Sunday, March 13, 2016


Germanwings: Madaktari watoe siri za marubani
Wachunguzi kutoka Ufaransa, wamependekeza sheria kali inayozuia madaktari kufichua siri za marubani wagonjwa iondolewe.
Wanasema iwapo sheria hiyo isingelikuwepo , ajali iliyosababishwa na rubani mwenza aliyekuwa amezongwa na mawazo isingelitokea.
Wachunguzi hao pia wanasema haifai kuwa marubani wanaruhusiwa wenyewe kujitathmini hali yao ya kiafya.