BAADA YA KUTUA BONGO DIAMOND ASEMA HAYa KUMHUSU ALI KIBA
Baada
 ya Diamond Platnumz kutua jijini Dar es salaam December 2 akitokea 
Afrika Kusini akiwa na tuzo zake 3 za Channel O, alikutana na wadau, 
mashabiki pamoja na 
waandishi pale Escape 1 kuzungumzia ushindi wake na safari nzima ilivyokuwa.
waandishi pale Escape 1 kuzungumzia ushindi wake na safari nzima ilivyokuwa.
Miongoni
 mwa maeneo aliyozungumzia ni pamoja na umoja unaohitajika kwa wasanii 
wa Tanzania ili waweze kuwa wengi katika majukwaa ya kimataifa.
“Ombi langu mimi kiukweli ni moja tu, Unajua lazima kama alivyosema 
mheshimiwa hapa muziki wetu ushakuwa, watu wanaukubali na tushaona njia 
kama tunaweza so lazima sisi tujiamini wenyewe tusikaekae sana nyuma 
kwasababu watu kuna ile kuogopa cha kuona kama aah watanipokea kweli. Na
 zile za aah ntashindwa kuongea kizungu ntachekwa mi nishachekwa sana 
kwenye kizungu sana, lakini saizi naweza nikaingia hata Big Brother na 
broken zangu hivyo hivyo lakini napita hivyo hivyo nimeingia pale juzi 
Fally hajaongea mi nimeongea “.
Diamond pia ameendelea kuwaomba wasanii wenzake kutotengenezeana beef za
 wenyewe kwa wenyewe, na hakusita kumtaja Ally Kiba wakati akitoa mifano
 alipokuwa Nigeria na kujiona yuko peke yake hakuna msanii yeyote wa 
nyumbani zaidi yake.
“Kingine mimi nilikuwa nataka niombe tufute zile zama zakutengenezeana 
matatizo wasanii wenyewe kwa wenyewe wa Tanzania kwasababu haiwezi 
kutusaidia kabisa, alikuwa anaongea kitu mkubwa hapa, nilivyofika 
Nigeria nilikuwa najiona kama mkiwa kwasababu niko peke yangu, 
nikiangalia huku simuoni hata Jaguar, huku siwaoni wasanii wenzangu 
namtafuta Dimpoz namtafuta nani, hata Ally simuoni yaani niko peke 
yangu.
 RSS Feed
 Twitter

11:32 AM
MZM

0 comments:
Post a Comment