Katika 
hali isiyokuwa ya kawaida mwanamke mmoja aliyejulikana kwa jina la Li 
Zhenghua 24, amekutwa akifanya jaribio la kumla Mtoto wake aliyejifungua
 siku chache zilizopita, baada ya kumkuta taya yake ikiwa imenasa 
kuzunguka Mkono wa Mtoto wake. 
Tukio hilo la ajabu lilitokea katika Hospitali iliyoko Shenzhen 
Kusini mwa jimbo la Guangdong, China ambapo mwanamke huyo alifikishwa 
kujifungua na baadaye wahudumu wa Hospitali kufanya jitihada za kutafuta
 ndugu zake. 
Hata hivyo mwanamke huyo akiwa na siku ya tatu Hospitalini hapo 
alikutwa na nesi akiwa katika jaribio la kumng’ata mtoto ambapo 
madaktari walitumia nguvu na kufanikiwa kumuokoa mtoto huyo ambaye 
tayari alikuwa na jeraha mkononi.
 RSS Feed
 Twitter

7:33 AM
MZM


0 comments:
Post a Comment