Indonesia imewauwa wasafirishaji nane wa madawa ya kulevya siku ya
Jumatano, wakiwemo raia saba wa kigeni, hatua iliyolaaniwa vika nya
Australia na Brazil, zilizojaribu kuwaokoa raia wake bila mafanikio.
Indonesia imetete hatua yake hiyo ikiitaja kuwa ni muhimu katika
mapambano dhidi ya madawa ya kulevya, na kusema haina wasiwasi kuhusiana
na hatua zilizochukuliwa na Australia...
Wednesday, April 29, 2015


Maelfu ya maafisa wa polisi nchini Marekani wameamriwa kuwasaidia
maafisa waliozingirwa mjini Baltimore, baada ya ghasia zilizosababishwa
na waandamanaji waliojawa na hasira, kufuatia kifo cha Mmarekani mweusi.
Muandamanaji akiwafokea polisi waliokuwa wanajaribu kudhibiti hali mjini Baltimore
Watu 27 wametiwa nguvuni huku polisi 15 wakijeruhiwa wakati waandamanaji
hao wengi wao wanafunzi...


Chama tawala nchini Afrika Kusini African National Congress ANC
kimelaani wimbi la mashambulizi dhidi ya raia wa kigeni ambayo
yamesababisha vifo vya watu sita na kusababisha hali ya wasiwasi nchini
humo
Taarifa kutoka kwa chama cha ANC imesema katika kipindi cha majuma
kadhaa sasa, taifa la Afrika Kusini limeghubikwa na wimbi la
mashambulizi ya kufedhehesha yanayowalenga raia wa...


Mapambano dhidi ya mauaji ya albino
Juhudi za kukabiliana na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi nchini
Tanzania zinapata nguvu mpya kupitia kampeni mbalimbali zinazolenga
kuhamasisha jamii kupinga vitendo hivyo vya kinyama.
Watoto wenye ulemavu wa ngozi katika shule ya msingi ya Mitindo.
Pamoja na kampeni kadhaa zilizoanzishwa, siku ya Jumapili (tarehe 15
Machi) kulitarajiwa...
Tuesday, April 21, 2015



Serikali
imerejesha mafunzo ya madereva kila baada ya miaka mitatu wakati wa
kumalizika kwa muda wa leseni zao, huku ikifafanua kuwa elimu
watakayoipata ina umuhimu katika kazi zao, kutokana na mabadiliko
mbalimbali yanayotokea katika sekta hiyo.
Naibu
Waziri wa Kazi na Ajira, Makongoro Mahanga, alitangaza uamuzi huo wa
Serikali jana katika mkutano kati...
Subscribe to:
Posts (Atom)