Saturday, August 29, 2015

 Mgombea wa Urais kwa kupitia Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa
 kijiji cha Kikondo kata ya Ilungu Mbeya vijijini akiwa njiani kuelekea mkoa wa Njombe .

Friday, August 28, 2015

 
Wanajeshi wa waasi CAR
Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya watoto UNICEF, limesema kuwa makundi yaliyojihami nchini Jamuhuri ya Afrika ya Kati, yamewaachilia watoto mia moja sitini na watatu.
Watoto hao waliachiliwa mjini Batangafo, baada ya majadiliano kati ya shirika hilo na makundi hayo ya waasi mwezi Mei mwaka huu, kama sehemu ya mpango wa amani.
 
Treni
Afisa mmoja wa serikali ya Poland, amesema kuwa ana imani kuwa treni moja ya kijeshi ambayo imefichwa tangu vita vya pili vya dunia, zaidi ya miaka sababini iliyopita, na kusemekana kubeba vitu vya z

Mtu yeyote anapoingia katika maisha huwa anakabiliwa na changamoto ya kuamua kati ya kujiajiri au kuajiriwa. Kuajiriwa kunakuhakikishia usalama kazini japokuwa usalama huo siku hizi ni nadra sana kuwepo, wakati kujiajiri hukuhakimkishia uhuru wa kuamua mambo yako. Watu wengi huamua kuchagua kuajiriwa kwa sababu ni rahisi kuliko kuwa wajasiriamali ambako ni kugumu, tatizo wanalolipata ni kuwa wanaishi kwa kutegemea mshahara ambao huwa hautoshi na kujiingiza kwenye madeni mabaya ambapo hukopa kwa ajili ya matumizi na kuendelea kuwa na madeni makubwa zaidi. Kukopa siyo kubaya ila kuna madeni mabaya na madeni mazuri madeni mabaya ni yale ambayo mtu anakopa kwa ajili ya hela ya kula au kutumia, madeni mazuri ni yale ambayo mtu anakopa kwa ajili ya kuwekeza kwenye vitegauchumi au kwenye biashara kwa kufanya hivyo mtu anaweza kujitoa kwenye matatizo.

Thursday, August 27, 2015


Junaid Hussain
Marekani imesema mpiganaji wa Kiingereza, ambaye alijiunga na kundi la Islamic State ameuawa katika shambulio la anga nchini Syria.
Junaid Hussain ambaye alikuwa akiendesha kampeni za kundi hilo la Islamic State kupitia mitandao ya kijamii na kufanya kazi kubwa kuwavuta na kuwaingiza katika kundi hilo, raia wa kigeni.

Wednesday, August 26, 2015

Akihutubia mamia ya watu waliojaa leo huko sumbawanga

Tuesday, August 18, 2015


Mfanyabiashara tajiri kijana Mohamed Dewji
Mfanyabiashara maarufu nchini na Mbunge wa Singida Mjini (CCM), Mohammed Dewji (pichani) kwa mara ya kwanza ameingia kwenye orodha ya mabilionea 29, akiwa tajiri kijana kuliko wote barani Afrika.
Jarida la Forbes la Marekani limemtaja Dewji (39), katika nafasi ya 24 ya matajiri wa Afrika akiwa na utajiri wa Dola 1.3 bilioni za Marekani (Sh2.34 trilioni) unaotokana na biashara mbalimbali anazozifanya kupitia kampuni yake ya Mohammed Enterprises (Metl Group).“Dewji alibadilisha biashara aliyoanzisha baba yake kutoka uuzaji bidhaa na kuwa na viwanda vya Metl,” inasema sehemu ya habari inayomuhusu bilionea huyo Mtanzania .
 
Shambulizi la Thailand lalaaniwa
Waziri mkuu wa Thailand ametaja shambulizi la bomu ambalo limewauwa zaidi ya watu ishirini mjini Bangkok hapo jana jumatatu kuwa kisa kibaya zaidi kuwahi kutokea nchini humo.

Thursday, August 6, 2015





Imesubiriwa kwa shauku iliyoje, mengi yamesemwa lakini imefikia hatua ya mitandao mingi kufanya tukio hili kuwa habari iliyofika kwenye madawati yao hivi punde.
Kwa post hii ya Diamond kwenye ukurasa wake wa Twitter na Instagram dakika chache zilizopita ni dhahiri kuwa familia ya Wasafi imepata ongezeko la mtoto wa kike.

Wednesday, August 5, 2015

 
Je unamfahamu Edward Lowassa ni nani katika siasa za Tanzania ?
Umoja usio rasmi wa vyama vinne vya upinzani nchini Tanzania unajulikana kwa jina la Katiba ya Wananchi (UKAWA), baada ya kusubiri kwa muda hatimaye umemtangaza Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa kuwa mgombea wake wa urais.
Lowassa anagombea kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), huku vyama vingine vitatu vikimuunga mkono. Hii inatokana na sheria za Tanzania ambayo haitambui umoja wa vyama.
Kabla ya kujiengua chama Tawala chama cha Mapinduzi CCM, Edward Lowassa amekuwa mwanachama wa CCM kwa muda wa miaka 38, ambapo alijiunga na chama hicho mara tu baada ya kumaliza elimu yake ya chuo kikuu mwaka 1977.

Tuesday, August 4, 2015

 NUH & SHISHI
Kuna sauti ambayo imerekodiwa na kinachosikika ni sauti ya mwanamke na mwanaume wakijibizana, waliotajwa kwamba ndio wanaosikika kwenye sauti hiyo ni Nuh Mziwanda na Wema Sepetu, imemfikia Soudy Brown tayari !!
Soudy Brown anasema sauti hiyo ilirekodiwa usiku mmoja kabla ya Tuzo za KTMA, na baada ya ishu kuwafikia wote wawili yani Nuh na mpenzi wake Shilole haijulikani nini kinaendelea kati yao kwa sasa.
Sauti yote iko hapa mtu wangu, ukiplay utawasikia wote ilivyokuwa kwenye U Heard August 03 2015