Kialama cha WhatsApp
WhatsApp
 imepitia mabadiliko mengi, na imekuwa kati ya applications zinazotumika
 na kupendwa zaidi duniani. Baada ya kununuliwa na Facebook, 
waendelezaji walianza kuongeza vitu vipya kama kupiga simu za sauti, 
kuweza kutuma mafaili, na kuongezwa kwa usalama zaidi. Kwasasa, WhatsApp
 ni moja kati ya application yenye watumiaji wengi zaidi, ikiwa na 
angalau watumiaji bilioni moja wanaotumia kikamilifu kila mwezi. Katika 
makala hii, tutafahamisha baadhi ya vitu vilivyopo WhatsApp na 
havitumiki mara nyingi, na namna vinavyoweza kutumika;
1. Kuweka maandishi yaliyokolea (bold), kiitaliano (italics) na kuyakata maandishi.
Unataka
 kutuma ujumbe ambao una muonekano maalumu? Kwa kuweka alama ya nyota 
mwanzo na mwisho wa neno, basi utakuwa umelifanya neno kukolea (bold). Kuyalaza maandishi (italics) weka alama ya underscore (_) mwanzo na mwishoni mwa neno, na ukitaka kulikata neno katikati weka alama ya tilde(~) mwanzo na mwisho.
2. Kuzima taarifa za wanaochati kwenye kundi (mute)
Kama
 una marafiki wanaopenda kuchati sana na hutaki kuwaudhi kwa kutoka 
kwenye kundi, basi unaweza ukazima taarifa kwa saa nane, siku saba au 
mwaka mzima. Wewe bonyeza kwenye taarifa za kundi halafu bonyeza mute na
 chagua muda unaotaka kutopata taarifa wanapochati. Utakuwa umewaweza
3. Kutuma ujumbe kwa namba nyingi kwa pamoja
Pengine
 una taarifa ambayo ungependa kutuma kwa watu wengi kwa pamoja, labda ni
 biashara na ungependa kila mtu imfikie inbox kwake. Sini hii inaitwa 
Broadcast List na inapatikana juu kabisa upande wa kulia kwenye skrini 
yako ya kuchati. Bonyeza Chats -> Broadcast Lists -> New List -> Add contacts, Andika meseji yako na bofya send
4. Kuweka shortcut  ya chati yako na mtu kwenye kioo cha simu yako
Labda
 una bae na unapenda ukibonyeza mara moja tu kwenye kioo muanze kuchati 
bila kuhangaika kuanza kutafuta jina lake lilipo. Fanya hivi, bonyeza 
namba yake na kuishikilia kwa muda kwenye chati zenu WhatsApp, kisha 
chagua Add Conversation Shortcut. Sini hii inafanya kazi kwenye simu za Android pekee
5. Kujibu ujumbe bila kufungua application yako
Shortcut
 hii inapatikana kwenye simu za Android pekee kwa sasa, na inakuwezesha 
kujibu meseji ya mtu aliyetuma bila kulazimika kufungua application 
yako. Unachotakiwa kufanya ni kwenda kwenye Settings -> Notifications -> chagua Always show popup. 
6. Zuia mafaili ya Picha, Sauti na Video zisijipakue
Inawezekana
 haupendezwi na namna ambavyo Video, sauti na picha hujidownloadi moja 
kwa moja na kujaza memori yako. Kama hutaki kujaza memori yako, unaweza 
kuzuia kwa kwenda  kwenye  Settings -> Data Usage -> Media auto-download na utaona sehemu ya kuzima mafaili yasijipakue.
Je ulifahamu mbinu hizi? Tafadhali tujulishe kwa kukomenti kwa akaunti yako ya Google hapa chini
 RSS Feed
 Twitter

9:21 AM
MZM

 Posted in 
0 comments:
Post a Comment