RAIS WA MAREKANI
BARRACK OBAMA AMEKAMILISHA ZIARA YAKE YA SIKU TATU NCHINI KENYA AMBAPO
ALIFUNGUA KONGAMANO LA KIBIASHARA AKAWAHUTUBIA WAKENYA KATIKA UWANJA WA
KASARANI NA BAADAYE KUZUNGUMZA NA VIONGOZI WA MASHIRIKA YA KIJAMII
KATIKA CHUO KIKUU CHA KENYATTA
16.10pm:Ndege iliombeba rais wa Marekani Barrack Obama imewasili katika uwanja wa ndege wa JKIA jijini Nairobi.
15.46pm:Msafara wa rais Uhuru Kenyatta umewasili katika uwanja wa Jomo Kenyatta tayari kumuaga rais Obama aliyewasili nchini siku ya ijumaa.
15.43pm:Msafara wa Rais Uhuru Kenyatta waonekana ukielekea katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta kumuaga rais Obama.
14.55pm:Obama amaliza mkutano wake na makundi ya kijamii katika chuo kikuu cha Kenyatta.
14.49pm:Obama:Iwapo kuna sheria ambazo zinatoa fursa kwa jamii kujieleza huchangia ukuwaji wa kimaendeleo.Tutaziangazia sheria zinazojaribu kuwazuia watu wengine kuzungumza.SWala la kigadi halifai kuchukuliwa kuyazima makundi ya kijamii ambayo ni halali.
14.34pm:Sisters Without Borders-Serikali inafaa kuwashirikisha wanawake katika harakati za kukabiliana na utovu wa usalama.Licha ya harakati zetu katika swala hilo serikali bado haijatilia mkazo swala la thuluthi moja ya wanawake katika kila sekta.
14:29pm:SUPKEM-Viongozi wa Kiislamu pia wameshirikishwa katika kukabiliana na ugadi pamoja na ukandamizaji ikiwemo ukosefu wa vitambulisho kwa vijana wa kiislamu.
14:26pm:SUPKEM-Hassan Olenaado:Tumezungumza na serikali kuhusu kuanza mikutano ya kukabiliana na itikadi kali
14.05pm:Habari njema nchini Kenya ni kwamba kuna katiba mpya ambayo inatoa mwongozo.Baadaye alifungua mjadala wazi katika kikao hicho.
14.02pm:Makundi ya kijamii yalijitokeza baada ya raia kujitokeza na kuanza kuzungumzia maswala yanayowaathiri
13.50pm:Obama awasili katika chuo kikuu cha Kenyatta na sasa anawahutubia viongozi wa makundi ya kijamii
12.42pm:Obama amaliza hotuba yake kwa kusema 'Thank you Asante sana'
12.41pm:Amesema kuwa vijana wamemfanya yeye kujisikia nyumbani.
12:35pm:Amewataka wakenya kutokubali kugawanywa katika misingi ya kikabila na kidini.
12:33pm:Amesema kuwa Marekani itashirikiana kwa hali na mali na kenya kukabiliana na tatizo la ugiadi.'Magaidi ni waoga ndio maana hupendelea kutafuta makundi madogo madogo ya kijamii na kujaribu kuyagawanya''.Amesisistiza kuwa ugaid ni sharti ukabiliwe kwa hali yoyote.
12.32pm:Amesema kuwa ni sharti wanawake wapewe nafasi sawa katika jamii.'Udhalilishaji wa wanawake ni utamaduni ambao umekuwa tangu zamani lakini sasa hauna nafasi katika maisha ya sasa .Wanawake na wasichana ni sharti waelemishwa,Amesema kuwa kuna ufanisi mkubwa katika jamii ambayo imewaelemisha wanawake wake.Tuwape wasichana wetu elimu.Tunapowaelimisha wanawake tunawapatia nguvu kuzaa watoto walioelimika.
12.25pm:Amasema kuwa harakati za kukabiliana na ufisadi lazima zianze kuanza juu na kwamba sheria za kukabiliana na janga hilo ni sharti ziwekwe,huku akiwataka wananchi kusimama kidete na kukataa ufisadi.
12.23pm:'Ufisadi ndio janga linalozuia mataifa mengi kupiga hatua'.Amesisitiza kuwa iwapo Ufisadi hautakabiliwa vilivyo utaathiri maendeleo ya taifa kwa jumla
12.17pm:Amesema kuwa Marekani ni mshirika wa karibu na rafiki mkubwa wa Marekani na hivyobasi itaendelea na ushirikiano huo kupitia kuhakikisha kuwa kuna uongozi mzuri nchini Kenya.
12.15pm:'Siasa za kikabila na za kibaguzi hazina mwelekeo na hazifai kuendelezwa',alisema Obama
12.14pm:Ufisadi-amesema kuwa unafaa kukabiliwa kwa njia mbali mbali kwa kuwa unawadhulumu wakenya wa kawaida pato lao la kila siku.
12.11pm:Amesema kuwa wakenya walikataa kugawanywa katika misingi ya kikabila huku sauti za viongozi na makundi ya kijamii yakisababisha kupitishwa kwa katiba mpya
12.09pm:Uwezo wa vijana na maendeleo yaliopigwa na kenya ni fursa nzuri kwa vijana kujiendeleza wakati wowote.
12.06pm:Babu yangu alikuwa mpishi wa wakoloni.Obama alieleza vile alivyoweza kupata elimu.
12.04pm:'katika uwanja wa ndege mwanamke mmoja aliona jina langu na kuniuliza iwapo ninahusiana na Mtu anayemjua kwa jina Barrack Obama,na hapo ndipo nilijua kuwa jina hilo ni muhimu'
12.00pm:Auma amkaribisha Obama
11.56am:Auma amewakumbusha wakenya kwamba rais Obama yuko hapa kikazi licha ya kuwa mwana wa kenya.
11.53am:Awahutubia wakenya kuhusu dhifa ya hapo jana ambapo anasema kuwa rais huyo wa Marekani alikula vyakula vya aina mbali mbali vya kienyeji licha ya kukaa Marekani kwa muda mrefu.
11.30am: Obama-Rais Barrack Obama wa Marekani pia amedaiwa kufika katika maeneo ya uwanja wa kasarani jijini Nairobi na wakati wowote kuanzia sasa atakaribishwa na mwenyeji wake Uhuru Kenyatta ndani ya Ukumbi huo.
11.25am:Uhuru awasili Ukumbini
11.10am:Ukumbi wa Kasarani
11.05am:Usalama Kasarani
11.01am:Obama akicheza densi
HABARI YA ASUBUHI -JUMAPILI TAREHE 26-JULY.
0 comments:
Post a Comment