Kanisa la Charleston
Utumizi wa neno ''uhalifu wa chuki''
ili kuelezea mauaji ya watu tisa katika kanisa moja la watu weusi mjini
Carolina Kusini nchini Marekani umezua mjadala kuhusu ni nini haswa
kinachosababisha mtu kutekeleza ugaidi.
Watu wengi wameonyesha
hasira zao kuhusu vile afisa mkuu wa polisi mjini Charleston
alivyoelezea kisa hicho wakati wa mkutano na vyombo vya habari.
Mshukiwa wa mauaji ya watu tisa akiandamana na maafisa wa polisi
Wanasema kuwa ''uhalifu wa kivita'' sio neno zito linalofaa kutumika
kuelezea kisa hicho na kudai kwamba iwapo waathiriwa wangekuwa watu
weupe na mshukiwa kuwa mwenye asili ya Asia,ama mweusi neno ugaidi
lingetumika.Mshukiwa Dylan Roof ,mwanamume mwenye umri wa miaka 21 ameshtumiwa kwa kuingia ndani ya kanisa saa tatu za usiku siku ya jumatano na kuwapiga risasi waumini waliokuwa katika maombi.
Mshukiwa wakati alipokuwa akiingia kanisani
Mwanaharakati Martin Luther King na Coretta Scott wote walizungumza katika eneo hilo.
0 comments:
Post a Comment