WAKILI
 Felix Kiprono aliyegonga vichwa vya habari baada ya kutoa azma yake ya 
kumuoa bintiye Rais Barack Obama, Malia sasa ametangaza kuwa ameamua 
kujiunga na dini ya Kiislamu.
Kiprono,
 24 aliambia Taifa Leo katika mahojiano kuwa atalichukua jina la 
Kiislamu la Adnan punde tu atakapomaliza masomo yake ya dini yaitwayo 
Tawhid.
“Natarajia kuyamaliza masomo yangu ya Tawhid niliyoyaanza mwaka wa 2012 nilipopewa cheti cha kubadili dini,” alisema Kiprono.
“Binti
 huyo alinifunza mengi kuihusu dini hiyo na nilipokata kauli kusilimu 
akanijulisha kwa masheikh na nikapata cheti katika Msikiti wa Jamia 
jijini Nairobi,” aliongeza.
Kiprono
 alisema atakamilisha mafunzo ya dini mwezi Oktoba na baadaye 
kuyabadilisha majina kwenye stakabadhi zake ili kuliongeza jina la 
Kiislamu, Adnan.
Aliongeza kuwa amekuwa akiyafuata maadili na mafunzo ya dini hiyo na hata kufunga katika mwezi mtukufu wa Ramadhan.
“Nimepata amani tele kwa kujiunga na dini hii na hivyo sitarajii kubatili uamuzi wangu kamwe,” alisema Kiprono.
Wakili
 huyo aligonga vichwa vya habari miezi za mwanzo wa 2015 alipotangaza 
kuwa angetaka kumuoa bintiye Rais Obama na kulipa mahari ya ng’ombe 50, 
kondoo 70 na mbuzi 30, kiwango alichosema kimewekwa na utamaduni wa 
kabila analotoka.
Kusubiri mwaliko rasmi
Aidha,
 wakili huyo amebatili uamuzi wake wa kukutana na Rais Obama atakapofika
 nchini Kenya wiki ijayo kwani amesema kuwa atasubiri kualikwa na 
mashemeji wake watarajiwa.
“Katika
 mila zetu kama waafrika mwanamume hana uhuru wa kukutana na mashemeji 
wake bila mpangilio maalum kutoka kwa wazee wa kijiji hivyo sitamtafuta 
Rais Obama atakapokuwa nchini kwani nina Imani ombi langu alilipata na 
atalishughulikia,” alisema Kiprono.
Kiprono aliongeza kuwa hatomtafuta pia bintiye Rais kwani ni msichana mdogo ambaye hajatimiza umri wa kufanya uamuzi wa ndoa.
“Angali
 msichana mdogo na hivyo kufanya urafiki wa kimapenzi naye itakuwa ni 
kukiuka sharia hivyo nitasubiri uamuzi wa wazazi wake,” alisema Kiprono.
Wakili huyo anaendelea na masomo ya uzamili wa sheria katika chuo kikuu cha Oxford Uingereza.
 RSS Feed
 Twitter

11:18 PM
MZM

 Posted in 
0 comments:
Post a Comment