Je unamfahamu Edward Lowassa  ni nani katika siasa za Tanzania ? 
                    
                
Umoja
 usio rasmi wa vyama vinne vya upinzani nchini Tanzania unajulikana kwa 
jina la Katiba ya Wananchi (UKAWA), baada ya kusubiri kwa muda hatimaye 
umemtangaza Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa kuwa mgombea wake wa 
urais.
Lowassa anagombea kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo
 (Chadema), huku vyama vingine vitatu vikimuunga mkono. Hii inatokana na
 sheria za Tanzania ambayo haitambui umoja wa vyama.
Kabla ya 
kujiengua chama Tawala chama cha Mapinduzi CCM, Edward Lowassa amekuwa 
mwanachama wa CCM kwa muda wa miaka 38, ambapo alijiunga na chama hicho 
mara tu baada ya kumaliza elimu yake ya chuo kikuu mwaka 1977.