Friday, June 17, 2016


Rapper Chidi Benz amefanikiwa kuirudisha afya yake baada ya kuachana na matumizi ya Madawa ya kulevya.

Mapema mwaka huu katika kituo kimoja cha runinga Chidi Benz alikiri kutumia Madawa ya kulevya na kuomba msaada ambapo meneja Diamond na Tip Top Connection, Babu Tale akishirikiana na Kalapina walimsaidia na kumpeleka katika kituo cha Bagamoyo Sober House ambacho kilimsaidia kuachana na Matumizi ya madawa ya kulevya.

Jumatano hii katika mitandao ya kijamii kumesambaa picha mpya za rapper huyo zikimuonyesha jinsi alivyopendeza hali ambayo imewafanya mashabiki kumpongeza Tabu Tale.

Chid Benzi akiwa  na Babu Tale
 


0 comments: