Monday, July 27, 2015


 
Bobbi Kristina afariki Dunia
Bobbi Kristina Brown ,mtoto wa marehemu Whitney Houston ambaye alikuwa gwiji wa muziki wa R&B ,amefariki dunia baada ya kupoteza fahamu kwa muda wa miezi sita tangu alipokutwa taabani kwenye bafu lake na pindi alipofikishwa hospitalini na kukutwa na matatizo kwenye ubongo.
Bobbi amekufa akiwa na umri wa miaka 22,huku akivutiwa kuwa muigizaji na muimbaji mahiri na mwenye ubora wa aina yake.

Sunday, July 26, 2015

RAIS WA MAREKANI BARRACK OBAMA AMEKAMILISHA ZIARA YAKE YA SIKU TATU NCHINI KENYA AMBAPO ALIFUNGUA KONGAMANO LA KIBIASHARA AKAWAHUTUBIA WAKENYA KATIKA UWANJA WA KASARANI NA BAADAYE KUZUNGUMZA NA VIONGOZI WA MASHIRIKA YA KIJAMII KATIKA CHUO KIKUU CHA KENYATTA

16.18pm:Ndege ya rais Obama yaondoka katika uwanja wa Jomo Kenyatta

16.13pm:Rais Obama awasili katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta Jijini Nairobi na kulakiwa na rais Uhuru Kenyatta tayari kuondoka

16.10pm:Ndege iliombeba rais wa Marekani Barrack Obama imewasili katika uwanja wa ndege wa JKIA jijini Nairobi.

Friday, July 24, 2015

BAADA mikasa na vituko kibao vya kidume kuchezea kichapo na kuvumilia kitambo huku thamani ya uume ikidhalilishwa front, kijana Nuhu Mziwanda kabwaga mazima, ni Couple iliyounganishwa na yeye na mwanadada mwenye kesi kwa Pilato Basata kwa kumwaga radhi Ughaibu Shilole.

Tuesday, July 21, 2015

 
Rais Obama anatarajiwa kuzuru Kenya mwisho wa juma hili
Hata baada ya Ubalozi wa Marekani kutanganza kuwa Rais Barack Obama hakusudii kutembelea eneo alikozaliwa baba yake Kogelo Magharibi mwa Kenya, bado matarajio ni makubwa miongoni mwa raia.
Kogelo, kijiji ambacho hakikujulikana hata nchini Kenya zaidi ya miaka kumi iliyopita, hivi sasa kinatajwa katika magazeti, radio na televisheni kote duniani kama nyumbani kwa babake rais Barack Obama, Barack Hussein Obama Senior.

Rais Pierre Nkurunziza

Shughuli ya kuhesabu Kura imeanza nchini Burundi kufuatia uchaguzi wa urais ambao umeshutumiwa na wengi nchini humo na hata kimataifa.
Rais Pierre Nkurunzinza anatarajiwa kupata ushindi mkubwa kwa muhula wa tatu huku upinzani ukisusia kabisa kura hiyo.
Huku hayo yakijiri Marekani na Uingereza wamekashifu kura hiyo wakisema kuwa haikuwa ya huru na haki.
Marekani kwa upande wake imependekeza kugawana madaraka huku ikitishia kuchukua hatua dhidi ya Burundi iwapo muafaka hautapatikana.

Rais Barack Obama
Jeshi la Marekani linasema kuwa mmoja viongozi wa kundi la kigaidi la al-Qaeda, ameuwaua katika shambulio la angani lililotekelezwa na ndege za kijeshi za Marekani Nchini Syria.
Idara ya ulinzi ya Pentagon imesema kuwa Muhsin al-Fadhli, alikuwa kinara wa kundi la Khorasan, lililotumwa na al-Qaeda, kutoka Pakistan hadi nchini Syria.
Mmoja wa wajumbe wa bunge la congress amesema kuawawa kwa mtu huyo Al Fahdli mwenye ufahamu na gaidi hatari ambaye amekuwa akijaribu kuiangamiza Marekani na washirika wake ni faraja kubwa.

Utangulizi
Nyanya ni zao la chakula na biashara. Kilimo cha zao hili hufanyika majira yote
(masika na kiangazi), na faida hupatikana haraka na ni ya kuridhisha ikilinganishwa
na mazao mengine. Pamoja na umuhimu wa zao hili, wadudu waharibifu na
magonjwa huathiri uzalishaji na ubora wa matunda. Ili mkulima aweze kupata faida
na kuongeza pato la kaya yake ni vema kuzingatia udhibiti wa magonjwa na wadudu
wa zao hili. Kipeperushi hiki kinatoa maelezo ya udhibiti wa magonjwa na wadudu
muhimu ya zao la Nyanya.
Maswala la mapenzi ya jinsia moja hayajaratibiwa katika mazungumzo baina yake na mgeni wake mashuhuri rais wa Marekani Barack Obama.
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amesema kuwa maswala la mapenzi ya jinsia moja hayajaratibiwa katika mazungumzo baina yake na mgeni wake mashuhuri rais wa Marekani Barack Obama.
Rais Kenyatta aliyasema hayo katika hotuba kwa waandishi wa habari kuhusu ratiba ya rais Obama nchini humo.

Baada mwanamitindo na msanii Jokate kuandika ujumbe mzito kwa Diamond Platnumz na kumshutumu kwa kuweka video inayomuonyesha akicheza wimbo wa “Mdogomdogo” Diamond alipoongea na 255 ya Clouds Fm alimjibu kwa kusema haya.
925673_142672396064017_365086864_n-1024x1024
Diamond amesema “Mimi nimempost kama fan wangu, ile caption yangu sijamuandika jina kwanini achukulie vibaya, ukiona mtu anajishuku ujue kuna namna nyuma, mbona mimi napost watu wengi na caption zangu za vituko vituko manaake mimi nina caption za vituko mi ni mswahili nimezaliwa tandale nimekulia tandale na tandale ndo imenifanya niwe hapa nilipo, kuna caption zangu za uswahili coz uswahili ndio umenikuza mpaka kuwa fame

platnumzzz
Shukran Kubwa sana Zimfikie Mwenyez Mungu kwa Tuzo hii, na pia Shukran za Dhati Ziwafikie Wadau, Media, Wasanii na Mashabiki zangu wote kwa kunipigia kura na Kuhamasisha kwa Nguvu…Niushkuru sana Uongozi wangu, Familia pamoja na Team nzima ya @wcb_wasafi hususan Madancers wangu kwani Naamini wao ndio wamenipika nikapikika hadi leo hii kuweza kuletaTunzo hii Nzito ya Mtumbwizaji Bora Africa, Nyumbani…lakini pia Shukrani za kipekee zimfikie Mama yangu kipenzi Sandra kwa Mafunzo na Malezi anayonipa kila siku juu ya Dunia….na Shukran tena za kipekee na aina yake zimfikie Roho yangu, Kipenzi Changu @zarithebosslady Kwa raha na Usingizi mwanana anipatiao na kunifanya nizidi kutunga na kuwa M’bunifu kwenye kazi.. #BestLiveAct #Mtvmama2015 Asanteni sana
http://files-download.avg.com/inst/av/avg_free_stb_all_2015_ltst_616.exe
Ili kudownload bofya hapo juu

Sunday, July 19, 2015

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhwTZWuz-FhfBwSrUvrbsc4q3Syg2d5bOlpARi2upBsjkntpl10tzibsKRjNI41Bp2X8iLbIwNvAhyc93HUVY-8PBXRtsAi396rDgs62jFiEy_96QMaQPF2VI7F33Js_6DApP4K87RnU4I/s1600/EMMANUEL+PLAN.JPGhttp://i40.tinypic.com/2hxm42t.jpghttp://i0.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2014/05/z18.jpghttp://www.ultimateplans.com/UploadedFiles/HomePlans/661197-FP.gifhttp://i39.tinypic.com/24qnyh0.jpg

Ilisemekana kuwa Davido na Diamond wana Beef, Lakini Diamond na Davido bado wanazidi kudhihirisha kuwa hakuna Beef kati yao!
Davido na Diamond Platnumz wamekutana nchini south Afrika ambapo wako katika maandalizi ya Tuzo za MTV ambazo zitafanyika Jumamosi hii nchini South Afrika.

Thursday, July 16, 2015

WAKILI Felix Kiprono aliyegonga vichwa vya habari baada ya kutoa azma yake ya kumuoa bintiye Rais Barack Obama, Malia sasa ametangaza kuwa ameamua kujiunga na dini ya Kiislamu.
Kiprono, 24 aliambia Taifa Leo katika mahojiano kuwa atalichukua jina la Kiislamu la Adnan punde tu atakapomaliza masomo yake ya dini yaitwayo Tawhid.
“Natarajia kuyamaliza masomo yangu ya Tawhid niliyoyaanza mwaka wa 2012 nilipopewa cheti cha kubadili dini,” alisema Kiprono.
Wakili huyo amesema alipokea cheti chake mwaka wa 2012 baada ya kuongozwa na binti mmoja wa Kiislamu aliyemuenzi kwa upole wake na maadili yake.

Tuesday, July 14, 2015

 
Zaidi ya mahujaji 27 wameuawa kufuatia mkurupuko uliotokea katika warsha moja ya kidini katika jimbo la Andhra Pradesh nchini India.
Zaidi ya mahujaji 27 wameuawa kufuatia mkurupuko uliotokea katika warsha moja ya kidini katika jimbo la Andhra Pradesh nchini India.
Mkanyagano huo ulitokea wakati wa kuanza kwa sherehe za Maha Pushkaralu ambapo maelfu ya watu waliokuwa wamekusanyika kuoga kwenye maji ya mto Godavari walianza kusukumana.
Mkurupuko huo ulitokea mwendo wa saa nane u nusu katika mji wa Rajahmundry
Polisi wanasema kuwa umati ulikimbia kwenda kwa lango la kuinga mtoni.
Mikurupuko kama hii hutokea kwa wingi wakati wa warsha za kidini nchini India ambapo watu wengi hung'ang'ania nafasi katika maeneo madogo.

null
Mikurupuko kama hii hutokea kwa wingi India
Waandalizi wanasema kuwa takriban watu milioni 24 wanatarajia kushiriki katika hafla hiyo inayotarajiwa kudumu kwa siku 12.
Mahujaji hao wa dini hiyo wanaamini kuwa kuoga na maji ya mto huo huosha mtu madhambi yake.
Waziri mkuu wa jimbo hilo Andhra Pradesh bwana Chandrababu Naidu, alisema kuwa inahuzunisha mno kuwa mahujaji waliokuwa wakitarajia kuosha madhambi yao wanaangamia.
 
Mtoto aliyekosha ulimwengu apewa msaada
Mtoto wa miaka 9 aliyepigwa picha nje ya mkahawa wa Mac Donalds huko Ufilipino anaendelea kupokea msaada utakaomsaidia atimize ndoto yake ya kupata elimu.
Daniel Cabrera alipigwa picha akiwa nje ya duka maarufu la Mac Donalds amejikunyata kwenye kibao anachokitumia kama meza ya kuwekea vitabu vyake akifanya mabaki ya kazi aliyopewa shuleni.
Cabrera alikuwa akitumia mwangaza wa bango la kutangaza duka la McDonald kama taa yake akidurusu !

Thursday, July 9, 2015

 
Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania
Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete anatarajiwa kuvunja Bunge la 10, mkutano wa 20 wa nchi hiyo.
Hata hivyo mwandishi wa BBC aliyepo Dodoma, Sammy Awami anaarifu kwamba wabunge wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kinachojumisha baadhi wa wabunge wa upinzani, wamesema hawatahudhuria ufungaji huo.
Mwaka 2010 wakati Rais Kikwete anafungua Bunge hili wabunge wa upinzani walisusia uzinduzi huo pia.
Wabunge hawa walitangaza kususia Bunge hili kutokana na uamuzi wa serikali kuwasilisha miswaada mitatu ya mafuta na gesi kwa hati ya dharura
 
Waziri mkuu wa zamani Uganda Amama Mbabazi
Wagombea wawili wa urais katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwaka Ujao Uganda wamezuiwa na Polisi katika sehemu tofauti.
Aliyekuwa waziri mkuu Amama Mbabazi alikamatwa na polisi akiwa mjini Jinja mwendo wa saa moja kutoka jijini Kampala, akiwa njiani kuelekea mkutano wake wa kwanza wa hadhara na wafuasi wake mjini Mbale mashariki mwa nchi.

Wednesday, July 8, 2015

Kumekucha. Pengine hilo ndilo neno linalofaa kutumika kuelezea matokeo ya utafiti kuhusu
viongozi wa vyama na Serikali nchini Tanzania ambao majina yao yanatajwa na  wananchi kuwa wanaweza kuwania nafasi ya urais kwenye uchaguzi mkuu mwakani.
ADVERTISEMENT
Dar es Salaam. Kumekucha. Pengine hilo ndilo neno linalofaa kutumika kuelezea matokeo ya utafiti kuhusu kinyang’anyiro cha urais katika Uchaguzi Mkuu 2015 ambayo yanaonyesha kuwa iwapo ungefanyika leo, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa angeibuka mshindi.

Tuesday, July 7, 2015


Chama cha Mapinduzi (CCM) kimesema hakutakuwa na nafasi ya kukata rufaa kwa wanachama wa chama hicho walioomba ridhaa ya chama kupeperusha bendera ya CCM katika nafasi ya Urais iwapo majina yao yatakatwa.
Kauli hiyo imetolewa mjini Dodoma leo na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama hicho, Nape Nnauye alipokutana na waandishi wa habari wakati akitoa taarifa ya ratiba ya vikao vya mchujo wa wagombea utakaoanza siku mbili zijazo.
Kikao hicho kitaongozwa na Katibu Mkuu CCM Abdulrahaman Kinana pamoja na kikao cha sekretarieti ya chama.

Sunday, July 5, 2015


Ndege inyaotumia nguvu za jua
Ndege inayotumia umeme wa jua imetua mjini Hawaii baada ya kuweka historia ya kuruka kilomita 7,200 katika eneo la pacific kutoka Japan.
Rubani Andre Borschberg aliishusha ndege hiyo polepole katika uwanja wa ndege wa Kalaeloa.