Askari wakiwataka wananchi kutawanyika baada ya kuahirishwa uchaguzi wa 
Serikali za mitaa katika kituo cha Mabibo Mpakani Mtaa wa Jitegemee, Dar
 es Salaam jana. Picha na Salim Shao 
            
Kwa ufupi
Mzindakaya alisema wagombea wa Chadema Kijiji cha 
Lamadi walienguliwa kutokana na kutokidhi vigezo baada ya kuwekewa 
pingamizi, huku wakisalia wa CCM pekee.
Mikoani. Mgombea uenyekiti kupitia CCM Mtaa wa 
Swea, Kata ya Mkolani, Nyamagana, Mwanza, Pius Mihayo amefariki dunia 
ghafla akiwa mtaani kwake, muda mfupi baada ya kupiga kura.
Msimamizi wa uchaguzi huo, Halifa Hida alisema 
mgombea huyo alifariki dunia ghafla akiwa kwenye mtaa wake wa Swea na 
chanzo cha kifo hicho hakijajulikana... “Sasa kwa mujibu wa taratibu za 
uchaguzi, tutatangaza matokeo ya wajumbe na nafasi za wagombea wa viti 
maalumu, nafasi ya uenyekiti haitatangazwa hadi taratibu nyingine za 
uchaguzi zitakapoandaliwa,” alisema Hida.
Mkoani Arusha msongamano wa kupiga kura, katika 
kituo cha Mbauda, Kata ya Sombetini unadaiwa kusababisha kifo cha mtu 
aliyetambulika kwa jina la Suleiman Bakari.
Tukio hilo lilitokea saa tatu asubuhi katika kituo
 hicho ambacho kilikuwa kimefurika watu. Mjomba wa marehemu, Ramadhani 
Athumani alisema kifo hicho kimewashtua kwani marehemu hakuwa mgonjwa.
“Marehemu alikuwa ni kinyozi na baada ya kupiga 
kura alianguka ghafla,” alisema Athumani na kuongeza kuwa mazishi 
yatafanyika leo saa saba.
Wagoma kupitishwa bila kupingwa
Vituko vya uchaguzi vimeendelea katika mikoa ya 
Kanda ya Ziwa ambako pamoja na mambo mengine, baadhi ya wagombea wa CCM 
waliopita bila kupingwa wameamua kujitoa baada ya kutishiwa maisha.
Tukio la wagombea kutishiwa maisha lilitokea 
wilayani Busega, Mkoa wa Simiyu ambako uchaguzi huo ulikumbwa na vurugu 
mbalimbali. Taarifa zilizotolewa na Mkuu wa wilaya hiyo, Paul Mzindakaya
 zinasema wagombea kupitia CCM katika Mji wa Lamadi, walijiondoa dakika 
za mwisho.
Hatua hiyo inadaiwa imetokana na wagombea hao 
kutishiwa maisha, kuchomewa moto nyumba zao na kwamba kutoka kwa wafuasi
 wa chama kimoja cha siasa.
Mzindakaya alisema wagombea wa Chadema Kijiji cha 
Lamadi walienguliwa kutokana na kutokidhi vigezo baada ya kuwekewa 
pingamizi, huku wakisalia wa CCM pekee.
“Mpaka sasa saa sita mchana, tumeamua kusitisha 
upigaji kura masanduku yote tumeyaondoa, hali si shwari eneo hilo, 
askari wamepelekwa kurejesha usalama na kamati ya ulinzi na usalama 
wilaya itakaa muda huu kujadili hali hii, ili tukubaliane kama tuendelee
 au tusitishe,” alisema Mzindakaya.
 RSS Feed
 Twitter

10:48 AM
MZM

0 comments:
Post a Comment