MWANAMKE 
mmoja aliyetambuliwa kwa jina la Doreen John Mlemba, mwenyeji wa Same 
mkoani Kilimanjaro, mwishoni mwa mwaka uliopita alikamatwa kwa 
kuhusishwa na shehena ya madawa ya kulevya aina ya Heroin, yenye thamani
 ya shilingi bilioni 2.5.
Madawa 
hayo yalikutwa kwenye nyumba moja iliyopo eneo la
Ununio, Tegeta jijini Dar es Salaam, ambayo ni mali ya Mbunge wa CCM (Jina linahifadhiwa) wa jimbo moja la mikoa ya Kanda ya Ziwa, Uwazi limefukunyua.
Ununio, Tegeta jijini Dar es Salaam, ambayo ni mali ya Mbunge wa CCM (Jina linahifadhiwa) wa jimbo moja la mikoa ya Kanda ya Ziwa, Uwazi limefukunyua.
Taarifa 
toka vyanzo mbalimbali makini, zinasema majirani wa nyumba hiyo walikuwa
 na mashaka na kinachofanyika ndani ya nyumba hiyo, kwani licha ya 
ukubwa na kukamilika kwa ujenzi wake, lakini haikuwa ikikaliwa na mtu na
 mara chache, watu walionekana wakiingia na kutoka bila kujulikana 
walichokuwa wakikifanya.
Kutokana 
na hali hiyo ya wasiwasi, wasamaria wema walitoa taarifa kwa Jeshi la 
Polisi ambalo liliifanyia kazi habari hiyo na kufika kwenye nyumba hiyo 
na kujaribu kugonga lakini bila mafanikio yoyote.
“Baada ya
 kugonga, ndipo polisi hao walipoamua kuvunja mlango na kufanya upekuzi 
katika sehemu zote ndani ya nyumba hiyo, ambapo walifanikiwa kulikuta 
sanduku ambalo baada ya kufunguliwa, zikagundulika kilo 35 za madawa ya 
kulevya aina ya Heroin,” kilisema chanzo chetu kilichoshuhudia zoezi 
hilo.
Kamanda 
wa Kikosi Cha Kupambana na Kudhibiti Madawa ya Kulevya nchini, SACP 
Godfrey Nzowa alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa 
baada ya kukamata shehena hiyo, vijana wake walijikuta katika wakati 
mgumu wa kumjua mmiliki wa nyumba hiyo.
Baada ya 
kutafuta nyaraka mbalimbali, hatimaye waligundua kuwa nyumba hiyo 
inamilikiwa na mbunge huyo wa zamani ambaye alitafutwa na kuhojiwa kwa 
saa kadhaa, ambapo alikiri kuimiliki, lakini akidai kwa muda huo, 
alikuwa ameipangisha kwa watu aliowataja, bila kujua shughuli iliyokuwa 
ikifanyika ndani yake.
Inadaiwa 
kuwa baada ya kupata ushirikiano huo kutoka kwa mbunge huyo, askari 
waliingia mtaani kuwasaka wapangaji hao, ambapo Septemba 15, mwaka jana,
 saa saba mchana, walifanikiwa kumkamata Doreen, akiwa shambani kwake, 
eneo la Ruaha Mbuyuni mkoani Iringa alikokuwa akivuna vitunguu, bamia na
 bilinganya.
“Tulifanya
 uchunguzi na tayari watu watano wameshakamatwa akiwemo Doreen, nyumba 
hiyo waliifanya kama ghala la kuhifadhia madawa na mtu mmoja bado 
tunaendelea kumsaka, baadhi ya waliokamatwa tulikuwa tukiwasaka kwa muda
 mrefu,” alisema Kamanda Nzowa.
Aliwashukuru
 wananchi kwa ushirikiano wao na kuwaomba waendelee hivyo na kwamba 
donge nono litatolewa kwa watakaofanya hivyo huku majina yao 
yakihifadhiwa.Gazeti hili lilimfikia Mbunge huyo mmiliki wa nyumba kwa 
njia ya simu, lakini alikataa kulizungumzia suala hilo, akidai liko 
chini ya polisi.
“Naomba 
suala hili umuulize Kamanda Nzowa, mimi siwezi kulizungumzia kwa vile 
lipo chini ya uchunguzi wao, pamoja na kwamba nawatambua hao wapangaji 
lakini siwezi kusema lolote,” alisema.
 RSS Feed
 Twitter

9:13 AM
MZM

0 comments:
Post a Comment