Friday, May 29, 2015

Benki ya Afrika ya Maendeleo, ADB imepata rais mpya, waziri wa kilimo wa Nigeria Akinwumi Adesina, ambaye amewashinda wapinzani 7 katika duru 6 za uchaguzi. Anachukua nafasi ya Donald Kaberuka anayemaliza muda wake.
Akinwumi Adesina, rais mteule wa Benki ya Afrika ya Maendeleo, ADB. Akinwumi Adesina, rais mteule wa Benki ya Afrika ya Maendeleo, ADB.
Akinwumi Adesina aliibuka mshindi baada ya duru sita za uchaguzi, zilizomalizika jana jioni katika makao makuu ya Benki ya Afrika ya Maendeleo mjini Abidjan, Cote d'Ivoire. Adesina, msomi mwenye shahada ya uzamili katika masuala ya uchumi na maendeleo, anachukua hatamu za benki hiyo ambayo inajikuta katika mazingira mapya kifedha barani Afrika.
Baada ya kupata ushindi wa karibu asilimia 60 ya wajumbe wa bodi ya magavana wa benki hiyo, Akinwumi Adesina alisema atakuwa rais mwenye kujituma.
Rais mpya wa Nigeria Muhammadu Buhari leo (29.05.2015) anaapishwa rasmi ili kuanza kuingia madarakani Viongozi kutoka Afrika na sehemu nyingine za dunia wanahudhuria sherehe za kuapishwa Rais huyo mjini Abuja.
Rais mpya wa Nigeria Muhammadu Buhari Rais mpya wa Nigeria Muhammadu Buhari
Nigeria leo inakianza kipindi kipya cha historia.Wengi wanatathmini kuapishwa kwa Jenerali Buhari kuwa tukio muhimu kabisa katika historia ya Nigeria.
Kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi hiyo yenye watu karibu Milioni 178 mabadiliko ya uongozi yamefanyika baada ya uchaguzi wa amani.

Saturday, May 23, 2015


HUDUMA  za kijamii mkoani Mtwara jana zilisimama kutokana na baadhi ya wananchi kudai kuwa wanaomboleza vifo vya watu vilivyotokea wakati wa
vurugu za gesi hivyo kupelekea huduma za kijamii kusimama.
 
Mmoja wa wananchi walioathiriwa na mgomo huo, Hilal John aliyekuwa safarini kuelekea Newala lakini alikosa usafiri kutokana na kumbukumbu hiyo alisema hatua hiyo imeathiri wananchi wa hali ya chini.
 
Alisema hali hiyo imesababisha wasafiri wanaokwenda wilaya zote pamoja na baadhi ya mikoa kushindwa kuondoka  kutokana na kutokuwepo kwa huduma hiyo kwa siku nzima ya jana.
 
Si hivyo tu, maduka mbalimbali nayo yalifungwa na hivyo kusababisha baadhi ya watu kukosa huduma hizo.

Thursday, May 21, 2015

benkaozlee
   
mshirikishe mwenzako


Burundi: rais aonekana akicheza licha ya maandamano

Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza ameonekana akicheza mpira pamoja na marafiki zake mjini Bujumbura licha ya mgogora wa kisiasa nchini mwake.

Rais Nkurunziza ni kocha aliyehitimu
Rais Nkurunziza,alikuwa akisakata kabumbu ndani ya mji mkuu wa Bujumbura mji uliokumbwa na maandamano makubwa tangu atangaze nia ya kuwania awamu ya tatu uongozini.
Hii leo habari kutoka Burundi zinasema kuwa mtu mmoja amepigwa risasi na kuuawa katika mji mkuu wa Bujumbura.

Rais Nkurunziza alikuwa akicheza dhidi ya marafiki zake
Mtu huyo alikuwa miongoni mwa waandamanaji wanaopinga hatua ya rais Pierre Nkurunziza kugombea urais kwa awamu ya tatu.
Walioshuhudia wanasema kuwa polisi walimpiga mwandamanaji huyo risasi mgongoni wakiwa katika eneo la Musaga linalotazamwa kama ngome ya upinzani.

Mechi hiyo ilikuwa mjini Bujumbura
Waandamanaji walijaribu kufika katikati mwa jiji la Bujumbura lakini walitimuliwa kwa mabomu ya moshi wa kutoa machozi.
Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza, amewaomba zaidi ya raia laki moja na hamsini waliokimbia ghasia nchini humo katika majuma kadhaa yaliyopita, warejee nyumbani.

Rais Nkurunziza anatimu yake ''Hallelujah FC ''
Katika hotuba kwenye runinga ya taifa, amesema kuwa asilimia tisini na tisa nukta tisa ya Burundi ina amani.
Anasema kuwa hakuna mtu yeyote anayetaka kufufua taharuki ya kikabila.



Tuesday, May 19, 2015

Ilikuwa ni shangwe na furaha pindi watu walipoweza kuona uimbo huu kwenye akaunti yangu ya fb na nika ona siyo vyema kuwaacha hihivi bila kuwaonjeshana nyinyi mashabiki zangu mnaonisapoti kwa kucheki nafanya nini kwenye akaunti yangu
Posted by benkaozlee

Friday, May 15, 2015


Nawaleta hawa kwenu

Thursday, May 14, 2015

Watch this my fans if you like you can comment on this


KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, wanafunzi wa shule za msingi za Mwangaza na Ngarenaro, juzi walidaiwa kupata kipigo kutoka kwa vijana waliojiita ‘Makamanda’ wa umoja wa vyama vya siasa vya upinzani ujulikanao kama Ukawa, baada ya baadhi yao kufika katika mkutano huo uliofanyika viwanja vya karibu na shule yao.
 
Baadhi ya viongozi wakuu wa umoja huo, akiwemo mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu, Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi) na Mbunge wa Arusha Mjini kwa tiketi ya Chadema, Godbless Lema, walishuhudia kitendo hicho, lakini cha kushangaza hawakuchukua hatua yoyote ya kuwazuia vijana hao kuwachapa watoto mijeledi kwa kisingizio kuwa hawakustahili kuwepo uwanjani hapo.
 
Hatua hiyo imekuja licha ya kuwa umoja huo ulikuwa unafanya mkutano wake katika eneo la shule ya Msingi Ngarenaro, uwanja ambao hutumika na shule za msingi za Ngarenaro na Mwangaza pamoja na shule ya Sekondari ya Ngarenaro.

Tuesday, May 12, 2015

 BEN POL KUJA NA REMIX YA SOPHIA KUTOKA CONGA MUSIC...
 
 Waweza pia kucheki na kudownload video kutoka kitaa kwetu blog

Wednesday, May 6, 2015


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki moon amelaani vikali shambulizi la waasi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambalo limeuwa wanajeshi wawili wa umoja huo ambao wanatoka Tanzania.
Wanajeshi wa Umoja wa Mataifa wakifanya doria Mashariki mwa Kongo
Shambulizi hilo lilifanywa Jumanne jioni katika kijiji cha Kisiki, umbali wa km 38 Kaskazini mwa mji wa Beni. Mbali na wanajeshi wawili waliouawa na 13 ambao walijeruhiwa, wengine wapatao 4 hawajulikani walipo.
Wanajeshi wa Tanzania ambao ni sehemu ya kikosi maalumu cha kuingilia kati walikuwa wakifanya doria walipofanyiwa shambulizi hilo na watu wanaoaminika kuwa waasi wa Allied Democratic Forces (ADF) kutoka Uganda.

Sunday, May 3, 2015

Tarehe May 3, 2015
Bomu lajeruhi watu watano mkoani Morogoro.
Bomu lajeruhi watu watano mkoani Morogoro.
Vijana wawili wanatafutwa na jeshi la Polisi mkoani Morogoro kwa kumrushia bomu dereva wa gari la mwenyekiti  wa Halmashauri ya wilaya ya Kilombero, David Ligazio ,Novatus Ngope (47), pamoja na kujeruhi watu wengine wanne walipokuwa kwenye sherehe za Siku ya Wafanyakazi Duniani juzi.
Bomu hilo liliwajeruhi watu hao walipokuwa kwenye maadhimisho hayo yaliyofanyika katika kijiji cha Msolwa Ujamaa, Kata ya Sanje ,wilayani Kilombero, mkoani Morogoro
Kwa mujibu wa Mkuu wa wilaya ya Kilombero, Lephy Gembe alithibitisha kutokea tukio hilo  na kusema tukio hilo lilitokea majira ya saa 2:00 usiku wa Mei Mosi mwaka huu eneo la Kijiji cha Sanje.
Alisema vijana wawili wanaotuhumiwa kurusha mlipuko huo baada ya kuwajeruhi watu hao watano, walifanikiwa kukimbia kutoka eneo la tukio na jeshi la  Polisi inaendelea kuwasaka ili sheria ichukue  mkondo wake.

Tarehe May 2, 2015
44
Mwanamuziki Naseeb Abdul, na mrembo Zari wakiingia ukumbini
22
Wanamuziki Nay wa Mitego na Shetta wakiwa katika pozi
11
Mwanamuziki Diamond akifanya majonjo kwa mama kijacho wake Zari
1111
Baadhi ya warembo waliotoa huduma katika hafla hiyo
5545
Baadhi ya warembo waliotoa huduma katika hafla hiyo

Tarehe May 2, 2015
Mwanamuziki Peter Okoye katika pozi
Mwanamuziki Peter Okoye katika pozi
Wanamuziki nchini Nigeria, Peter na Paul Okoye, wamekuwa wakikwaruzana mara kwa mara kiasi cha kuwashangaza watu kuwa iwaje ndugu wa damu wanakosana wakati wanafanya kazi kama timu.
Hatua hiyo imepelekea Peter, kuweka wazi kuwa, kugombana kwao kusichukuliwe kama kitu cha ajabu kwani nao ni binadamu hivyo kukosana kupo na hakupingiki.
Amesema kuwa kutofautiana kwao ni jambo la kawaida na imekuwa ikitokea hivyo mara nyingi lakini baadaye maisha yanaendelea.
Ameongeza kuwa huwa inatokea kutofautiana kwa hapa na pale kama walivyo binadamu wengine na baadaye kumaliza tofauti zao na kufanya kazi.
Amesema kuwa wao ni kama wanandoa walioishi kwa zaidi ya miaka 20 hivyo kukosana kupo na kama binadamu hupatana na kupanda jukwaani kufanya makamuzi kama kawaida bila watu kujua kama wamegombana.

Tarehe May 3, 2015
Msanii wa filamu nchini Tanzania, Weru Sengo katika pozi
Msanii wa filamu nchini Tanzania, Weru Sengo katika pozi
Wasanii Steve Nyerere na Weru Sengo, katika pozi
Wasanii Steve Nyerere na Weru Sengo, katika pozi
Msanii wa filamu nchini Tanzania, Weru Sengo anadaiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na msanii mwenzake Steve Nyerere, ambapo wamekuwa wakionekana sehemu mbalimbali wakila bata.
Inadaiwa kuwa badala ya kutoka katika matembezi au kula bata na mke wake, Steve, amekuwa akitoka na Weru, jambo ambalo watu wameona sio la kulifumbia macho na inadaiwa kuwa hata katika shoo ya Zari, walikuwa wote na kumuacha mke wake.
Vyanzo hivyo vimedai kuwa Steve, aweke bayana kama ameamua kuoa mke wa pili bila kumshirikisha mke wake kabla hawajamfanyia maandamano kama wanawake kutokana na mke wake kuwa mvumilivu na mtu anayejiheshimu.
Chanzo hicho kimetoa wito kwa mke wa Steve kumpenda mume wake zaidi ya mwanzo, kama amesikia au kuona kitu ni kawaida kwenye ndoa kupata majaribu, hivyo asimame kama mama na kudai kuwa lazima kama mke anajua udhaifu wa mume wake na kumtaka amkamatie hapo kwenye udhaifu bila kusahau kumuomba Mungu.
Kwa mujibu wa mke wa Steve, Suzy Cleo, amesema kuwa anashukuru kwa ushauri alioupata kutoka cha chanzo makini na kudai kuwa atahakikisha kuwa hatatikisika kama mwamba wa mlima Sayun

Rio Ferdinand akiwa na mkwewake Rebecca Ellison enzi za uhai wake
Rio Ferdinand akiwa na mkwewake Rebecca Ellison enzi za uhai wake
Rebecca Ellison ambaye alikuwa ni mke wa mlinzi wa zamani wa klabu ya Manchester United na timu ya taifa ya Uingereza Rio Ferdinand amefariki dunia baada ya kusumbuliwa na maradhi ya kansa kwa muda mfupi.
Rebecca alizaa watoto watatu na Ferdinand, watoto wao wanafahamika kwa majina ya Lorenz, Tate na Tia.
Habari hizi zimemdhoofisha Ferdinand wakati huu mgumu wa ligi kuu ya soka Uingereza, Ferdinand kwa sasa anapambana kwenye kikosi chake cha Queens Park Rangers kuhakikisha kinasalia kwenye likgi kuu kwa msimu ujao.

Tarehe May 1, 2015
Pacquiao (kushoto) akiwa na Mayweather na rekodi zaokwa pamoja
Pacquiao (kushoto) akiwa na Mayweather na rekodi zaokwa pamoja
Kuelekea pambano la ndondi la kukata na shoka kati ya Floyd Mayweather Jr dhidi ya Manny Pacquiao ‘Pac Man’ kuna orodha ya mabondia watano ambao kwa nyakati tofauti wamewahi kupambana na Mayweather na Pacquiao.
Na hivi ndivyo namna ambavyo kila mmoja aliwashinda wapinzani hao.
OSCAR DE LA HOYA
Mayweather alishinda, ilikuwa ni mwaka 2007
Pacquiao alishinda, ilikuwa ni mwaka 2008
Kwa mujibu wa wachambuzi wa mchezo huo wanasema kuwa, Pacquiao alishinda kwa mbinu bora zaidi.
Floyd Mayweather akimchapa konde la maana usoni mpinzani wake Oscar de la Hoya
Floyd Mayweather akimchapa konde la maana usoni mpinzani wake Oscar de la Hoya
Manny Pacquiao akimchakaza pia De La Hoya na kumsababishia kustaafu masumbwi rasmi
Manny Pacquiao akimchakaza pia De La Hoya na kumsababishia kustaafu masumbwi rasmi
RICKY HATTON
Mayweather alishinda kwa Techinical Knock Out mwaka 2007, tarehe 10
Pacquiao alishinda kwa Knock Out tarehe , 2009
Katika hili pambano Pacquiao anapewa faida kwa kushinda kwa ubora zaidi ya Mayweather
Hapa anasema; “Bado narudia kwa kusema kuwa Floyd anatakiwa kujifunza zaidi namna ya kumpiga huyu”, De La Hoya.
Mayweather akipambana na Ricky Hatton
Mayweather akipambana na Ricky Hatton
Pacquiao akionekana kumchakaza Ricky Hatton kiasi cha kupoteza fahamu kabisa katika mzunguko wa pili tu
Pacquiao akionekana kumchakaza Ricky Hatton kiasi cha kupoteza fahamu kabisa katika mzunguko wa pili tu
JUAN MANUEL MARQUEZ
Mayweather alishinda mwaka 2009
Pacquiao alidroo mwaka 2004
Pacquiao alishinda mwaka 2008
Pacquiao alishinda kwa pointi za majaji 2011
Pacquiao alipoteza kwa Knock Out katika raundi ya 6 mwka 2012
Hapa karata imemuangukia Mayweather.
Mayweather akipambana na Manuel Marquez
Mayweather akipambana na Manuel Marquez
Marquez alimpa Pacquiao wakati mgumu sana, lakini alisubiri mpaka pambano la mwisho kati ya mapambano 4 kumshinda Pacquiao
Marquez alimpa Pacquiao wakati mgumu sana, lakini alisubiri mpaka pambano la mwisho kati ya mapambano 4 kumshinda Pacquiao
SHANE MOSLEY
Mayweather alishinda mwaka 2010
Pacquiao alishinda mwaka 2011
Mayweather akimuadhibu Mosley
Mayweather akimuadhibu Mosley
Mosley akipokea kichapo toka kwa Pacquiao
Mosley akipokea kichapo toka kwa Pacquiao
MIGUEL COTTO
Mayweather alishinda mwaka 2012
Pacquiao alishinda mwaka 2009
Mayweather vs Pacquiao: kwenye pambano hili Pacquiao alionekana kushinda kwa mbinu bora zaidi ya Mayweather.
Miguel anasema: “Manny ana kasi na nguvu. Manny yuko bora zaidi ya Mayweather”
Miguel Cotto akimtundika konde Mayweather kabla ya kushindwa katika raundi ya mwisho kabisa ya mchezo
Miguel Cotto akimtundika konde Mayweather kabla ya kushindwa katika raundi ya mwisho kabisa ya mchezo
Pacquiao akizichapa dhidi ya Cotto
Pacquiao akizichapa dhidi ya Cotto

Saturday, May 2, 2015


iunasikitishasana
KWANZA KABISA WANAANZA TOA JENEZA LA ALIEKUFA KWA UGONJWA NA KUZANIWA AMEROGWA NA ALIYEZIKWA AKIWA HAI MAANA KATIKA KABURI HILO WALIZIWA WATU WAWILI KATIKA KABURI MOJA  ALIE HAI NA MFU
JENEZA LA ALIEKUFA KWA UGONJWA TAYARI LIMETOLEWA HILO PEMBENI SASA ANAFUKULIWAALIEZIKWA HAI
MWILI WA ALIEZIKWA AKIWA HAI SASA UNATOLEWA KABURINI