Saturday, June 27, 2015


Uchumi mbaya wazua wasiwasi Ugiriki
Mawaziri wa fedha wa mataifa ya ulaya wamekatalia mbali ombi la Ugiriki la kutaka iongezewa muda zaidi wa kulipa deni lake kutoka Jumanne ijayo.
Ugiriki ina hadi Jumanne ijayo kulipa deni lake la zaidi ya dola bilioni moja nukta saba.
Serikali ya Uigiriki chini ya Alexis Tsipras ilikuwa imeombamuda wa majuma mawili iliiandae kura ya maoni

Friday, June 26, 2015

 
Mtu mmoja amechinjwa Ufaransa
Mtu mmoja amechinjwa na mwengine akajeruhiwa vibaya baada ya shambulizi la kiislamu katika mji wa Lyon Ufaransa.
Vilipuzi kadhaa vilitegwa katika karakana moja iliyoko Saint-Quentin-Fallavier

Runinga ya taifa imepeperusha picha za shambulizi hilo
Watu wenye silaha wameshambulia hoteli moja ya kitalii iliyoko kwenye pwani ya Tunisia na kuwauwa watu 37.


Takriban watu 30 wamepoteza maisha yao baada ya shambulizi la kigaidi katika kituo cha kijeshi cha wanajeshi wa kimatifa wa kulinda amani nchini Somalia Amisom. 
Takriban watu 30 wamepoteza maisha yao baada ya shambulizi la kigaidi katika kituo cha kijeshi cha wanajeshi wa kimatifa wa kulinda amani nchini Somalia Amisom.

Thursday, June 25, 2015

 
 Makamu wa rais Burundi anaaminika kuwa ametorokea Ubeljiji 
Moja kati ya makamu wa rais wa Burundi ametoroka nchini humo baada ya kutangaza kuwa anapinga hatua ya rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu.
Makamu wa pili wa Rais wa Burundi Gervais Rufikiri amekimbia baada ya kuiambia runinga ya France24 kuwa muhula huo wa tatu unakiuka sheria na katiba ya taifa hilo.

Kiongozi wa ujasusi wa Rwanda anatarajiwa kufika mahakamani hivi leo

Kiongozi wa ujasusi wa Rwanda ameachiliwa kwa dhamana.
Luteni jenerali Karenzi Karake ametakiwa kufika kwenye kituo cha polisi kila siku.
Luteni jenerali Karenzi Karake alikamatwa siku ya jumamosi katika uwanja wa ndege wa Heathrow Jumamosi iliyopita chini ya kibali cha kukamatwa cha ulaya.

Tuesday, June 23, 2015


 
James Horner
James Horner, mtunzi nguli wa eneo maarufu kwa watu maarufu la Hollywood ambaye aliandika na kushinda katika tuzo za Oscar juu ya filamu maarufu ulimwenguni ya Titanic,amefariki dunia mjini California kutokana na ajali ya ndege akiwa na umri wa miaka 61.
James alipata mafunzo ya urushaji wa ndege,inaarifiwa alikuwa peke yake wakati alipopata ajali hiyo,na ndege binafsi ndogo ambayo alipata nayo ajali eneo la Kusini mwa Santa Barbara mwanzoni mwa wiki hii .
Mwandishi huyu na mtunzi wa tungo mbali mbali ametia mkono wake katika kazi tatu tofauti za filamu za msanii James Cameron , pamoja na filamu ya A Beautiful Mind, Braveheart, Troy na ile ya Apollo 13.katika utendaji kazi wake uliotukuka, James alipewa tuzo ya Oscar kwa filamu ya Titanic na wimbo uliotawala humo na nyinginezo .
James alipewa tuzo ya ushirika katika tuzo ya pili kwenye mashairi na msanii Will Jennings kwa wimbo bora wa asili , na kwa mafanikio makubwa waliyoyapata katika wimbo maarufu wa My Heart Will Go On, ambao uliimbwa na Celine Dion.
Ajali hiyo ilitokea katika msitu mzito wa taifa la Marekani wa Los Padres, Kaskazini mwa Los Angeles, wakati ndege hiyo ikidondoka ilitoa mshindo mkuu na kuripuka mara tu ilipotua aridhini moto ambao baadaye ulizimwa na kikosi cha wazima moto wa eneo hilo. Wanaeleza mashuhuda ambao ni wazima moto.
Msaidizi wa marehemu Horner , Sylvia Patrycja amethibitisha juu ya kifo hicho kwa kuandika kweny ukurasa wake wa facebook mwanzoni mwa wiki hii akisema kuwa: "tumempoteza mtu wa kipekee sana ambaye alikuwa na moyo mkuu wa kujitoa na mtu mwenye kipaji kisicho elezeka .amekufa wakati anafanya kitu akipendacho. Asante kwa mchango wako mkubwa na upendo uliokuwa nao tutaonana mbinguni ."

Bango lenye elimu kwa umma Sierra Leone
Maofisa wa afya nchini Sierra Leone wamesema kwamba kuna wagonjwa wawili wapya wanaougua ugonjwa wa ebola na kwamba wamegunduliwa katika mji mkuu wa nchi hiyo Freetown.
Hapo awali ilidhaniwa kwamba mji huo ulikuwa hauna maambukizi ya ugonjwa huo,na hakukuwa na wagonjwa walioripotiwa hapo kabla kwa muda wa wiki kadhaa.
Naye msemaji wa kituo cha karantini cha taifa hilo amesema kwamba kulikuwa na wasiwasi mkubwa kwasababu vituo vyote vya karantini na vitendea kazi vyake vilikuwa vimefungwa mjini Freetown.
Na akaongeza kusema kwamba kuna shaka kuwa kutatokea maambukizi mapya kutoka katika eneo lenye msongamano wa makazi duni.
Nako upande wa Kaskazini mwa nchi hiyo ya Sierra Leone unaendelea kupata maambukizi mapya ya ugonjwa.
 
Puff Dadddy
Mwanamuziki mashuhuri wa nyimbo za Hip hop P Diddy amekamatwa kwa kushukiwa kumshambulia mtu kwa silaha mjini Los Angeles.
Kisa hicho kinadaiwa kufanyika katika chuo kikuu cha California Jumatatu alasiri, mahala ambapo mwanawe wa kiume ni mmojawapo ya wachezaji katika timu ya soka ya Marekani.
Hayo ni kwa mjibu wa maafisa wa polisi.
Silaha hiyo ni kifaa cha chuma kilichoundwa kama mpira, ambacho kinajulikana kama kettlebell, na ambacho hutumika katika mafunzo ya unyanyuaji mizani.
Rekodi za jela zinaonyesha kuwa bwana Diddy ambaye jina lake kamili ni Sean Combs, aliachiliwa huru kwa dhamana ya dola elfu mia moja na sitini, mnamo Jumatatu jioni.
Maafisa bado hawajamtambua mhathiriwa aliyeshambuliwa ama kusema kilichosababisha shambulio hilo.
Mwanawe Combs, Justin Combs, alikuwa chuoni humo wakati wa tukio hilo.
Justin, amechezea timu ya soka ya Marekani UCLA, mechi kadhaa tangu ajiunge na chuo hicho yapata miaka mitatu iliyopita.
Mwanawe Snoop Dogg, Cordell Broadus pia anaichezea timu hiyo.


 Joto kali 

Waziri mkuu nchini Pakistan Nawaz Sharrif ametaka hatua za dharura kuchukuliwa huku idadi ya watu waliofariki kutokana na wimbi la joto katika mkoa wa kusini wa Sindh ikifikia 700.
Mamlaka ya kukabiliana na majanga ya dharura NDMA imesema kuwa imepokea maagizo kutoka kwa
Nawaz Sharrif kuchukua hatua za dharura.
null
 Joto kali 
Jeshi tayari limepelekwa katika eneo hilo kujenga vituo vya kukabiliana na joto hilo ili kuisaidia mamlaka hiyo.
Wengi wa waathiriwa ni watu wazima kutoka kwa familia zinazopata mapato ya chini.
null
 Joto kali 
Maafisa wa afya wanasema vifo vingi vimetokea katika mji mkuu wa Karachi ambao ulikumbwa na joto la viwango vya juu vya hadi digree 45 c.
Katibu wa afya katika mkoa wa Sindh Saeed Mangnejo amesema kuwa watu 612 walifariki katika hospitali kuu ya serikali mji huo katika kipindi cha siku nne zilizopita.
null
 Joto kali
Wengine 80 wameripotiwa kufariki katika hospitali za kibinafsi.

Sunday, June 21, 2015

 
Polisi
Askari polisi mmoja wa Israel, ameumia vibaya aliposhambuliwa kwa kisu katika eneo la mashariki mwa Jerusalem, ambalo linakaliwa na Israel.
Polisi wa Israel wanasema, walimpiga risasi na kumjeruhi kijana mdogo wa Kipalestina, aliyefanya shambulio.
Jambo hilo limetokea nje ya lango la asili, la Damascus Gate, la kuingilia mji wa kale.
Siku mbili zilizopita, mwanamume aliyekuwa na silaha, alimpiga risasi na kumuua mwanamume wa Israel, na kumjeruhi mwengine, katika ufukwe wa magharibi, unaokaliwa.
 
Mapigano makali yaendelea Mogadishu 
Mapigano makubwa yameripotiwa kwenye mji kuu wa Somalia Mogadishu baada ya shambulizi la gari la kujitoa mhanga kutokea karibu na makao makuu ya idara ya ujasusi ya nchi hiyo.
Maafisa nchini Somalia wanasema kuwa wapiganaji kutoka kundi la al-Shabab waliingia jengo lililo karibu na makao hayo makuu ya ujasusi, na kukana madai ya al-Shabab kuwa waliingia makao ya ujasusi yenyewe.
Hakuna ripoti zozote zilizotolewa za watu kuuawa au kujeruhiwa
Al-Shabab wameapa kuongeza mashambulzii dhidi ya serikali ya Somalia wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadan ambao ulianza siku ya Jumatano.

Saturday, June 20, 2015

 
Al Shabaab 
Wanamgambo wamewaua karibu walinda usalama 15 nchini Somalia baada ya kufanya shambulizi katika mji ulio karibu na mji mkuu Mogadishu.

 Maandamano mjini London
Maelfu ya watu wa Uingereza waandamana mjini London kupinga mpango wa serikali wa kubana matumizi.
 Majruhi wa ajali ya gari akihudumiwa
Polisi wa Austria wanasema kuwa mtu mmoja aliendesha gari lake kwa kasi na kutumbukia kwenye kundi la watu waliokuwa wakitembea kwa miguu katikati ya mji wa kale wa Graz, na kuuwa watu watatu.

Friday, June 19, 2015

 
Hospitali moja mjini Stockholm nchini Sweden inatarajiwa kufungua kliniki ya kwanza ya wanaume waliobakwa.
 
Kanisa la Charleston 
Utumizi wa neno ''uhalifu wa chuki'' ili kuelezea mauaji ya watu tisa katika kanisa moja la watu weusi mjini Carolina Kusini nchini Marekani umezua mjadala kuhusu ni nini haswa kinachosababisha mtu kutekeleza ugaidi.
 
Mtu aliyekunywa pombe haram akihudumiwa 

Watu wapatao 35 wamekufa katika mji wa Mumbai nchini India baada ya kunywa pombe haramu.
Wengi wao wamelazwa hospitali.

Thursday, June 18, 2015

 
Mfanyibiashara tajiri zaidi barani Afrika kutoka Nigeria Aliko Dangote amesema kuwa anapania kununua klabu ya Arsenal ya Uingereza.
Bilioneya huyo mmiliki wa kampuni ya kusafisha mafuta nchini Nigeria amesema fedha atakazopata kutoka kwa mauzo ya mijengo