Monday, December 28, 2015

Samia
Makamu wa rais wa Tanzania Bi Samia Suluhu Hassan alihudhuria mkutano huo
Chama cha Mapinduzi kimewataka wanachama wake visiwani Zanzibar kujiandaa kwa marudio ya uchaguzi.
Tamko hilo limetolewa huku mazungumzo hakiendelea kutafuta suluhu ya mzozo kuhusu matokeo ya uchaguzi wa Oktoba 25 ambayo yalifutiliwa mbali.
Wito wa wafuasi kujiandaa kwa marudio ya uchaguzi umetolewa baada ya kikao cha kamati maalum ya halmashauri kuu ya taifa ya CCM Zanzibar katika afisi kuu za chama Kisiwandui.

Saturday, December 12, 2015

Burundi
Watu zaidi ya 200 wameuawa Burundi tangu kuanza kwa machafuko Aprili
Miili zaidi ya 34 imepatikana katika barabara za mji mkuu wa Burundi huku machafuko yakiendelea.
Mwandishi wa BBC ameona maiti 21 katika mtaa mmoja wa Bujumbura na maafisa wa serikali wamesema kuna miili mingine 13.
Maiti nyingi zinaonekana kuwa za vijana waliouawa kwa kupigwa risasi, baadhi wakiwa wamefungwa mikono yao ikiwa pamoja mgongoni.
Miili hiyo imepatikana siku moja baada ya watu wenye silaha kushambulia maeneo matatu ya jeshi.
Hannibal
Hannibal amekuwa kwenye kizuizi cha nyumbani Oman tangu 2012
Mwana wa kiume wa aliyekuwa kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi, Hannibal, ameachiliwa huru baada ya kutekwa nyara kwa muda na kundi la wapiganaji, duru za kiusalama zinasema.
Kwenye video iliyoonyeshwa kwenye runinga ya Lebanon, mfanyabiashara huyo alionekana akiitisha habari zaidi kuhusu kutoweka kwa mhubiri mashuhuri wa dhehebu la Washia nchini Lebanon Musa al-Sadr. Al-Sadra alitoweka mwaka 1978. Alionekana kwenye video hiyo akiwa amejeruhiwa machoni.
Aliachiliwa huru katika mji wa Baalbek na kupelekwa mjini Beirut, polisi waliambia shirika la habari la AP.
Hannibal, 40, alipatiwa hifadhi na Oman mwaka 2012.

Friday, December 11, 2015

Tanzania
Tanzania na Nigeria ndizo nchi pekee zenye maabara ya aina hiyo Afrika kusini mwa jangwa la Sahara
Tanzania ni moja kati ya nchi zilizofanikiwa duniani kuratibu maabara inayohamishika kwa ajili ya mapambano dhidi ya Ebola na magonjwa mengineyo ya mlipuko.
Maabara hii inaweza kusafirishwa mpaka kwenye maeneo yaliyoathirika, ikiwa ndani ya masanduku yaliyofungwa vyema badala ya kusafirisha sampuli kwa ajili ya vipimo kutoka eneo moja kwenda jingine na kuwa katika hatari ya kuathiriwa na vijidudu vingine.

Tuesday, December 8, 2015

Jackson
Samuel L Jackson ni mmoja wa Wamarekani weusi waliofanikiwa sana Hollywood
Nyota wa Hollywood Samuel L Jackson atahamia Afrika Kusini iwapo Donald Trump atashinda uchaguzi wa urais Marekani, tovuti ya News 24 imeripoti.
Trump, mmoja wa wanaowania tiketi ya kugombea urais Marekani kupitia chama cha Republican, ameshutumiwa vikali baada ya kupendekeza Waislamu wazuiwe kuingia Marekani.
Haijabainika iwapo matamshi ya mwigizaji huyo, yaliyopeperushwa kwenye sehemu ya kipindi cha Jimmy Kimmel Live iliyorekodiwa awali Jumatatu, yalitolewa kabla au baada ya matamshi hayo ya majuzi zaidi kutoka kwa Trump.

Wednesday, December 2, 2015

 
Polisi wenye silaha wakipiga doria katika eneo palipotokea mauaji hayo.
Polisi nchini Marekani imesema takriban watu 14 wameuawa na wengine 14 kujeruhiwa baada ya kupigwa risasi na watu wenye silaha katika mji wa San Bernadino mashariki mwa Los Angeles.
Polisi mjini humo inasema tukio hilo imetokea kwenye kituo cha huduma kwa watu wenye ulemavu na inawezekana lilihusisha watu watatu wenye silaha ambao wametoroka kwa gari.
Watu hao wenye silaha wanasemakana walivyalia kijeshi na walitumia silaha za masafa marefu.
Mkuu wa kituo hicho cha watu wenye ulemavu palipoteka mauaji hayo ya kinyama anasema milio ya silaha ilisikika katika jengo lililokodishwa kwa ajili ya pati iliyoandaliwa na Idara ya Afya.

Saturday, November 28, 2015

Rais wa Uturuki Rcep Tayyip Erdogan ameonyesha kujuta kwamba Uturuki iliidungua ndege ya kijeshi ya Urusi karibu na mpaka wa taifa hilo na Syria,lakini hakuomba msamaha kwa tukio hilo.
Aliuambia mkutano wa hadhara huko Balikesir kwamba alitamani kwamba tukio hilo halingetokea na kwamba halitarudiwa tena.
Rais wa Urusi Vladmir Putin amekataa kulijadili swala hilo na Erdogan hadi atakapoomba msamaha.
Moscow inapanga kuiwekea vikwazo vya kiuchumi Uturuki na tayari imeanza kupitia safari za watalii.
Uturuki imewaonya raia wake kutosafiri Urusi kwa dharura.

Saturday, October 31, 2015

FULL-TIME: #LFC defeat Chelsea Football Club 3-1 at Stamford Bridge thanks to a Philippe Coutinho brace and a goal from substitute Christian Benteke.




Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wabunge ambao wataingia Bungeni baada ya uchaguzi Mkuu uliofanyika nchini kote Oktoba 25, 2015 ni kama ifuatavyo. 
Idadi kubwa ya wabunge hao ni kutoka chama tawala cha CCM, ikifuatiwa na Chadema na CUF na vyama vingine kama NCCR-Mageuzi na ACT-Wazalendo.
WABUNGE WALIOSHINDA KUPITIA CCM
Jimbo la Busega (Raphael Chegeni), Nyamagana (Stanslaus Mabula), Msalala (Ezekiel Maige), Ngara (Alex Gashaza), Kigamboni (Faustine Ndugulile), Kishapu (Suleiman Nchambi) na Kisarawe (Suleiman Jaffo).
Majimbo mengine ni Bagamoyo (Dk Shukuru Kawamba), Ilemela (Angelina Mabula), Ilala (Mussa Azzan ‘Zungu’), Singida Mjini (Mussa Sima), Same Magharibi (Dk Mathayo David Mathayo), Rungwe (Saul Amon), Mbogwe (Augustino Masele), Chalinze (Ridhiwani Kikwete), Iramba Magharibi (Mwigulu Nchemba) na Hanang (Dk Mary Nagu).
Aidha, majimbo mengine ni Njombe Kaskazini (Joram Hongoli), Dodoma Mjini (Antony Mavunde), Mtama (Nape Nnauye), Babati Vijijini (Jitu Soni), Kahama Mjini (Jumanne Kishimba), Sikonge (George Kakunda), Nzega Mjini (Hussein Bashe), Urambo (Margaret Sitta), Mpanda Vijijini (Moshi Kakoso) na Geita Mjini (Constantine Kanyasu).
Chama hicho pia kilijipatia ushindi katika majimbo ya Mbeya Vijijini (Oran Njeza), Mafinga Mjini (Cosato Chumi), Kalenga (Godfrey Mgimwa), Isimani (William Lukuvi), Songea Mjini (Leonidas Gama), Mkalama (Allan Kiula), Newala (George Mkuchika), Kavuu (Dk Prudenciana Kikwembe) na Kwimba (Mansoor Shanif).
Mengine ni Bukoba Vijijini (Jason Rweikiza), Nyasa (Stella Manyanya), Kondoa Mjini (Edwin Sanda), Kondoa Vijijini (Dk Kashatu Kijaji), Chemba (Juma Nkamia), Chamwino (Joel Mwaka), Mtera (Livingstone Lusinde), Bahi (Omar Baduel), Mpwapwa (George Lubeleje), Kibakwe (George Simbachawene) na Kongwa (Job Ndugai).
CCM pia imepata Sengerema (William Ngeleja), Maswa Mashariki (Stanslaus Nyongo), Maswa Magharibi (Mshimba Ndaki), Itilima (Njalu Silanga), Bariadi (Andrew Chenge), Meatu (Salum Hamis), Muheza (Balozi Adadi Rajabu), Kasulu Mjini (Daniel Nsanzugwanko), Buhigwe (Albert Ntabaliba), Handeni Vijijini (Mboni Mhita) na Morogoro Mjini (Abdulaziz Abood).
Gairo (Ahmed Shabiby), Rorya (Lameck Airo), Ngorongoro (William Ole Nasha), Mvomero (Suleiman Murad), Morogoro Kusini Mashariki (Mgumba Omary), Morogoro Kusini (Prosper Mbena), Nkasi Kusini (Deuderius Mipata), Nkasi Kaskazini (Ally Keissy), Singida Kaskazini (Lazaro Nyalandu), Singida Magharibi (Elibariki Kingu) na Igunga (Dk Dalaly Kafumu).
Mengine yaliyoenda CCM ni Solwa (Ahmed Salum), Katavi (Issac Kamwele), Mpanda Mjini (Sebastian Kapufi), Mpanda Vijijini (Moshi Kakoso), Nsimbo (Richard Mbogo), Ruangwa (Kassim Majaliwa), Sumbawanga Mjini (Aeshi Hilaly), Kyela (Dk Harrison Mwakyembe), Ileje (Janeth Mbene) na Mbarali (Pirmohamed Mulla).
Majimbo mengine yaliyochukuliwa na chama hicho ni Busokelo (Atupele Mwakibete), Vwawa (Japhet Hasunga), Lupa (Victor Mwambalaswa), Songwe (Philipo Mulugo), Madaba (Joseph Mhagama), Peramiho (Jenista Mhagama), Kilosa Kati (Mohamed Bawazir), Kiteto (Emanuel Papian), Mbulu (Paul Isaay) na Karagwe (Innocent Bashungwa).
Kyerwa (Innocent Bilakwate), Nkenge (Dk Diodorus Kamala), Muleba Kusini (Profesa Anna Tibaijuka), Muleba Kaskazini (Charles Mwijage), Biharamulo Magharibi (Mukasa Oscar), Mwibara (Kangi Lugola), Bunda Vijijini (Boniphace Getere), Makete (Dk Norman Sigala), Kibaha Vijijini (Hamoud Jumaa) na Sumve (Richard Ndassa).
Magu (Kiswaga Destery), Chato (Dk Merdad Kalemani), Nzega Vijijini (Dk Khamis Kigwangallah), Njombe Mjini (Edward Mwalongo), Mwanga (Profesa Jumanne Maghembe), Nyangh’wale (Hussein Kassu), Newala Vijijini (Rashid Akbal), Butiama (Nimrod Mkono), Korogwe Vijijini (Stephen Ngonyani) na Korogwe Mjini (Mary Chatanda).
Misungwi (Charles Kitwanga), Busanda (Lolensia Bukwimba), Manonga (Seif Gulamali), Tabora Mjini (Emmanuel Mwakasaka), Mlalo (Rashid Shangazi), Kisesa (Luhaga Mpina), Lindi Mjini (Selemani Kaunje), Mkinga (Dustan Kitandula), Mbinga Mjini (Sixtus Mapunda), Mbinga Vijijini (Martin Msuha) na Musoma Mjini (Vedastus Mathayo).
Mengine ni Geita Vijijini (Joseph Kasheku), Kibaha Mjini (Silvestry Koka), Bukombe (Dotto Biteko), Shinyanga Mjini (Steven Masele), Msalala (Ezekiel Maige), Pangani (Jumaa Aweso), Mufindi Kaskazini (Mahamoud Mgimwa), Mufindi Kusini (Mendrad Kigola), Kilolo (Venance Mwamoto) na Maswa Mashariki (Stanslaus Nyongo).
Maswa Magharibi (Mashimba Ndaki), Chilonwa (Joel Mwaka), Mtwara Vijijini (Hawa Ghasia), Nanyamba (Abdallah Chikota), Tunduru Kusini (Daimu Mpakate), Tunduru Kaskazini (Ramo Makani), Bunda Vijijini (Boniface Mgetere), Mkuranga (Abdallah Ulega) na Mbulu Vijijini (Gregory Massay) nayo yameenda CCM.
Mengine ni Mbulu Mjini (Zacharia Paul), Kilindi (Kigua Mohamed), Namtumbo (Edwin Ngonyani), Ushetu (Elias Kuandikwa), Bumbuli (January Makamba), Segerea (Bonnah Kaluwa), Kalambo (Josephat Kandege), Wanging’ombe (Gerson Lwenge), Kigoma Kaskazini (Peter Serukamba), Muhambwe (Justus Nditiye), Kasulu Vijijini (Agustie Vuma) na Kilolo (Venance Mwamoto).
WABUNGE WA CHADEMA
Kwa upande wa CHADEMA, hadi sasa kimejinyakulia majimbo 35 ambayo ni Kibamba (John Mnyika), Mikumi (Joseph Haule), Bukoba Mjini (Wilfred Lwakatare), Same Mashariki (Nagenjwa Kayoboka), Rombo (Joseph Selasini), Bunda Mjini (Ester Bulaya), Hai (Freeman Mbowe) na Mbeya Mjini (Joseph Mbilinyi).
Majimbo mengine ni Kawe (Halima James Mdee), Longido (Onesmo Nangole), Ukonga (Waitara Mwita), Mlimba (Suzan Kiwanga), Singida Mashariki (Tundu Lissu), Ubungo (Said Kubenea), Mbozi (Paschal Haonga), Tunduma (Frank Mwakajoka), Momba (David Silinde), Kilombero (Peter Lijualikali) na Karatu (Willy Qambalo).
Aidha, chama hicho kilishinda katika majimbo ya Simanjiro (James ole Millya), Arumeru Magharibi (Gipson ole Meseyeki), Tarime Mjini (Ester Matiko), Siha (Godwin Mollel), Buyungu (Kasuku Bilago), Monduli (Julius Kalanga), Arumeru Mashariki (Joshua Nassari), Serengeti (Marwa Ryoba) na Babati Mjini (Pauline Gekul).
Mengine ni Moshi Mjini (Jaffar Michael), Tarime Vijijini (John Heche), Iringa Mjini (Peter Msigwa), Ndanda (Cecil Mwambe) na Moshi Vijijini (Anthony Komu). CUF yenyewe hadi sasa kina majimbo 17 ambayo ni Temeke (Abdallah Mtolea), Mchinga (Hamidu Bobali), Kilwa Kusini (Said Bungala), Kaliua (Magdalena Sakaya), Tandahimba (Ahmad Katani), Mtwara Mjini (Maftaha Nachuma), Kinondoni (Maulid Mtulia), Kilwa Kaskazini (Vedasto Ngombale) na Tanga Mjini (Musa Mbaruk). Majimbo mengine ni Wawi, Chakechake, Ole, Ziwani, Kojani, Gando, Wete na Mgogono.
WABUNGE WENGINE KUPTIA CHADEMA, CUF, ACT WAZALENDO na NCCR MAGEUZI
Hai(Freeman Mbowe), Vunjo (James Mbatia) Kigoma Mjini (Zitto Kabwe), Arumeru Mashariki (Joshua Nassari), Kawe (Halima Mdee), Ukonga (Waitara Mwita), Kibamba (John Mnyika), Ubungo (Said Kubenea), Bunda Mjini (Ester Bulaya), Tunduma (Frank Mwakanjoka), Siha (Dk Godwin Mollel), Tarime Vijijini (Esther Matiko), Same Mashariki (Nagenjwa Kayoboka), Kaliua (Magdalena Sakaya), Mlimba (Suzan Kiwanga), Iringa Mjini (Peter Msigwa).
Chanzo: Habari Leo Online

Friday, October 30, 2015


 Msafara wa Bw Magufuli umelindwa vikali na maafisa wa usalama
11:30am: Msafara wa Rais mteule John Magufuli pamoja na ule wa Rais Jakaya Kikwete waelekea ikulu chini ya ulinzi mkali. 

Friday, October 23, 2015

 Albino
Visa vya albino kushambuliwa na kukatwa viungo huongezeka sana wakati wa uchaguzi
Mwanamume mwenye ulemavu wa ngozi anauguza majeraha baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana eneo la Mkuranga, Tanzania.
Shambulio hilo dhidi ya albino huyo limetokea siku chache tu kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika.
Kumekuwepo na wasiwasi kwamba huenda watu wenye ulemavu wakashambuliwa zaidi kwani baadhi ya watu wanaoamini katika ushirikina hudai viungo vyao vinaweza kumpa mtu bahati.
Wanaume watatu wanadaiwa kuingia kwa nguvu nyumbani kwa Mohammed Said, 35, katika mji huo ulio katika mwambao wa Pwani kilomita 42 kutoka mji mkuu wa kibiashara wa Dar es Salaam.
Walimkata kichwani kwa upanga wakati wa shambulio hilo Jumatano usiku.
Polisi wamesema wanawasaka watu hao.

Saturday, October 17, 2015

 Aliyekuwa Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe enzi za Uhai wake.
 Msaidizi wa Mbunge huyo, Casablanga Haule enzi za Uhai wake.
 Padri Plasdus Ngabuma enzi za Uhai wake.
 Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Ludewa, Deogratias Filikunjombe wakati wa ibada ya kuuaga iliyofanyika nyumbani kwake Kijichi Dar es Salaam leo mchana.



Mke wa marehemu Deogratias Filikunjombe, Sarah Filikunjombe (kushoto) akilia kwa uchungu baada ya kupata tarifa za kifo cha mumewe.filikunjombeNdugu, jamaa na marafiki wakionekana wenye huzuni nyumbani kwa Deogratias Filikunjombe.filikunjombe (3)Nyumbani kwa Deogratias Filikunjombe Mbagala Kijichi, Dar es Salaam.silaaCapt. William Silaa enzi za uhai wake.chopaFilikunjombe akiwaaga wananchi wake.
Mbunge wa Ludewa Mhe. Deogratias Haule Filikunjombe amefariki dunia katia ajali ya Chopa katika hifadhi ya wanyama ya Selous, pamoja na rubani Kepteni William Silaa mfanyakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa.
Wengine waliofariki kwenye ajali hiyo ni Vitalis Blanka haule na Ofisa Tawala wa Wilaya ya Tarime, Bw. Egdi Mkwera ambaye alikuwa mtaalam wa mifugo.
Picha hapo chini ni Chopa iliyosababsha kifo cha Filikunjombe, Capt. William Silaa na watu wengine wawili.  chopa 2

Thursday, October 8, 2015

http://ichef.bbci.co.uk/news/ws/660/amz/worldservice/live/assets/images/2015/10/08/151008115839_bard_prison_initiative_512x288_bardprisoninitiative.jpg

Kundi la wafungwa kutoka New York limeshinda mdahalo dhidi ya kundi kutoka Chuo Kikuu cha Harvard, chuo kilichoorodheshwa bora zaidi duniani.
Wafungwa hao kutoka Eastern New York Correctional Facility walikuwa wamewaalika wanafunzi hao kutoka Harvard kwa shindano la mjadala gerezani.
Kwenye mdahalo huo, wafungwa walitetea msimamo kwamba watoto wa wazazi walioingia Marekani kinyume cha sheria wanafaa kukataliwa shuleni.
Mdahalo huo uliamuliwa na jopo lisiloegemea upande wowote.
Muda mfupi baada ya kushindwa, wanafunzi hao wa Harvard walijitetea kwenye ukurasa wa timu yao kwenye Facebook.


Mchoraji wa miundo ya magari nchini India Sudhakr Yadav amejaribu kuweka rekodi ya pili ya Guiness kwa kutengeneza gari analotumai litakuwa ndilo kubwa zaidi duniani.
Gari hilo, ambalo limeundwa likifanana na gari aina ya Ford Toure lililoundwa mwaka 1922, lina urefu wa futi 26 (mita 8) kwenda juu na ukubwa wa futi 50 lina ukubwa maradufu wa basi lililo na ghorofa mbili mjini London.

Sunday, October 4, 2015


Mwanasiasa mkongwe na Mwenyekiti wa chama cha kisiasa cha  DP Christopher Mtikilaamefariki dunia alfajiri ya leo wakati akitokea Morogoro kuelekea Dar es salaam.

Tuesday, September 29, 2015


Kanisa KageraHaijabainika ni nani anayeteketeza makanisa hayo
Makanisa manne yameteketezwa katika mkoa wa Kagera, kaskazini magharibi mwa Tanzania na kufikisha saba, idadi ya makanisa yaliyochomwa moto eneo hilo mwezi huu.
Hadi sasa haijabainika ni kundi gani linalohusika na vitendo hivyo, kwa mujibu wa polisi.
Lakini baadhi ya viongozi wa dini wameambia mwandishi wa BBC Leonard Mubali kuwa huenda ni matokeo ya uhasama wa kidini.
Kuchomwa kwa makanisa hayo kumeongeza hofu kwa viongozi wa makanisa na waumini kuhusu usalama wao.

Sunday, September 27, 2015

Naibu spika wa bunge Job Dungai, yeye ndiye kashikilia rungu, Ripoti " ijadiliwe au la"Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya bunge ya hesabu za serikali, (PAC), Zitto Kabwe. Taarifa ya CAG kuhusu akaunti nya Tegeta Escrow, iko mikononi mwake

Saturday, September 26, 2015

 
 Mpagi Edward Edmary
Mnamo mwaka 1982 Mpagi Edward Edmary ,dereva wa texi nchini Uganda alipewa hukumu ya kifo kwa mauaji ya kinyama ya jirani yake.
Licha ya Edward kuwa mtu asiye na hatia hakuhukumiwa na mauaji yoyote.
Edward alisingiziwa katika mgogoro wa shamba wa familia.

Saturday, September 19, 2015

 
Rais Barack Obama amemteua Eric Fanning kuwa katibu mpya katika jeshi la Marekani. 
Rais wa Marekani Barack Obama amemteua Eric Fanning kuwa katibu mpya katika jeshi la Marekani.

Friday, September 11, 2015

hii ndio shule ya Sekondari Masimbwe aiko wilayani Ludewa kata mpya ya Lubonde
 Mkuu wa shule ya Masimbwe Mwalimu Eliud Sanga

Tuesday, September 8, 2015


Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini, Monica Laurent (kushoto), akizungumza na wanahabari wakati akimkaribisha msemaji wa mkutano huo kuzungumza na waandishi.
Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa nchini, Sisty Nyahoza (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi, kuhusu vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu ambavyo ninastahili kushiriki uchaguzi mkuu. Kulia ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Emmanuel Kayuni.

Wednesday, September 2, 2015

 
Mwanamke mmoja aliyekuwa akitumia choo cha muda, alibebwa na kupelekwa sehemu nyingine wakati choo hicho kilipoinuliwa juu na tracta kimakosa na kuhamishwa hadi eneo lingine.
Mwanamke huyo alikuwa ameenda kutumia choo hicho kabla ya ufunguzi wa tamasha la Newlyn Fish Festival, Cornwall nchini Uingereza.

Saturday, August 29, 2015

 Mgombea wa Urais kwa kupitia Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wakazi wa
 kijiji cha Kikondo kata ya Ilungu Mbeya vijijini akiwa njiani kuelekea mkoa wa Njombe .

Friday, August 28, 2015

 
Wanajeshi wa waasi CAR
Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya watoto UNICEF, limesema kuwa makundi yaliyojihami nchini Jamuhuri ya Afrika ya Kati, yamewaachilia watoto mia moja sitini na watatu.
Watoto hao waliachiliwa mjini Batangafo, baada ya majadiliano kati ya shirika hilo na makundi hayo ya waasi mwezi Mei mwaka huu, kama sehemu ya mpango wa amani.
 
Treni
Afisa mmoja wa serikali ya Poland, amesema kuwa ana imani kuwa treni moja ya kijeshi ambayo imefichwa tangu vita vya pili vya dunia, zaidi ya miaka sababini iliyopita, na kusemekana kubeba vitu vya z

Mtu yeyote anapoingia katika maisha huwa anakabiliwa na changamoto ya kuamua kati ya kujiajiri au kuajiriwa. Kuajiriwa kunakuhakikishia usalama kazini japokuwa usalama huo siku hizi ni nadra sana kuwepo, wakati kujiajiri hukuhakimkishia uhuru wa kuamua mambo yako. Watu wengi huamua kuchagua kuajiriwa kwa sababu ni rahisi kuliko kuwa wajasiriamali ambako ni kugumu, tatizo wanalolipata ni kuwa wanaishi kwa kutegemea mshahara ambao huwa hautoshi na kujiingiza kwenye madeni mabaya ambapo hukopa kwa ajili ya matumizi na kuendelea kuwa na madeni makubwa zaidi. Kukopa siyo kubaya ila kuna madeni mabaya na madeni mazuri madeni mabaya ni yale ambayo mtu anakopa kwa ajili ya hela ya kula au kutumia, madeni mazuri ni yale ambayo mtu anakopa kwa ajili ya kuwekeza kwenye vitegauchumi au kwenye biashara kwa kufanya hivyo mtu anaweza kujitoa kwenye matatizo.

Thursday, August 27, 2015


Junaid Hussain
Marekani imesema mpiganaji wa Kiingereza, ambaye alijiunga na kundi la Islamic State ameuawa katika shambulio la anga nchini Syria.
Junaid Hussain ambaye alikuwa akiendesha kampeni za kundi hilo la Islamic State kupitia mitandao ya kijamii na kufanya kazi kubwa kuwavuta na kuwaingiza katika kundi hilo, raia wa kigeni.

Wednesday, August 26, 2015

Akihutubia mamia ya watu waliojaa leo huko sumbawanga

Tuesday, August 18, 2015


Mfanyabiashara tajiri kijana Mohamed Dewji
Mfanyabiashara maarufu nchini na Mbunge wa Singida Mjini (CCM), Mohammed Dewji (pichani) kwa mara ya kwanza ameingia kwenye orodha ya mabilionea 29, akiwa tajiri kijana kuliko wote barani Afrika.
Jarida la Forbes la Marekani limemtaja Dewji (39), katika nafasi ya 24 ya matajiri wa Afrika akiwa na utajiri wa Dola 1.3 bilioni za Marekani (Sh2.34 trilioni) unaotokana na biashara mbalimbali anazozifanya kupitia kampuni yake ya Mohammed Enterprises (Metl Group).“Dewji alibadilisha biashara aliyoanzisha baba yake kutoka uuzaji bidhaa na kuwa na viwanda vya Metl,” inasema sehemu ya habari inayomuhusu bilionea huyo Mtanzania .
 
Shambulizi la Thailand lalaaniwa
Waziri mkuu wa Thailand ametaja shambulizi la bomu ambalo limewauwa zaidi ya watu ishirini mjini Bangkok hapo jana jumatatu kuwa kisa kibaya zaidi kuwahi kutokea nchini humo.

Thursday, August 6, 2015





Imesubiriwa kwa shauku iliyoje, mengi yamesemwa lakini imefikia hatua ya mitandao mingi kufanya tukio hili kuwa habari iliyofika kwenye madawati yao hivi punde.
Kwa post hii ya Diamond kwenye ukurasa wake wa Twitter na Instagram dakika chache zilizopita ni dhahiri kuwa familia ya Wasafi imepata ongezeko la mtoto wa kike.

Wednesday, August 5, 2015

 
Je unamfahamu Edward Lowassa ni nani katika siasa za Tanzania ?
Umoja usio rasmi wa vyama vinne vya upinzani nchini Tanzania unajulikana kwa jina la Katiba ya Wananchi (UKAWA), baada ya kusubiri kwa muda hatimaye umemtangaza Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa kuwa mgombea wake wa urais.
Lowassa anagombea kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), huku vyama vingine vitatu vikimuunga mkono. Hii inatokana na sheria za Tanzania ambayo haitambui umoja wa vyama.
Kabla ya kujiengua chama Tawala chama cha Mapinduzi CCM, Edward Lowassa amekuwa mwanachama wa CCM kwa muda wa miaka 38, ambapo alijiunga na chama hicho mara tu baada ya kumaliza elimu yake ya chuo kikuu mwaka 1977.

Tuesday, August 4, 2015

 NUH & SHISHI
Kuna sauti ambayo imerekodiwa na kinachosikika ni sauti ya mwanamke na mwanaume wakijibizana, waliotajwa kwamba ndio wanaosikika kwenye sauti hiyo ni Nuh Mziwanda na Wema Sepetu, imemfikia Soudy Brown tayari !!
Soudy Brown anasema sauti hiyo ilirekodiwa usiku mmoja kabla ya Tuzo za KTMA, na baada ya ishu kuwafikia wote wawili yani Nuh na mpenzi wake Shilole haijulikani nini kinaendelea kati yao kwa sasa.
Sauti yote iko hapa mtu wangu, ukiplay utawasikia wote ilivyokuwa kwenye U Heard August 03 2015

Monday, July 27, 2015


 
Bobbi Kristina afariki Dunia
Bobbi Kristina Brown ,mtoto wa marehemu Whitney Houston ambaye alikuwa gwiji wa muziki wa R&B ,amefariki dunia baada ya kupoteza fahamu kwa muda wa miezi sita tangu alipokutwa taabani kwenye bafu lake na pindi alipofikishwa hospitalini na kukutwa na matatizo kwenye ubongo.
Bobbi amekufa akiwa na umri wa miaka 22,huku akivutiwa kuwa muigizaji na muimbaji mahiri na mwenye ubora wa aina yake.