Maofisa
 wa ulinzi nchini marekani wamekiri kuwa maabara kadhaa zilizopokea 
kimakosa sampuli hai za vidudu hatari vya kimeta ni zaidi ya mara mbili 
ya matarajio ya awali.
Pentagon imesema vifaa hamsini na moja 
katika majimbo kumi na saba nchini Marekani, pamoja na maabara zilizopo 
nchini Canada, Australia na Korea kusini walitumiwa sampuli hizo kutoka 
maabara ya jeshi la marekani.Imesema usafirishaji wa vijidudu hivyo vilianza miongo kadhaa iliiyopita na iliendelea mpaka wiki iliyopita.
Hadi sasa hakuna mtu aliyeathirika lakini zaidi ya watu ishirini walikuwa wakibeba sampuli hizo wamekuwa wakitibiwa kwa tahadhari tu.
 RSS Feed
 Twitter

1:29 AM
MZM

0 comments:
Post a Comment