara ya ulinzia ikipewa dola milioni 435. Wizara ya afya imepata dola milioni 525.
Wizara ya nishati na maendeleo ya madini ilipata dola milioni 695 huku Wizara ya kilimo ambayo nidiyo muhimu nchi Uganda ikiewa dola milioni 522.

Tuesday, May 31, 2016

Msanii Korede Bello aachia wimbo wake mpya unaoitwa One and Only kama video yake inavyoonekana hapojuu.unaweza kuiangalia moja kwa moja hapo juu

Monday, May 30, 2016

 
Chuo kikuu cha Dodoma
Wanafunzi katika chuo kikuu cha Dodoma nchini Tanzania wamefukuzwa chuoni humo baada ya kuzuka kwa mgogoro kati ya serikali na wahadhiri wa chuo hicho.
Wanafunzi hao waliagizwa kuondoka katika chuo hicho kufikia saa kumi na mbili jioni siku ya Jumapili.

Ilani
Ilani hiyo imesema kuwa kulikuwa na makosa katika mafunzo ya wanafunzi wanaosomea shahada ya elimu ikiwemo sayansi,hesabati,teknolojia hivyobasi serikali imewataka wanafaunzi hao kuondoka chuoni humo hadi ilani nyengine itakapotolewa.
Maelezo kuhusu mgogoro huo kati ya wahadhiri wa chuo hicho na serikali hayajulikani.

Thursday, May 26, 2016

Wolper akiri kuwa na uhusiano na Harmonize, asema hakujua kama ‘Mkongo’ ana mke.
Mwigizaji Jackline Wolper jana amefanya mahojiano na Zamaradi Mketema kwenye kipindi cha TakeOne na kuzungumzia mambo mengi kuhusu yeye na aliyekuwa mpenzi wake Putin ‘Mkongo’ aliyemvisha pete, na uhusiano wake na msanii Harmonize.
‘Ni kweli Raj (Harmonize)ni mpenzi wangu,ukweli nilimjua siku nyingi nilikuwa nikimchukulia kama mwanamuziki tu, tuna mwezi mmoja na wiki mbili sasa’’ alisema Jack.

Tuesday, May 24, 2016


3ede2cfb-a205-4083-9c8e-b5227c971c2b

Zitto Kabwe akimvisha pete mchumba wake
Zitto Kabwe amemchumbia msichana mrembo anayetarajia kumbadilisha jina soon kuwa ‘Mrs Kabwe.’ Mchumba wake anaitwa Anna Bwana anayefanya kazi BBC Media Fund ambapo kabla ya hapo alikuwa mfanyakazi wa shirika la Oxfam.
Baada ya kuwasaini Davido na Alikiba, record label kongwe duniani, Sony Music imemsaini msanii wa Afrika Kusini, Mobi Dixon.
Mobi-Dixon
Mobi Dixon anakuwa msanii wa tatu kutoka Afrika kusainiwa kwenye label hiyo.

Monday, May 23, 2016


Kialama cha WhatsApp
WhatsApp imepitia mabadiliko mengi, na imekuwa kati ya applications zinazotumika na kupendwa zaidi duniani. Baada ya kununuliwa na Facebook, waendelezaji walianza kuongeza vitu vipya kama kupiga simu za sauti, kuweza kutuma mafaili, na kuongezwa kwa usalama zaidi. Kwasasa, WhatsApp ni moja kati ya application yenye watumiaji wengi zaidi, ikiwa na angalau watumiaji bilioni moja wanaotumia kikamilifu kila mwezi. Katika makala hii, tutafahamisha baadhi ya vitu vilivyopo WhatsApp na havitumiki mara nyingi, na namna vinavyoweza kutumika;

Saturday, May 21, 2016

Msanii Kadjanito ameachia video mpya ya wimbo ‘One More Night. Video imeongozwa na GQ Digital Vibes.
Msanii wa Hip Hop Stamina ameachia wimbo mpya unaitwa “Mmeniroga”, Producer Rash Don

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mheshimiwa Charles Kitwanga kuanzia leo tarehe 20 Mei, 2016.

Rais Magufuli ametengua uteuzi huo kufuatia kitendo cha Mheshimiwa Charles Kitwanga kuingia bungeni na kujibu swali linaloihusu wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi akiwa amelewa.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam

Friday, May 20, 2016

Swala
Shambulio lilitekelezwa wakati wa swala jioni
Polisi nchini Tanzania wanawazuilia watu watatu wanaotuhumiwa kuhusika shambulio katika msikiti mmoja mjini Mwanza magharibi mwa nchi hiyo.
Watu watatu, akiwemo Imam, walifariki wakati wa shambulio hilo lililotekelezwa katika msikiti wa Rahman wakati wa swala ya usiku siku ya Jumatano.
Kwa mujibu wa kamanda wa polisi jijini humo, Ahmed Msangi, uchunguzi wa mwanzo umebaini kwamba mauaji hayo yalifanywa kwa kutumia mapanga na kuongeza kuwa, polisi wanachunguza chanzo cha shambulizi hilo.
Baadhi ya walioshuhudia tukio hilo, wamesema shambulio hilo lilitekelezwa na kundi la watu wasiopungua 15.
Staa wa Marekani, Ne-Yo jana usiku alitua jijini Dar es Salaam akitokea Marekani akiwa na ulinzi mkali.
Muimbaji huyo wa ‘Miss Independent’ alitua kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere mida ya saa tano kasoro usiku. Staa huyo aliyekuwa amevaa nguo zote nyeusi na kofia ambayo alikuwa ameifunika na hood aliwapungia mkono waandishi wa habari na mashabiki waliokuwa wamejitokeza kumpokea kabla ya kuingia moja kwa moja kwenye gari na kufunga vioo.
Mlinzi wake pandikizi la mtu, alimzuia staa huyo kutoongea na waandishi wa habari kwa kudai kuwa alihitaji kupumzika kutokana na uchovu wa safari hiyo. Hata hivyo baada ya kuombwa na waandishi wa habari walau wamuulize maswali machache, alifungua kioo cha gari na Ne-Yo kusalimia.
“Fantastic so far,” alijibu Ne-Yo baada ya kuulizwa anajisikiaje kuja Tanzania. “ I am happy to be here looking forward to perform with Diamond and everyone who will be at the show,” aliongeza.
Ne-Yo atatumbuiza Jumamosi hii kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza kwenye tamasha la Jembeka linalodhaminiwa na Vodacom. Diamond na wasanii wengine zaidi ya 20 watatumbuiza kwenye tamasha hilo kubwa linaloandaliwa na kituo cha redio cha Jembe FM.
Drake amezidi kuonyesha ubora wake kwenye tuzo za BET zitakazofanyika, Juni 26 huko Los Angeles, Marekani.
drake
Mwaka 2016 umekuwa wa neema kwa Drake baada ya kuonekana mara tisa kati ya vipengele sita alivyowekwa akifuatiwa na Beyonce pamoja na Rihanna. Pia albamu yake ya ‘Views’ inazidi kushika namba moja kwenye chati za Billboard baada ya kuuza nakala zaidi ya milioni 1.04 ndani ya wiki mbili tangu alipoiachia mwishoni mwa mwezi Aprili.
Tuzo hizo za BET zitafanyika kwenye ukumbi wa Microsoft Theater, Los Angeles huku Afrika Mashariki tukiwakilishwa na Diamond kwenye kipengele cha Best International Act: Africa lakini pia atafanikiwa kufanya show kwenye tuzo hizo.

Wednesday, May 4, 2016

 Jani
Mvulana huyo amepewa $10,000
Mvulana wa umri wa miaka 10 nchini Finland ameshangaza wengi baada ya kugundua udhaifu katika mtandao wa kijamii wa Instagram.
Mvulana huyo kwa jina Jani ametunukiwa $10,000 (£7,000) baada ya kugundua udhaifu huo uliowezesha mtu kuingia kwenye mtandao huo wa kusambaza picha na kufuta maoni ya watu.
Jambo la kushangaza zaidi ni kwamba kisheria haruhusiwi kutumia mtandao huo hadi atimize umri wa miaka 13.
Facebook, inayomiliki Instagram, ilichukua hatua upesi na kuondoa udhaifu huo.
Sasa, ndiye mtu mchanga zaidi kutunukiwa pesa kwa kugundua udhaifu katika mitandao ya kampuni hiyo.
Aliandikia wasimamizi wa mtandao huo barua pepe Februari kuwafahamisha kuhusu ugunduzi wake.
Wataalamu wa mtandao huo walimfungulia akaunti ndipo aweze kuthibitisha madai yake na akafanikiwa.
Mvulana huyo kutoka Helsinki, ameambia gazeti la Iltalehti la Finland kwamba atatumia pesa hizo kununua baiskeli, mpira na mavazi ya kuchezea kandanda na kompyuta za kutumiwa na ndugu zake.

Facebook imeambia BBC kwamba imelipa jumla ya $4.3m kwa watu waliogundua udhaifu kwenye mitandao yake.
Malipo hayo hutolewa kama kishawishi kuzuia watu kuuzia wahalifu ugunduzi wao na hivyo kusaidia kampuni husika.
Bagaza
Kanali Bagaza alikuwa na umri wa miaka 69
Rais wa zamani wa Burundi Kanali Jean-Baptiste Bagaza amefariki akitibiwa nchini Ubelgiji.
Kanali Bagaza amekuwa akitibiwa kwa muda katika hospitali ya Sainte Elisabeth mjini Brussels.
"Imethibitishwa, rais wa zamani Jean Baptiste Bagaza amefariki dunia akiwa nchini Ubelgiji,2 ameandika mshauri wa rais wa Burundi Willy Nyamitwe kwenye Twitter.
"Alikuwa seneta maisha.”
Kanali Bagaza aliingia madarakani Novemba 1976 kupitia mapinduzi ya kijeshi.
Aliondolewa madarakani kupitia mapinduzi mengine yaliyoongozwa na binamu wake Meja Pierre Buyoya Septemba 1987.

Tuesday, May 3, 2016


Afeni Shakur
Mamaake aliyekuwa mwanamuziki wa mtindo wa Rap Tupac Shakur ,Afeni Shakur amefariki akiwa na umri wa miaka 69.
Kaunti ya California imethibitisha kifo chake kupitia ujumbe wa Twitter.Hakuna maelezo zaidi yaliotolewa.
Alice Faye Williams,alibadilisha jina lake na kuitwa Shakur akiwa mtu mzima alipokuwa mwanaharakati wa kisiasa na kujiunga na vuguvugu la Black Panther.
Alikuwa na mimba ya Tupac mwaka 1971 alipokamatwa na kufungwa jela pamoja na wanachama wengine wa vuguvugu hilo na kukabiliwa na mashtaka ya njama ambayo baadaye yalitupiliwa mbali.
Shakur alikuwa kigezo kizuri cha muziki wa mwanawe na alisimamia muziko wake baada ya kifo chake.

 Tupac Shakur
Tupac Shakur alifariki mwaka 1996 akiwa na umri wa miaka 25,baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana katika gari moja.
Mauaji yake bado hayajapata ufafanuzi.

IMF: Uchumi wa Tanzania waongoza Afrika Mashariki
Tanzania inatarajiwa kusajili kiwango cha juu zaidi cha ukuaji wa uchumi wake mwaka huu katika kanda ya Afrika Mashariki na kati.
Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya shirika la fedha la kimataifa - IMF.
Katika ripoti yake iliyotolewa hii leo Tanzania inatarajiwa kusajili kiwango cha juu cha ukuaji wa uchumi wake wa asilimia 6.9% mwaka wa 2016.
Kasi hiyo ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania ni ya pili tu nyuma ya Ivory Coast baina ya mataifa ya Kusini mwa jangwa la Sahara .

 Tanzania inatarajiwa kusajili kiwango cha juu cha ukuaji wa uchumi wake wa asilimia 6.9% mwaka wa 2016.
Ivory Coast inatarajiwa kukuwa kwa kasi ya asilimia 8.5%.
Katika kanda ya Afrika Mashariki ,uchumi wa Kenya ndio wa pili kwa kasi ya ukuaji kwa asilimia 6%.
IMF hata hivyo inasema kuwa kasi ya ukuaji wa uchumi kusini mwa jangwa la Sahara unatarajiwa kupungua kwa mwaka wa pili mfululizo kutokana na kudorora kwa viwango vya uzalishaji na hivyo uwekezaji.
Kwa mujibu wa shirika la fedha la kimataifa - IMF, eneo hilo linakadiria kushuka kwa ukuwaji wa uchumi kwa asilimia 3 mwaka huu.
Kiwango hicho ni cha chini kabisa kuwahi kushuhudiwa katika miaka 15.

 Mataifa yanayotegemea mapato yanayotokana na mafuta ndiyo yalioathirika zaidi kama vile Nigeria na Angola.
Mataifa yanayotegemea mapato yanayotokana na mafuta ndiyo yalioathirika zaidi kama vile Nigeria na Angola.
Aidha Zambia pia imeathirika vibaya kutokana na ukosefu wa soko la kimataifa la shaba yake.
Ripoti hiyo inaitaja Afrika Kusini kama moja ya mataifa ambayo kiwango chake cha ukuaji kimedorora kwa kiasi kikubwa mno.
Katika orodha ya mataifa yanayotarajiwa kuwa na kiwango cha juu cha ukuaji Kusini mwa jangwa la sahara Ivory Coast ndio inayoongoza.
Orodha ya mataifa ya kanda ya Kusini mwa Jangwa la Sahara na viwango vya kasi ya ukuaji wa uchumi 2016.
  1. Ivory Coast 8.5%
  2. Tanzania 6.9%
  3. Senegal 6.6%
  4. Kenya 6%
  5. Zambia 3.4%
  6. Nigeria 2.3%
  7. Afrika Kusini 0.6%

Thursday, April 28, 2016


Madhara ya mvua kubwa mjini Dar es Salaam
Leo imekuwa siku ngumu sana kwa uchukuzi mjini Dar es Salaam, Tanzania.
Kisa na maana,,,,mafuriko.
Wenyeji walitatazikika kuendesha shughuli zao za kawaida
 Baadhi ya barabara kuu za kitovu hicho cha kibiashara cha Tanzania, zilikuwa hazipitiki.
Maji kila mahali 
Mvua kubwa inayoendelea kunyesha hivi sasa kanda yote ya Afrika Mashariki imesababisha mafuriko makubwa ambayo muundo msingi wa barabara za miji ya Nairobi na Dar es Salaam haziwezi kumudu.
Magari ambayo yalijaribu kutumia mabarabara ya Dar es Salaam yalikwama mengine huku yale yenye kimo cha juu yakifaulu kupita.

 Magari mengi yamekwama barabarani 
Wenyeji sasa wameanza kuhoji uwezo wa muundo msingi wa maji taka wa mji huo wa Dar es Salaam hususan ukizingatia kuwa ndio sasa msimu wa mvua umeanza.
Mtangazaji wetu wa Dar es Salaam Sammy Awami amefaulu kuondoka nyumbani kwake na katika pita pita zake ametutumia picha hizi zinazoonesha hali halisia ya baadhi ya mabarabara ya Dar es Salaam.

 Wenye magari mjini Nairobi wataabika mabarabarani 
Nchini Kenya hali sio tofauti.
Barabara ya kisasa ya Thika Super Highway haipitiki baada ya mvuo kubwa kunyesha mchana na kusababisha mafuriko makubwa.
 

Thursday, April 21, 2016

 
Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imekiri Serikali kupoteza mapato mengi ya ndani kwa miaka ya nyuma kutokana na mapungufu ya Sheria ya kodi ya ongezeko la thamani ya mwaka 1997 na Sheria ya Usimamizi wa kodi. Mapungufu ya Sheria hizo yaliikosesha nchi mapato kwa kile kilichodaiwa kuwepo kwa misululu mingi ya misamaha ya kodi, iliyotolewa kwa sababu mbalimbali.
Katika mafunzo maalumu ya elimu kwa mlipa kodi yaliyotolewa kwa wamiliki wa mabasi nchini TABOA na mamlaka hiyo yalikusudia kutoa uelewa na umuhimu wa kutumia mashine za kutolea risiti pamoja na sheria mpya za kodi kama zilizofanyiwa marekebisho.

BAADA ya jana kutolewa kwenye michuano ya klabu bingwa barani Afrika na Al Ahly ya Misri, Yanga sasa imepangiwa kucheza na Sagrada Esperance ya Angola kwenye michuano ya kombe la shirikisho.

Sagrada wako nafasi ya 10 katika msimamo wa ligi ya Angola wakiwa na alama 9 pekee.

Yanga sasa itaanzia nyumbani Dar es Salaam katika mchezo wa kwanza kati ya Mei 6 na 8 kabla ya kurudiana kati ya Mei 17-18.

Mechi nyingine zitakuwa kama ifuatavyo:

MO Bejaja(Algeria) vs Esparance (Tunisia)

Stade Malien(Mali)vs FUS Rabat( Morocco)

Etoile du Sahel (Tunisia) vs CF Mounana(Gabon)

http://www.channelten.co.tz/wp-content/uploads/2016/01/tbs-may16-2013113.jpg

Wizara ya Viwanda na Biashara imeliagiza Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kusimamia na kuhakikisha wazalishaji wa bidhaa nchini wanakuwa na alama ya Msimbomilia au BarCode inayotambulisha bidhaa husika lengo likiwa ni kuondokana na bidhaa feki.
Wizara hiyo imesema kuwepo kwa alama hiyo kutaziwezesha bidhaa za nchini kuwa na soko na hatimaye kuepukana na bidhaa toka nje ya nchi ambazo viwango vyake vya ubora vinatiliwa shaka.
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Odilo Majengo amesema Wizara yake ipo katika kuvifanyia maboresho viwanda vya ndani ili vizalishe bidhaa zenye ubora na zenye kutambulika nje ya nchi hivyo matumizi ya BarCode yatasaidia kuinua viwango vya ubora wa bidhaa nchini.
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kwa kushirikiana na Kampuni inayotoa nembo hizo za BarCode ya GSI wamesaini hati ya makubaliano ya kuhakikisha wafanyabiashara wa ndani wanatambulika kwa kutumia nembo hiyo ya biashara.

Wednesday, April 20, 2016


Kaimu kamishina wa madini, Ally Samaje
MADINI aina ya Tanzanite ya thamani ya Sh bilioni 2.5 yaliyokamatwa mwaka jana yakitoroshwa nje ya nchi, yatauzwa kwa mnada wa hadhara wakati wa maonesho ya kimataifa ya madini ya vito yaliyoanza jana hapa.
Madini hayo yalikamatwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) yakitaka kutoroshwa kwenda nje ya nchi bila kufuata utaratibu wa kisheria na baada ya kukamatwa yametaifishwa na serikali.
Akizungumza jana jijini hapa wakati wa ufunguzi wa maonesho hayo ya tano ya madini ya vito ya siku tatu, Kaimu Kamishna wa Madini nchini, Ally Samaje, alisema madini hayo yatapigwa mnada katika maonesho hayo ikiwa ni sehemu ya kudhibiti utoroshwaji wa madini nchini.

Thursday, April 14, 2016



RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dkt. Ali Mohamed Shein jana Jumamosi, April 9, 2016 ametangaza Baraza la Mawaziri litakalosimamia kazi za serikali kwa kipindi cha uongozi wake wake kwa mujibu wa sheria.

Dkt. Shein amesema amepunguza ukubwa wa baraza hilo kutoka wizara 16 hadi kuwa wizara 13, ambapo wizara tatu amezivunja na kuzigawa ndani ya hizo wizara 13 za sasa.

Mawaziri ni 13 na Manaibu waziri 7.Ameongeza kuwa, mawaziri aliowatangaza leo atawaapisha kesho Jumapili asubuhi katika Viwanja vya Ikulu visiwani Zanzibar.

Sunday, April 3, 2016


Wachezaji wa ligi kuu ya Uingereza wanatumia madawa yaliyopigwa marufuku
Serikali ya Uingereza imeanzisha uchunguzi wa dharura kufuatia ufichuzi kuwa wachezaji nyota wa kandanda nchini Uingereza wamekuwa wakitumia madawa yaliyopigwa marufuku ya kuongeza nguvu mwilini.
Gazeti la Sunday Times limechapisha rhttps://www.blogger.com/blogger.g?blogID=5420544876886876991#editor/target=post;postID=5548928251777649508ipoti ya uchunguzi iliyothibitisha kuwa sio tu wasakataji dimba bali hata waendesha baiskeli, wachezaji Kriketi na hata wachezaji wa tenisi wamekuwa wakipokea matibabu kutoka kwa daktari mmoja ambaye anajulikana kwa kupeana madawa hayo yaliyopigwa marufuku ya kututumua misuli.
Daktari Mark Bonar ambaye anazahanati yake mjini London Uingereza amekuwa akiwatoza wachezaji nyota maelfu ya pauni za Uingereza kwa matibabu hayo fiche ambayo imegunduliwa kuwa ni matibabu ya madawa yaliyopigwa marufuku na shirikisho la kupambana na madawa haramu WADA.

Sunday, March 13, 2016


Germanwings: Madaktari watoe siri za marubani
Wachunguzi kutoka Ufaransa, wamependekeza sheria kali inayozuia madaktari kufichua siri za marubani wagonjwa iondolewe.
Wanasema iwapo sheria hiyo isingelikuwepo , ajali iliyosababishwa na rubani mwenza aliyekuwa amezongwa na mawazo isingelitokea.
Wachunguzi hao pia wanasema haifai kuwa marubani wanaruhusiwa wenyewe kujitathmini hali yao ya kiafya.

Wednesday, February 10, 2016

 
Marehemu Idi Amin Dada aliiongoza Uganda kwa miaka minane kati ya mwaka wa 1971 hadi 1979
Mgombea wa urais katika uchaguzi mkuu ujao nchini Uganda ameahidi kurejesha nyumbani mabaki ya aliyekuwa rais wa nchini hiyo Idi Amin Dada na kuujengea makavazi.
Aliyekuwa waziri mkuu wa Uganda Amama Mbabazi,alisema endapo atachaguliwa kuwa rais azimio lake la kwanza itakuwa kuwapatanisha waganda wa kila tabaka na kabila.
Kwa madhumuni hayo anapanga kuwaleta pamoja watu anaohisi kuwa wanaomuunga mkono Idi Amin wale waliomuunga mkono Milton Obote na wale wanaomuunga mkono rasi wa sasa Yoweri Kaguta Museveni.
Viongozi hao watatu ndio waliochangia kwa njia moja au nyengine mwelekeo wa kisiasa wa Uganda.

Amama Mbabazi ameahidi kurejesha nyumbani mabaki ya aliyekuwa rais wa nchini hiyo Idi Amin Dada na kuujengea makavazi.
Marehemu Idi Amin Dada aliiongoza Uganda kwa miaka minane kati ya mwaka wa 1971 hadi 1979 utawala ambao ulishuhudia mauaji ya wapinzani wake wengi.
Vilevile anatuhumiwa kwa kuwatimua wahindi wote nchini Uganda kabla ya kupinduliwa na Milton Obote.
Marehemu Idi Amin aliaga dunia akiwa uhamishoni nchini Saudi Arabia.
Rais Yoweri Museveni, anatarajiwa kuchaguliwa tena kuongoza taifa hilo la Afrika Mashariki kwa hatamu ya tano.

Chifu Mandla Mandela taabani kwa kuukubali Uislamu 
Hatua ya mjukuu wa kiongozi mwanzilishi wa Afrika Kusini Nelson Mandela , Mandla, 42, kuslimu na kuoa mke wa nne imevutia hisia kali kutoka kwa viongozi wa kabila lake la AbaThembu.
Wazee hao viongozi wenza wa kabila la Mvezo iliyokuwa ya marehemu ya Mandela ''hawaamini kuwa Chifu mzima wa kabila la Mvezo anaweza kuasi tamaduni zake na kuiga zile za mke wake ''
Mandla alifunga ndoa yake ya nne na bi Rabia Clarke katika msikiti mmoja mjini Cape Town Afrika Kusini mwishoni mwa juma.

Rais Magufuli 

Serikali ya Tanzania imebaini wizi wa takribani shilingi milioni 700 sawa na dola laki tatu za marekani ($320,000 )katika shirika lake la Ndege (ATCL) kupitia kampuni ya wakala wa ukatishaji tiketi ya Salama World Travel iliyopo visiwa vya Comoro.