Wednesday, February 10, 2016

 
Marehemu Idi Amin Dada aliiongoza Uganda kwa miaka minane kati ya mwaka wa 1971 hadi 1979
Mgombea wa urais katika uchaguzi mkuu ujao nchini Uganda ameahidi kurejesha nyumbani mabaki ya aliyekuwa rais wa nchini hiyo Idi Amin Dada na kuujengea makavazi.
Aliyekuwa waziri mkuu wa Uganda Amama Mbabazi,alisema endapo atachaguliwa kuwa rais azimio lake la kwanza itakuwa kuwapatanisha waganda wa kila tabaka na kabila.
Kwa madhumuni hayo anapanga kuwaleta pamoja watu anaohisi kuwa wanaomuunga mkono Idi Amin wale waliomuunga mkono Milton Obote na wale wanaomuunga mkono rasi wa sasa Yoweri Kaguta Museveni.
Viongozi hao watatu ndio waliochangia kwa njia moja au nyengine mwelekeo wa kisiasa wa Uganda.

Amama Mbabazi ameahidi kurejesha nyumbani mabaki ya aliyekuwa rais wa nchini hiyo Idi Amin Dada na kuujengea makavazi.
Marehemu Idi Amin Dada aliiongoza Uganda kwa miaka minane kati ya mwaka wa 1971 hadi 1979 utawala ambao ulishuhudia mauaji ya wapinzani wake wengi.
Vilevile anatuhumiwa kwa kuwatimua wahindi wote nchini Uganda kabla ya kupinduliwa na Milton Obote.
Marehemu Idi Amin aliaga dunia akiwa uhamishoni nchini Saudi Arabia.
Rais Yoweri Museveni, anatarajiwa kuchaguliwa tena kuongoza taifa hilo la Afrika Mashariki kwa hatamu ya tano.

Chifu Mandla Mandela taabani kwa kuukubali Uislamu 
Hatua ya mjukuu wa kiongozi mwanzilishi wa Afrika Kusini Nelson Mandela , Mandla, 42, kuslimu na kuoa mke wa nne imevutia hisia kali kutoka kwa viongozi wa kabila lake la AbaThembu.
Wazee hao viongozi wenza wa kabila la Mvezo iliyokuwa ya marehemu ya Mandela ''hawaamini kuwa Chifu mzima wa kabila la Mvezo anaweza kuasi tamaduni zake na kuiga zile za mke wake ''
Mandla alifunga ndoa yake ya nne na bi Rabia Clarke katika msikiti mmoja mjini Cape Town Afrika Kusini mwishoni mwa juma.

Rais Magufuli 

Serikali ya Tanzania imebaini wizi wa takribani shilingi milioni 700 sawa na dola laki tatu za marekani ($320,000 )katika shirika lake la Ndege (ATCL) kupitia kampuni ya wakala wa ukatishaji tiketi ya Salama World Travel iliyopo visiwa vya Comoro.