Mwigizaji Jackline Wolper jana 
amefanya mahojiano na Zamaradi Mketema kwenye kipindi cha TakeOne na 
kuzungumzia mambo mengi kuhusu yeye na aliyekuwa mpenzi wake Putin 
‘Mkongo’ aliyemvisha pete, na uhusiano wake na msanii Harmonize.
‘Ni kweli Raj (Harmonize)ni 
mpenzi wangu,ukweli nilimjua siku nyingi nilikuwa nikimchukulia kama 
mwanamuziki tu, tuna mwezi mmoja na wiki mbili sasa’’ alisema Jack.
(Picha kwa msaada wa mtandao)
‘’Nisingependa
 kumuongelea mwanaume niliyekuwa naye ‘Putin’, nikiona picha 
zake,nikisikia jina lake yaani kuna vitu nikiviona kuhusu yeye naumia 
sana , na mimi nikimpenda mwanaume nampenda kutoka moyoni, nilijuana 
naye mwaka 2012 nilikuwa namzungusha kwasababu watu walikuwa wakiniambia
 kabila lao ni waongo, sasa kipindi alivyorudi hapa nchini alinikuta 
nipo singo, nilikuwa sipo sawa’’
‘’Katika maisha yangu sijawahi 
kumpeleka mwanaume kwa wazazi wangu nilimuamini nikampeleka kwetu na 
unajua mwanaume yeyote unayempeleka kwenu hutokubali kuachana naye 
kwasababu utakuwa unawaangusha wazazi wako na familia yako na ikiwa 
wamempokea vizuri lakini kwanini nimekubali kumuacha’’(analia)
‘’Ni kweli alikuwa mume wa mtu, 
baadhi ya watu walikuwa wakiniambia na kunitumia picha siku ambayo 
alinivisha pete, n asiku ambayo alinivisha pete nilikuwa sijui ilikuwa 
ni sehemu ambayo tulikuwa tunapenda kukaa na kunywa kila siku ananivisha
 pete nikakubali baada ya kunivalisha watu wakawa wananiambia kwanini 
nimevishwa pete na mume wa mtu sikutaka kumuamini mtu kwa sababu 
mahusiano yangu mengi yamekuwa yakiharibika kwa sababu kuwasikiliza 
watu, niliziona picha za harusi lakini nilihisi ni harusi tu, sikuelewa 
kwa sababu nilikuwa kwenye mapenzi’’
‘’Putin alikuwa akinidanganya 
kuhusiana na mke wake na niliamini ndoa nyingi watu wanaoana na kuachana
 na aliniambia ni kweli alikua na mwanamke lakini waliachana, lakini 
mwanamke aliyekuwa naye ni tofauti na watu walivyokuwa wakiambia yeye 
aliniambia kuwa hawajaoana na mwanamke huyo ila walitaka kufunga ndoa, 
kiukweli ni mtu ambaye anaweza sana kujielezea alinidanganya sana, 
nilimuamini sana kuliko wale watu zaidi ya kumi waliokuwa wakinieleza 
ukweli kuhusu yeye sikuwaamini, na wale waliokuwa wananiambia ukweli 
hawakuwa wabaya lakini sikuwaelewa kwa sababu nilikuwa kwenye mapenzi 
tayari’’ (analia).
‘’Nilitoka naye hapa tukaenda 
South Afrika(analia) tulienda kwa ajili ya kusoma nakumbuka ilikuwa 
mwezi wa 12 mwaka jana akaniambia ameshalipa kila kitu na ameninulia 
gari ya kuendea shule,nikakaa miezi mitatu sikusoma lakini wazazi wangu 
walikuwa wanajua nasoma ilikuwa ni lazima nimsitiri mchumba wangu kwa 
wazazi wangu nikawadanganya kuwa nasoma, mama yangu alikuwa anampenda 
sana mchumba wangu lakini baba yangu hakukubaliana na naye, alikuwa 
akisema kuwa kama atanichukua kunipeleka South Afrika basi akamilishe 
ishu ya kunivisha pete na kunioa kabisa, akanivisha pete mbele ya wazazi
 wangu wakakubaliana baada ya mwezi wangeleta mahali ’’ alisema  Jack.
‘’Tulivyofika South Afrika 
nilikuwa namfanyia kila kitu kama mke wa mtu, nilikuwa namdanganya mama 
nasoma lakini baada ya hapo nikaona mambo hayaendi kwa sababu kuna siku 
nilienda salun nikasikia kuwa mke wake naye yupo kule Sauz na alikuwa 
ananiaga sana anasafiri anaweza akakaa siku mbili au tatu nikamuuliza 
akaniambia sio kweli yupo Kongo’’ alisema Jack.
‘’Siku iliyofuata alikuja 
nyumbani akiwa amechelewa, nilikuwa chumbani yeye alikuwa sebuleni 
ana’preview’ picha nikataka kumpora simu nikamwambia nimeona picha ukiwa
 na mke wako, na mtoto wako, akaniambia alimkuta mwanamke wake kwa kaka 
yake akataka kupiga picha naye ndo akapiga, halafu alikuwa anavaa pete 
ya ndoa nikamwambia siitaki hiyo pete akaiuza, lakini kuna siku alirudi 
akiwa ameivaa ile pete nikakasirika nikamwambia naondoka akanitupia ile 
pete kitandani akaniambia nikaitupe chooni’’ alisema Jack.
‘’Kuna kipindi nilikuwa nalewa 
sana kutokana na stress, kuna siku nilikuwa ‘location’ nilikuwa nimelewa
 hadi nikazima akapigiwa simu akanifuata akanipeleka nyumbani akanivua 
nguo zote akaanza kunirekodi na kunipiga picha, lakini nilifanikiwa 
kuzifuta, lakini baada ya wiki mbili alinitumia meseji na kunitisha kuwa
 kitu atakachonifanya watanzania watafunga macho na sitoamini’’ 
Alimalizia Jack
Source: Clouds FM
 RSS Feed
 Twitter

1:41 AM
MZM
 Posted in 
0 comments:
Post a Comment